JACOB MAKAME
New Member
- Jun 23, 2014
- 2
- 0
Kada wa CHADEMA DAUDI NTINONU leo majira ya saa sita mchana nusura ampige risasi Kiongozi wa Vijana wa Mkoa wa Geita aitwaye Neema Chozaile.
Ntinonu ambaye alikuwa ameongozana na Diwani viti mahalumu wa Nyamagana Bi Neema Mafuma na Elikana Paschael ambae ni mtumishi wa Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Ziwa Magharibi, mala tu baada ya kushuka katika gari la CHADEMA aina ya Ford ranger lenye no CDA 156 katika ofisi za jimbo la geita waliingia ofisini na kuanza kumtupia maneno makali ya uzalilishaji na kisha Ntinonu akatoa Bastola yake yenye rangi nyeusi na kutaka kumfyatua Neema.
Chanzo cha mzozo huo ni mambo ya kusikitisha kwani imebainika kuwa Ntinonu na Peter Makere[mkt Kanda] wanatumiwa na Kada wa CCM aitwaye Mabina ambaye ni ndugu wa Ntinonu na mtia nia waubunge CCM kutengeneza mtandao Jambo ambalo Kamanda Mawazo[mkt mkoa] na Viongozi wa Jimbo la geita akiwemo Rogers na Neema CHOZAIRE wamekuwa wakilipinga
========================================
Ntinonu ambaye alikuwa ameongozana na Diwani viti mahalumu wa Nyamagana Bi Neema Mafuma na Elikana Paschael ambae ni mtumishi wa Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Ziwa Magharibi, mala tu baada ya kushuka katika gari la CHADEMA aina ya Ford ranger lenye no CDA 156 katika ofisi za jimbo la geita waliingia ofisini na kuanza kumtupia maneno makali ya uzalilishaji na kisha Ntinonu akatoa Bastola yake yenye rangi nyeusi na kutaka kumfyatua Neema.
Chanzo cha mzozo huo ni mambo ya kusikitisha kwani imebainika kuwa Ntinonu na Peter Makere[mkt Kanda] wanatumiwa na Kada wa CCM aitwaye Mabina ambaye ni ndugu wa Ntinonu na mtia nia waubunge CCM kutengeneza mtandao Jambo ambalo Kamanda Mawazo[mkt mkoa] na Viongozi wa Jimbo la geita akiwemo Rogers na Neema CHOZAIRE wamekuwa wakilipinga
========================================
![]()
Freeman Mbowe
Mmoja wa wagombea kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anadaiwa kuwatishia wanachama wenzake kwa bastola baada ya kuibuka makundi yanayohasimiana ndani ya chama hicho.
Tukio hilo linadaiwa kutokea juzi katika kitongoji cha Mkoani kwenye viwanja vya ofisi ya serikali ya mtaa, muda mfupi kabla ya uchaguzi wa uongozi kata ya Kalangalala mjini.
Akithibitisha taarifa hiyo jana, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Peter Kakamba, alimtaja anayedaiwa kuwatishia wenzake kuwa ni Daud Ntinonu.
Walalamikaji katika tukio hilo ni Neema Chozaire (25), Elikana Gideon (30) na Duba Jackson (35).
Walalamikaji hao wamefungua jalada namba GE/RB/5301/2014 la kutishiwa na bastola. ''Ni kweli taarifa ipo na tayari uchunguzi umeanza wa kumtafuta mtuhumiwa…tukimpata tutamhoji na upelelezi ukikamilika tutawasilisha jalada kwa mwanasheria mkuu wa serikali, hilo ndilo jukumu letu," alisema Kakamba.
Hata hivyo, alisema bastola inayodaiwa kutumika itafahamika baada ya upelelezi kukamilika.
Awali akizungumzia madai hayo, Chozaire alisema tukio hilo lilitokea juzi kati ya saa 5:30 asubuhi katika mtaa wa Mkoani, baada ya kutokea kutoelewana kati yake na mtuhumiwa pamoja na wapambe wake kwa kutomuunga mkono.
"Wakati watu walipojitokeza kuamua ugomvi, Ntinonu alitoa bastola yake na kunielekeza kichwani, lakini baadhi ya watu waliingilia kati kumzuia," alisema Chozaire.
Chozaire ambaye ni Mratibu wa Baraza la Vijana mkoa wa Geita (Bavicha), alikiri kuwapo makundi yanayolumbana ndani ya Chadema akihofiwa ni mamluki baada ya kuhamia chama hicho akitokea CCM.
Akizungumzia tuhuma hizo, Ntononu, aliyewahi kuwa mwenyekiti wa CCM wilaya ya Geita kabla ya kuhamia Chadema, alikanusha tuhuma hizo.
Malumbano ndani ya chama hicho mkoani hapa, yamechukua sura mpya baada ya uongozi wa kanda kutoa tamko la kumvua uongozi aliyekuwa katibu wake wa wilaya, Rogers Luhega, aliyewania ubunge jimbo la Geita 2010.
CHANZO: NIPASHE