Meli ya Kinana na ujangili wake gumzo bungeni

rosemarie

JF-Expert Member
Mar 22, 2011
6,887
3,412
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, ametangaza upya vita dhidi ya majangili wa nyara za taifa na rasilimali nyingine nchini, huku akiwema wazi mpango wa kufanya doria 100,000 na kukunua ndege mbili katika mwaka ujao wa fedha kwa lengo la kuwakabili maadui hao wa maendeleo.

Waziri Kagasheki amesema licha ya changamoto kubwa ya kusimamia rasilimali za nchi hususan wanyamapori, wizara yake itaimarisha usimamizi na udhibiti kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola pamoja na wananchi.

Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake bungeni jana Jumanne mjini Dodoma, Waziri huyo alisema suala la doria na udhibiti wa ujangili limekuwa changamoto kubwa na kwamba serikali kupitia wizara yake haitashindwa kuwadhibiti.

"Wizara itaendelea kuimarisha usimamizi wa rasilimali za wanyamapori kwa kuendelea kufanya doria ndani na nje ya mapori ya akiba kwa kuendesha doria - siku 100,000. Miundombinu, vitendea kazi na huduma vitaboreshwa kwa watumishi katika vituo 27 kwenye mapori ya akiba na kanda nane za vikosi dhidi ya ujangili," alisema Waziri Kagasheki.

Alisema biashara ya uvunaji haramu wa mazao ya misitu na nyuki itadhibitiwa zaidi kwa kuongeza doria 20,700 katika maeneo ya nchi kavu na majini pamoja na kudhibiti viwango vya ubora wa mazao ya misitu na nyuki ili kuongeza thamani yake na kuongeza mapato ya nchi.

Kuhusu maboresho ya maeneo ya kufikia watalii alisema wizara yake kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) itajenga nyumba 29 katika hifadhi tisa za Arusha, Katavi, Kilimanjaro, Mikumi, Mkomazi, Ruaha, Rubondo, Serengeti na Udzungwa pamoja na kujenga barabara mpya zenye urefu wa kilomita 115 katika mwaka ujao wa fedha 2013/2014.

"Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro itajenga jengo moja la familia sita za wafanyakazi, jengo la mapokezi uwanja wa ndege wa Ndutu, jiko kwenye kambi ya kulala wageni ya Simba A pamoja na nyumba moja ya Askari eneo la Lositete. Mamlaka itaendelea na ujenzi wa jengo la kitega uchumi (kwa ubia) lenye gorofa 10 mjini Arusha,"alisema Waziri Kagasheki ambaye hotuba yake ya bajeti kwa Wizara ya Maliasili na Utalii imechapishwa katika gazeti hili.

Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Mali Asili na Mazingira, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bw. James Lembeli, alisema kamati yake imesikitishwa na tatizo kubwa la ujangili wa tembo unaozidi kukua badala ya kupungua.

"Kwa sasa ujangili wa tembo umekuwa ni janga la kitaifa, ni ukweli usiofichika kwamba leo hii si tu tembo wanauawa bali wanateketezwa, kwa mujibu wa tafiti zilizokwishafanywa na taasisi za utafiti wa wanyamapori nchini takwimu zinazoshabihiana na za taarifa za utafiti wa kimataifa zinaonesha kwamba tembo wasiopungua 30 wanauawa kwa siku, 850 kwa mwezi na tembo 10,000 kila mwaka,"alisema Bw. Lembeli.

Wakati huo huo, Siasa zenye dalili za kuchafuana kwa malengo ya kisiasa zimeibuka bungeni na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahaman Kinana, akijikuta katikati ya siasa hizo, kabla ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi, kusimama na kulitaka Bunge kuepuka kuhusishwa na uongo.

Ni kama vile ulikuwa mpambano kati ya wabunge wa CHADEMA wakiongozwa na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa na wabunge wa CCM, wakiongozwa na Waziri Dk. Nchimbi ambako mivutano ya hoja zilizomhusisha Kinana bungeni huku Spika wa Bunge, Anne Makinda aliamua kuweka kuachia kwa muda kila upande ukamilishe mashambulizi dhidi ya upande mwingine na kisha upande ulioshambuliwa ujibu mapigo.

