VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Sijui viongozi wa CCM na Serikali kimewapata kitu gani.Kuna kauli zisizo na nauli.Kauli zimejaa kiburi na jeuri. Kauli zisizojaa hata kwenye bakuli. Hazieleweki.Hakibebeki.Haziambiliki. Mimi sijadili kauli ya Mwenyekiti wetu aliyoitoa Dodoma.Najadili kauli ya mmoja wa Mawaziri wa nchi hii na aliyehojiwa Dodoma kama mmoja wa 'waharibu chama. Waziri Benard Camilius Membe.
Unataka kujua kauli yenyewe? Utaiamini? Utaamini kama ameisema Waziri Membe? Ni kwamba, Waziri Membe alikitaka chama tawala-CCM kimteue mgombea wa Urais wake hadi ifikikapo Disemba mwaka huu. Yaani,uteuzi wa mgombea ufanyike kabla ya kuisha mwaka huu. Aisee!? Kauli hii kaitoa yeye.Imeripotiwa na baadhi ya magazeti leo hii (kama sikosei Mwananchi).
CCM sasa inataka kuvuka mipaka.Mipaka hadi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Jaji Damian Lubuva. Tume ya Uchaguzi ndiyo yenye dhamana ya kutangaza tarehe za kuanza mchakazo wa kiuchaguzi: kuchukua fomu,kuteuliwa na kadhalika. Si mwingine. Waziri Membe halijui jambo hili? Kauli yake inaonesha kujisahau au dharau. Si kauli nzuri.
Sasa chama kinayumba. Wanaohojiwa ndio wanaotoa kauli zilizo kinyume na Sheria na Taratibu za Uchaguzi. Nani aaminike chamani? Shime viongozi wangu,muwe na uchaguzi wa maneno kabla ya uchaguzi wa viongozi kichama na kiserikali!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Unataka kujua kauli yenyewe? Utaiamini? Utaamini kama ameisema Waziri Membe? Ni kwamba, Waziri Membe alikitaka chama tawala-CCM kimteue mgombea wa Urais wake hadi ifikikapo Disemba mwaka huu. Yaani,uteuzi wa mgombea ufanyike kabla ya kuisha mwaka huu. Aisee!? Kauli hii kaitoa yeye.Imeripotiwa na baadhi ya magazeti leo hii (kama sikosei Mwananchi).
CCM sasa inataka kuvuka mipaka.Mipaka hadi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Jaji Damian Lubuva. Tume ya Uchaguzi ndiyo yenye dhamana ya kutangaza tarehe za kuanza mchakazo wa kiuchaguzi: kuchukua fomu,kuteuliwa na kadhalika. Si mwingine. Waziri Membe halijui jambo hili? Kauli yake inaonesha kujisahau au dharau. Si kauli nzuri.
Sasa chama kinayumba. Wanaohojiwa ndio wanaotoa kauli zilizo kinyume na Sheria na Taratibu za Uchaguzi. Nani aaminike chamani? Shime viongozi wangu,muwe na uchaguzi wa maneno kabla ya uchaguzi wa viongozi kichama na kiserikali!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam