Napenda kutoa MASIKITIKO yangu makubwa kwa mgawo wa umeme Jijini Mwanza jinsi unavyokera na kuleta usumbufu mkubwa kwa wananchi. Kwanza kama kuna mgawo wa umeme tunatakiwa kutangaziwa kwenye vyombo vya habari au kupitia magari ya matangazo. Hapa Mwanza maeneo ya Nyakato, Mwananchi sasa imekuwa kawaida umeme kukatwa kuanzia saa moja na nusu asubuhi mpaka saa kumi na mbili jioni na kukatwa tena saa moja jioni mpaka saa nne usiku. Wenyewe wanajua fika kuwa umeme ndiyo maisha kwa kila kitu ukianzia matumizi ya nyumbani kama kupika, kupiga pasi, kuchemsha maji, vyakula kwenye friji, redio, TV, kutengeneza barafu kwa ajili ya sisi wanyonge na kusukuma maji n.k. Hapa nilipo hakuna hata tone la maji kwenye mabomba ya majumbani na kila kitu ni hovyo. Hakuna maji kwa ajli ya matumizi ya nyumbani na hii yote inasabishwa na TANESCO. Tuelezwe wazi kama nchi IMEFILISIKA ili tujue moja. Wakati wa Prof. Muhongo kukatika katika kwa umeme Jijini Mwanza ilikuwa ni ndoto. Tutamkumbuka Prof. kwa msimamo aliokuwa nao kwenye Wizara ya Nishati.