PreGE2025 Meneja wa Bandari ya Mtwara, Ferdinand Nyathi: Bilioni 434.5 kujenga Bandari ya Kisiwa Mgao

PreGE2025 Meneja wa Bandari ya Mtwara, Ferdinand Nyathi: Bilioni 434.5 kujenga Bandari ya Kisiwa Mgao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Meneja wa Bandari ya Mtwara, Ferdinand Nyathi amesema Serikali imegharamia na kuisadia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kusaini mkataba na Mkandarasi ambaye ni kampuni ya China Harbour Engineering ( CHEC) kwa ajili ujenzi wa Bandari ya Kisiwa Mgao kwa thamani ya shilingi bilioni 434.5.

Meneja wa Bandari ya Mtwara, Ferdinand Nyathi amesema Serikali imegharamia na kuisadia Mamlaka...jpg
Nyathi ameeleza hayo leo Aprili 04, 2025 wakati wa kongamano maalumu la miaka minne ya uongozi Rais Samia Suluhu Hassan, lililofanyika katika Ukumbi wa Benki Kuu mkoani Mtwara.

Amesema ujenzi wa bandari hiyo tayari umeanza kutekelezwa na mkandarasi yupo saiti, pia mradi huo utakapokamilika unatatajiwa kuwa kichecheo kikubwa cha uchumi wa ushoroba wa kusini hususani katika usafirishaji wa madini.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Bandari ya Kisiwa Mgao inajengwa Mtwara Vijijini na ni maalumu kwa ajili ya kusafirishia mizigo michafu kama makaa ya mawe, sulphur na saruji.

Aidha, Nyathi amesema Serikali imefanya upanuzi wa Bandari ya Mtwara kwenye maeneo ya gati, miundombinu ya barabara, mizani pamoja na mifumo ya TEHAMA

Pia Serikali ya awamu ya sita imegharamia ujenzi wa gati jipya kwa shilingi bilioni 157.8 ambalo lipo Bandari ya Mtwara, vifaa vya zaidi ya shilingi bilioni 100 na ununuzi wa boti ya kisasa kwa zaidi ya shilingi bilioni 20.
 
Huko Visiwani badala ya kujenga Bandari wangekodisha hata kwa kampuni zinazoendesha Cruise Ships ili vitumike kwa shughuli za kitalii.

Sasa una bandari Mtwara smbayo haijafikia kiwango cha juu cha efficiency yake alafu unawaza kujenga Bandari ingine visiwani huko.

Hivi hii nchi ukiwa kiongozi ndo unakosa akili namna hii?
 
Hakuna kisiwa ni sawa sawa kuita Ubungo Kisiwani ambayo ni Ubungo Maziwa.
Kasema ni bandari ya kusafirisha Mkaa wa Mawe,Saruji ni bidhaa in bulk form.
 
Huko Visiwani badala ya kujenga Bandari wangekodisha hata kwa kampuni zinazoendesha Cruise Ships ili vitumike kwa shughuli za kitalii.

Sasa una bandari Mtwara smbayo haijafikia kiwango cha juu cha efficiency yake alafu unawaza kujenga Bandari ingine visiwani huko.

Hivi hii nchi ukiwa kiongozi ndo unakosa akili namna hii?
Kama kawa, nyumbu likiwa na stress zake za kupigwa tone tone, limeshafika na kuponda bila hata kuyaelewa maelezo na mkakati uliopo. Sababu ya kujengwa imesemwa kwenye maelezo lakini nyumbu limekimbia haraka kuja kutoa comment itakayomfurahisha bwana'ake lissu akijiona.
 
Back
Top Bottom