Katika kuacha mashambulizi na kujibu mapigo kuchukue nafasi yake, Spika alisikika akisema; "Nyingi (wapinzani) mlivyokuwa mkizungumza (kuporomosha mashambulizi) wenzenu walinyamaza wakiwasilikiza."

Katika hoja zake, Msigwa alidai Kinana anahusika katika biashara haramu ya pembe za ndovu akigusia tukio la mwaka 2009 ambako shehena ya pembe za ndovu zenye uzito wa tani 4 kutoka Tanzania na Kenya ziliripotiwa kukamatwa na vyombo vya usalama vya Vietnam akiitaja kampuni ya wakala wa meli ya Sharaf Shipping Co. Ltd inayomilikiwa na familia ya Kinana.

Waziri Nchimbi alianza kwa kueleza namna Wizara ya Maliasili na Utalii inavyofanya jitihada kutimiza majukumu yake na kwa sababu Waziri kivuli, Mchungaji Peter Msigwa alidai hakuna cha maana kilichofanyika, Nchimbi alisema anaamini mtu wa namna hiyo (aina ya Msigwa) upeo wake wa uelewa una utata mkubwa na baadae kufafanua tuhuma dhidi ya Kinana.

Nchimbi alisema wahusika walikwisha kufikishwa mahakamani na kwamba Msigwa na viongozi wenzake wa upinzani wanafahamu tofauti kati ya kampuni ya Uwakala wa Meli (Shipping Argent) na Kampuni ya Kupeleka na Kuingiza Mizigo (Clearing and Forwading Co. Ltd).

Pamoja na Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) Tundu Lissu kutaka kumzuia Nchimbi kujibu tuhuma, Spika Anne Makinda alipuuza na kumtaka Nchimbi kuendelea kuzungumza akisema; "wakati Msigwa anatoa tuhuma dhidi ya Kinana na makada wengine wa CCM, aliachwa ahitimishe tuhuma zake bila kuingiliwa."

Nchimbi aliwataja waliokamatwa na kufunguliwa kesi ni pamoja na Ladislaus Tesha, Gabriel Chambo, Shaaban Yasin, Erick Leo (anayedaiwa kuwa Mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato eneo la Bandari ya Dar es Salaam), Issa Ahmed, Norbert Kiwale na Aboubakar Omar Hassan.

Nchimbi alilieleza Bunge ya kuwa kesi dhidi ya watuhumiwa hao ilifunguliwa katika Mahakama ya Kisutu lakini ilisimamishwa kwa muda ili kupata ushahidi kutoka nchi ya Vietnam na kwamba Vietnam ilikataa kutoa ushahidi kwa maelezo kuwa haina mkataba na Tanzania katika ushirikiano dhidi ya makosa ya jinai lakini kumekuwa na jitihada za kupata kibali cha mpito cha mkataba huo kutoka China ili kupata ushahidi na kesi hiyo iweze kuendelea katika Mahakama ya Kisutu
 
Kinana ni jangili kama wanataka ushaidi waje arusha.wapo watu walio bebaga pembe hizo miaka ya 80 na kuipeleke burundi enzi hizo kabla ya kuamishia njia ya dar.kuanzia miaka ya 89 na95 alikuwa anafanya biashara ya mandrax kutoka pakstan alikuwa anapitishia KIA alikuwa anapitishiwa na albat wa dahaco na kumkabidhi msamba mmoja mwenye jina la tahiri wa mbuguni ambaye wameishi na waakina kinana na ahmed tangia wakiwa wadogo na kuipeleke kwa kinana kordo area kwenye nyumba ya kinana iliokuwa inalindwa na jeshi.CCM ikitaka aibu iendele kumkumbatia waone tutaanika mambo yake yote na tuna muitaji msigwa tumpe historia nzima na tutamkutanisha wale wote waliowahii kufanya hizo kazi kwa kinana.
 
wajinga waje wabishe sasa....! mwanangu wakikuudhi wataje!
Kinana ni jangili kama wanataka ushaidi waje arusha.wapo watu walio bebaga pembe hizo miaka ya 80 na kuipeleke burundi enzi hizo kabla ya kuamishia njia ya dar.kuanzia miaka ya 89 na95 alikuwa anafanya biashara ya mandrax kutoka pakstan alikuwa anapitishia KIA alikuwa anapitishiwa na albat wa dahaco na kumkabidhi msamba mmoja mwenye jina la tahiri wa mbuguni ambaye wameishi na waakina kinana na ahmed tangia wakiwa wadogo na kuipeleke kwa kinana kordo area kwenye nyumba ya kinana iliokuwa inalindwa na jeshi.CCM ikitaka aibu iendele kumkumbatia waone tutaanika mambo yake yote na tuna muitaji msigwa tumpe historia nzima na tutamkutanisha wale wote waliowahii kufanya hizo kazi kwa kinana.
 
Kinana ni jangili kama wanataka ushaidi waje arusha.wapo watu walio bebaga pembe hizo miaka ya 80 na kuipeleke burundi enzi hizo kabla ya kuamishia njia ya dar.kuanzia miaka ya 89 na95 alikuwa anafanya biashara ya mandrax kutoka pakstan alikuwa anapitishia KIA alikuwa anapitishiwa na albat wa dahaco na kumkabidhi msamba mmoja mwenye jina la tahiri wa mbuguni ambaye wameishi na waakina kinana na ahmed tangia wakiwa wadogo na kuipeleke kwa kinana kordo area kwenye nyumba ya kinana iliokuwa inalindwa na jeshi.CCM ikitaka aibu iendele kumkumbatia waone tutaanika mambo yake yote na tuna muitaji msigwa tumpe historia nzima na tutamkutanisha wale wote waliowahii kufanya hizo kazi kwa kinana.
Tatizo sio KINANA, tatizo ni CCM
 
Kinana ni jangili kama wanataka ushaidi waje arusha.wapo watu walio bebaga pembe hizo miaka ya 80 na kuipeleke burundi enzi hizo kabla ya kuamishia njia ya dar.kuanzia miaka ya 89 na95 alikuwa anafanya biashara ya mandrax kutoka pakstan alikuwa anapitishia KIA alikuwa anapitishiwa na albat wa dahaco na kumkabidhi msamba mmoja mwenye jina la tahiri wa mbuguni ambaye wameishi na waakina kinana na ahmed tangia wakiwa wadogo na kuipeleke kwa kinana kordo area kwenye nyumba ya kinana iliokuwa inalindwa na jeshi.CCM ikitaka aibu iendele kumkumbatia waone tutaanika mambo yake yote na tuna muitaji msigwa tumpe historia nzima na tutamkutanisha wale wote waliowahii kufanya hizo kazi kwa kinana.
Duu aisee Jf ni habari nyingine
 
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, ametangaza upya vita dhidi ya majangili wa nyara za taifa na rasilimali nyingine nchini, huku akiwema wazi mpango wa kufanya doria 100,000 na kukunua ndege mbili katika mwaka ujao wa fedha kwa lengo la kuwakabili maadui hao wa maendeleo.

Waziri Kagasheki amesema licha ya changamoto kubwa ya kusimamia rasilimali za nchi hususan wanyamapori, wizara yake itaimarisha usimamizi na udhibiti kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola pamoja na wananchi.

Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake bungeni jana Jumanne mjini Dodoma, Waziri huyo alisema suala la doria na udhibiti wa ujangili limekuwa changamoto kubwa na kwamba serikali kupitia wizara yake haitashindwa kuwadhibiti.

"Wizara itaendelea kuimarisha usimamizi wa rasilimali za wanyamapori kwa kuendelea kufanya doria ndani na nje ya mapori ya akiba kwa kuendesha doria - siku 100,000. Miundombinu, vitendea kazi na huduma vitaboreshwa kwa watumishi katika vituo 27 kwenye mapori ya akiba na kanda nane za vikosi dhidi ya ujangili," alisema Waziri Kagasheki.

Alisema biashara ya uvunaji haramu wa mazao ya misitu na nyuki itadhibitiwa zaidi kwa kuongeza doria 20,700 katika maeneo ya nchi kavu na majini pamoja na kudhibiti viwango vya ubora wa mazao ya misitu na nyuki ili kuongeza thamani yake na kuongeza mapato ya nchi.

Kuhusu maboresho ya maeneo ya kufikia watalii alisema wizara yake kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) itajenga nyumba 29 katika hifadhi tisa za Arusha, Katavi, Kilimanjaro, Mikumi, Mkomazi, Ruaha, Rubondo, Serengeti na Udzungwa pamoja na kujenga barabara mpya zenye urefu wa kilomita 115 katika mwaka ujao wa fedha 2013/2014.

"Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro itajenga jengo moja la familia sita za wafanyakazi, jengo la mapokezi uwanja wa ndege wa Ndutu, jiko kwenye kambi ya kulala wageni ya Simba A pamoja na nyumba moja ya Askari eneo la Lositete. Mamlaka itaendelea na ujenzi wa jengo la kitega uchumi (kwa ubia) lenye gorofa 10 mjini Arusha,"alisema Waziri Kagasheki ambaye hotuba yake ya bajeti kwa Wizara ya Maliasili na Utalii imechapishwa katika gazeti hili.

Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Mali Asili na Mazingira, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bw. James Lembeli, alisema kamati yake imesikitishwa na tatizo kubwa la ujangili wa tembo unaozidi kukua badala ya kupungua.

"Kwa sasa ujangili wa tembo umekuwa ni janga la kitaifa, ni ukweli usiofichika kwamba leo hii si tu tembo wanauawa bali wanateketezwa, kwa mujibu wa tafiti zilizokwishafanywa na taasisi za utafiti wa wanyamapori nchini takwimu zinazoshabihiana na za taarifa za utafiti wa kimataifa zinaonesha kwamba tembo wasiopungua 30 wanauawa kwa siku, 850 kwa mwezi na tembo 10,000 kila mwaka,"alisema Bw. Lembeli.

Wakati huo huo, Siasa zenye dalili za kuchafuana kwa malengo ya kisiasa zimeibuka bungeni na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahaman Kinana, akijikuta katikati ya siasa hizo, kabla ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi, kusimama na kulitaka Bunge kuepuka kuhusishwa na uongo.

Ni kama vile ulikuwa mpambano kati ya wabunge wa CHADEMA wakiongozwa na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa na wabunge wa CCM, wakiongozwa na Waziri Dk. Nchimbi ambako mivutano ya hoja zilizomhusisha Kinana bungeni huku Spika wa Bunge, Anne Makinda aliamua kuweka kuachia kwa muda kila upande ukamilishe mashambulizi dhidi ya upande mwingine na kisha upande ulioshambuliwa ujibu mapigo.

Katika kuacha mashambulizi na kujibu mapigo kuchukue nafasi yake, Spika alisikika akisema; "Nyingi (wapinzani) mlivyokuwa mkizungumza (kuporomosha mashambulizi) wenzenu walinyamaza wakiwasilikiza."

Katika hoja zake, Msigwa alidai Kinana anahusika katika biashara haramu ya pembe za ndovu akigusia tukio la mwaka 2009 ambako shehena ya pembe za ndovu zenye uzito wa tani 4 kutoka Tanzania na Kenya ziliripotiwa kukamatwa na vyombo vya usalama vya Vietnam akiitaja kampuni ya wakala wa meli ya Sharaf Shipping Co. Ltd inayomilikiwa na familia ya Kinana.

Waziri Nchimbi alianza kwa kueleza namna Wizara ya Maliasili na Utalii inavyofanya jitihada kutimiza majukumu yake na kwa sababu Waziri kivuli, Mchungaji Peter Msigwa alidai hakuna cha maana kilichofanyika, Nchimbi alisema anaamini mtu wa namna hiyo (aina ya Msigwa) upeo wake wa uelewa una utata mkubwa na baadae kufafanua tuhuma dhidi ya Kinana.

Nchimbi alisema wahusika walikwisha kufikishwa mahakamani na kwamba Msigwa na viongozi wenzake wa upinzani wanafahamu tofauti kati ya kampuni ya Uwakala wa Meli (Shipping Argent) na Kampuni ya Kupeleka na Kuingiza Mizigo (Clearing and Forwading Co. Ltd).

Pamoja na Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) Tundu Lissu kutaka kumzuia Nchimbi kujibu tuhuma, Spika Anne Makinda alipuuza na kumtaka Nchimbi kuendelea kuzungumza akisema; "wakati Msigwa anatoa tuhuma dhidi ya Kinana na makada wengine wa CCM, aliachwa ahitimishe tuhuma zake bila kuingiliwa."

Nchimbi aliwataja waliokamatwa na kufunguliwa kesi ni pamoja na Ladislaus Tesha, Gabriel Chambo, Shaaban Yasin, Erick Leo (anayedaiwa kuwa Mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato eneo la Bandari ya Dar es Salaam), Issa Ahmed, Norbert Kiwale na Aboubakar Omar Hassan.

Nchimbi alilieleza Bunge ya kuwa kesi dhidi ya watuhumiwa hao ilifunguliwa katika Mahakama ya Kisutu lakini ilisimamishwa kwa muda ili kupata ushahidi kutoka nchi ya Vietnam na kwamba Vietnam ilikataa kutoa ushahidi kwa maelezo kuwa haina mkataba na Tanzania katika ushirikiano dhidi ya makosa ya jinai lakini kumekuwa na jitihada za kupata kibali cha mpito cha mkataba huo kutoka China ili kupata ushahidi na kesi hiyo iweze kuendelea katika Mahakama ya Kisutu

Hawa wachafu ndio wanajidai wazalendo.Waachie nchi yetu. Kuna wakati Mwenyezi Mungu atashusha radi kuondoa wapinga Tanzania.
Tuache hii michezo michafu kama tuna hati miliki ya Taifa hili. Hiyo ni dhambi na kosa la jinai
 
Waraka wa Mzee Kinana umeleta Kizazaa sehemu fulani,


Yaan kwa Lugha za medani ‘Ghala kuu limetekwa dakika chache kabla ya kuanza vita ‘

Kama Matusi Mzee Kinana katukanwa sana mpaka Bungeni tena akiwa Katibu Mkuu wa Chama tawala iweje leo ashindwe kuvumilia matusi ya Musiba?

Waraka wa Mzee Kinana umemtaja Musiba tu lakin mpaka sasa washajibu watu kama 10 hivi kumtukana Comrade kwa Waraka ule eti unapasua chama!

Iweje upasue Chama wakati Musiba sio maana Ccm ?

Jibu ni moja tu, tufani limezuiwa kwa sasa

Waraka mmoja tu page mbili watu wameingia studio kufoji audio

Ikipigwa press conference sijui itakuaje?
 
Huu uzi mbona umefufuliwa leo na ni wa zamani sana.
Kuna hii comment naona ni nzito sana!
Kinana ni jangili kama wanataka ushaidi waje arusha.wapo watu walio bebaga pembe hizo miaka ya 80 na kuipeleke burundi enzi hizo kabla ya kuamishia njia ya dar.kuanzia miaka ya 89 na95 alikuwa anafanya biashara ya mandrax kutoka pakstan alikuwa anapitishia KIA alikuwa anapitishiwa na albat wa dahaco na kumkabidhi msamba mmoja mwenye jina la tahiri wa mbuguni ambaye wameishi na waakina kinana na ahmed tangia wakiwa wadogo na kuipeleke kwa kinana kordo area kwenye nyumba ya kinana iliokuwa inalindwa na jeshi.CCM ikitaka aibu iendele kumkumbatia waone tutaanika mambo yake yote na tuna muitaji msigwa tumpe historia nzima na tutamkutanisha wale wote waliowahii kufanya hizo kazi kwa kinana.
 
Back
Top Bottom