Nawaza kwamba mfumo wa Elimu ya msingi hapa Tanzania unashida.
Unahitaji marekebisho makubwa.
1. Naona kwamba ufumo huu una upungufu mkubwa katika matumizi ya Lugha.
Kuendelea kusisitiza matumizi makubwa ya Lugha ya KISWAHILI, naona ni kuwazuia wasomi wetu kuwa washindani wazuri kwenye viwango vya kimataifa.
Lugha ya Kiingereza ni pendekezo langu.
Bwana Exaud, ninakubali kabisa na. 2-4 kati ya mapendekezo yako. Sikubali kuhusu swali la Kiswahili kuwa kizuizi kwa wototo kwenye uwanja wa kimataifa.
A Kwanza kabisa mwanafunzi anayemaliza darasa la saba hatashindana kwenye ngazi ya kimataifa.
B Pili mtoto atajenga akili vizuri zaidi katika lugha yake au angalau katika lugha inayoeleweka kirahisi kwake - hii ni Kiswahili si Kiingereza.
C Mafundisho ya msingi kwa lugha ya kigeni yataacha wanafunzi wengi kubaki nyuma, ni wachache tu wanaoweza kusogea mbele.
D mifano mingi ya kimataifa yanaonyesha ya kwamba watoto wanaopata elimu ya msingi kwa lugha ya nyumbani hawana matatizo kujifunza lugha ya kigeni (kama Kiingereza, kifaransa, n.k.) wakifaulu kutumia Kiingereza kushinda wanafunzi Watanzania. Linganisha wanafunzi Wajerumani au Wasweden wa ngazi ya A-level jinsi wanavyojua Kiingereza na wanagunzi wa A-level wa Tanzania - ingawa wale Wajeumani au Wasweden wanajifunza masomo yao kwa lugha yao isipokuwa Kiingereza kama somo tu. Huko ni pia wengi wanaofaulu masomo mengine kushinda Watanzania.
E Je umeshawahi kutafakari ya kwamba matokeo mabaya ya hisabati katika Afrika ya Mashariki ni tokeo la Kiingereza kama lugha ya mafunzo kwa walimu wasiojua lugha ile ya kutosha? Ya kwamba hali ya kujifunza kwa lugha ya kigeni inakwamisha akili ya walimu na pia ya wanafunzi?