Candela
JF-Expert Member
- Aug 12, 2021
- 857
- 2,289
Hivi juzi nilipokea simu kutoka kwa ndugu huko mkoani. Akisema amepata kibarua mkoa nilipo hivyo anaomba aje akae kwangu.
Nilimkaribisha lakini nikamwambia mimi naishi kibachela nyumbani sipiki akasema ye anataka pa ku lala tu.
Alipofika akaanza kusema vyakula vya hotel hivi mara vile bora awe anapika. Akataka anunue gesi nikamwambia acha ntanunua(sikutaka akiondoka aseme aliacha gesi kwangu).
Huyu kijana kapika wiki kama 3 hivi kafulia na mimi sijawah kula akipika.
Sasa analalamika kwa ndugu zake mimi simjali narudi nimekula sijui kama amekula au laa. Kwa kifupi anataka nimlee kama familia na mimi nilishamwambia toka mwanzo nakula kwa mkopo mda mwingine ndio maana sipiki hata kama sina hela nakopa kwa mama ntilie. Huyu nimtimue au nifanyeje?
Nilimkaribisha lakini nikamwambia mimi naishi kibachela nyumbani sipiki akasema ye anataka pa ku lala tu.
Alipofika akaanza kusema vyakula vya hotel hivi mara vile bora awe anapika. Akataka anunue gesi nikamwambia acha ntanunua(sikutaka akiondoka aseme aliacha gesi kwangu).
Huyu kijana kapika wiki kama 3 hivi kafulia na mimi sijawah kula akipika.
Sasa analalamika kwa ndugu zake mimi simjali narudi nimekula sijui kama amekula au laa. Kwa kifupi anataka nimlee kama familia na mimi nilishamwambia toka mwanzo nakula kwa mkopo mda mwingine ndio maana sipiki hata kama sina hela nakopa kwa mama ntilie. Huyu nimtimue au nifanyeje?