Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,559
- 3,953
Mgombea ubunge wa Jimbo la Uyole mkoani Mbeya, ambaye pia ni Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, ametoa wito kwa wananchi wa jimbo hilo kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kutimiza haki yao ya msingi ya kikatiba.
Dkt. Tulia ameyasema hayo leo Oktoba 29, 2025, mara baada ya kupiga kura katika Kituo cha Tambukaleli, ambapo amepongeza mwamko mkubwa wa wananchi waliojitokeza mapema asubuhi kushiriki zoezi hilo huku kukiwa na hali ya amani na utulivu.
Amesisitiza kuwa Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kulinda usalama wa wananchi na siyo kuwatisha, hivyo wananchi waendelee kujitokeza kwa utulivu na nidhamu kutekeleza wajibu wao wa kiraia.
Dkt. Tulia ameyasema hayo leo Oktoba 29, 2025, mara baada ya kupiga kura katika Kituo cha Tambukaleli, ambapo amepongeza mwamko mkubwa wa wananchi waliojitokeza mapema asubuhi kushiriki zoezi hilo huku kukiwa na hali ya amani na utulivu.
Amesisitiza kuwa Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kulinda usalama wa wananchi na siyo kuwatisha, hivyo wananchi waendelee kujitokeza kwa utulivu na nidhamu kutekeleza wajibu wao wa kiraia.