VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Akiwa ameshindwa kuiwakilisha hoja ya kujivua gamba katika vikao vya Kamati Kuu na ile Kamati ya Nidhamu ya CCM,Mwenyekiti wa CCM Taifa,Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameamua kuisogeza,pasipo maandishi, hoja hiyo kwa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa inayokutana hapa Dodoma.Rais Kikwete ambaye ndiye Mwenyekiti wa vikao vyote vya kitaifa vya CCM,amejikuta akigeukwa na wasaidizi na washauri wake wakuu na wa karibu kuhusu hoja ya kujivua gamba.Katibu Mkuu wa CCM Taifa,Wilson Mukama alinukuliwa jana akimnong'oneza Kikwete kuwa kuwatosa magamba ni gharama kubwa kuliko kuwa nao.Alimshauri akae mbali na hoja hiyo kwa kuiacha mikononi mwa wajumbe wa NEC.Wachambuzi wa mambo hapa Dodoma wanatabiri kuwa hoja ya gamba italetwa kama AoB(Mengineyo) na si kama hoja rasmi.Makongoro Nyerere,Mwenyekiti wa CCM Mara,maarufu kama Mzee wa site ameapa kuweka hoja hiyo mezani.Kikao cha NEC kilichoanza jana,kimegawanyika katika makundi mawili:wachukia gamba na wapenda gamba huku wapenda gamba wakiwa na nguvu zaidi.Nilipomdodosa Bashe juu ya gamba,alinijibu kwa kujiamini kuwa Lowassa na Chenge hawagusiki.Mimi ni Vuta-Nkuvute kwa niaba ya JamiiForums-Dodoma.