Meneja wa Teknolojia wa tume ya uchaguzi Kenya IEBC atoweka

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
f057daae34e6976fb487c650af9e8d3a.jpg
Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya IEBC, imesema kuwa mmoja wa mameneja wake wa masuala ya teknolojia hajulikani aliko.

IEBC inasema kuwa mtu huyo alionekana mara ya mwisho siku ya Ijumaa jioni.

Mawasiliano ya mwisho kutoka kwa mtu huyo aliyafanya siku ya Jumamosi mwendo wa saa tisa alfajiri kupitia ujumbe wa sms na mmoja wa wafanyakazi wenzake.

Aliyoyaandika kwenye ujumbe huo yalionyesha kuwa alikuwa akijielewa na alikuwa na mipango ya siku.

Ripoti tayari imepelekwa kwa polisi huku IEBC, familia yake na pia polisi wakishirikiana kujaribu kubaini aliko.
Kisa hiki kinatokea ikiwa imesalia juma moja kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini Kenya ambao utafanyika tarehe 8 Agosti.

Chanzo: BBC
 
Mkuu.. Wala siyo siasa za Kenya tu bali Afrika kwa ujumla siasa zao ni za ajabu sana

Kwasababu uchu wa madaraka ni mkubwa zaidi kuliko uchu wa maendeleo, ambapo husababisha kutatiza usalama kwa raia wao.
Kupotea kwa watu muhimu nchini Kenya ni kwaida sana..

Mwaka juzi alipotea afisa mmoja wa usalama tena akiwa ikulu..

Mwaka Jana akapota na kukutwa kauawa wakili maarufu na mfanyabiashara maarufu nchini humo....

Mwaka huu angalia kifo cha utata cha aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani......

Hutu naye tena kiujumla Kenya si sehemu salama kwa sasa.......
 
Kupotea kwa watu muhimu nchini Kenya ni kwaida sana..

Mwaka juzi alipotea afisa mmoja wa usalama tena akiwa ikulu..

Mwaka Jana akapota na kukutwa kauawa wakili maarufu na mfanyabiashara maarufu nchini humo....

Mwaka huu angalia kifo cha utata cha aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani......

Hutu naye tena kiujumla Kenya si sehemu salama kwa sasa.......

Mwisho wa huo ujinga umefika!!!!!
 
Naona Jubilee wana hali Mbaya sana...kipindi hiki inaonyesha RAILA na NASA wamewabana kuanzia kwa wapiga kura adi upande wa Intelligence...Uhuru na Ruto wakicheza ICC itawahusu na this time hawatachomoka cz ata 2013 walifanya usanii hawakushinda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom