Beira Boy
JF-Expert Member
- Aug 7, 2016
- 17,895
- 25,945
Amani iwe nanyi wapendwa katika bwana,
Mwanamke mmoja anayekwenda kwa jina Milembe ambaye ni Afisa wa mgodi wa Geita anayehusika katika kitengo cha manunuzi amekamatwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumuoa mwana mke mwenzake had kumvisha pete ya uchumba.
Jeshi la polisi linamshilikia mwanamke huyo kwa kosa la kumuoa mwanamke mwenzie na kumuvisha pete, jeshi la polisi limesema kitendo hicho ni kinyume cha sheria na nchi hairuhusu mambo hayo.
LONDON BABY
======================================
Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mtumishi wa mgodi wa GGM, Milembe Suleiman anayetuhumiwa kujihusisha na mapenzi ya jinsi moja.
Mfanyakazi huyo ambaye ni Afisa Ugavi kitengo cha manunuzi anashikiliwa baada ya ‘video’ inayomwonyesha akimvisha pete ya uchumba mwanamke mwenzake kusambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
Video hiyo ambayo imezua mijadala hasa ikizingatia kwamba iko kinyume cha utamaduni wa Kitanzania na Serikali ambayo imekuwa ikikemea na kupiga marufuku vitendo vya mapenzi ya jinsi moja.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo amesema wanamshikilia kwa uchunguzi kwa kuwa nchi hairuhusu mambo hayo.
Ofisa Habari wa GGM, Dili Tenga amesema hayo ni masuala binafsi ya mfanyakazi hivyo wao kama mgodi hawawezi kuyazungumzia lakini wanaviachia vyombo vya dola viendelee na uchunguzi wake.
Mwananchi
Mwanamke mmoja anayekwenda kwa jina Milembe ambaye ni Afisa wa mgodi wa Geita anayehusika katika kitengo cha manunuzi amekamatwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumuoa mwana mke mwenzake had kumvisha pete ya uchumba.
Jeshi la polisi linamshilikia mwanamke huyo kwa kosa la kumuoa mwanamke mwenzie na kumuvisha pete, jeshi la polisi limesema kitendo hicho ni kinyume cha sheria na nchi hairuhusu mambo hayo.
LONDON BABY
======================================
Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mtumishi wa mgodi wa GGM, Milembe Suleiman anayetuhumiwa kujihusisha na mapenzi ya jinsi moja.
Mfanyakazi huyo ambaye ni Afisa Ugavi kitengo cha manunuzi anashikiliwa baada ya ‘video’ inayomwonyesha akimvisha pete ya uchumba mwanamke mwenzake kusambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
Video hiyo ambayo imezua mijadala hasa ikizingatia kwamba iko kinyume cha utamaduni wa Kitanzania na Serikali ambayo imekuwa ikikemea na kupiga marufuku vitendo vya mapenzi ya jinsi moja.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo amesema wanamshikilia kwa uchunguzi kwa kuwa nchi hairuhusu mambo hayo.
Ofisa Habari wa GGM, Dili Tenga amesema hayo ni masuala binafsi ya mfanyakazi hivyo wao kama mgodi hawawezi kuyazungumzia lakini wanaviachia vyombo vya dola viendelee na uchunguzi wake.
Mwananchi