Mechi kati ya Tanzania 11 vs Real Madrid, mapungufu

Mechi kati ya Tanzania 11 vs Real Madrid, mapungufu

Governor of Bettors-GB

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2013
Posts
10,879
Reaction score
10,100
Wakuu hii mechi nilikuwa naisuburi kwa ham sana.Kwa sie wadau wa michezo.

Lakini Umuhim wa mechi na hali halisi naona haviendani kabisaa.

Maana majuzi tu tumeowaona Real Madrid wakicheza na Machenster.

Nionavyo mie na mapunguf ni kama ifuatavyo:-

-Jina la timu ya Tanzania

Hivi inakuwaje watu waite timu ya Tanzania kwamba TANZANIA ELEVEN,ndio nini hasa ki mantic,Yaani Real Madrid Veteran wakicheza na Tanzania Eleven,TFF mjipange,matukio mengine hayarudii kwa miongo kadhaaa.Hata huku Mchangani watu wanajipanga kwenye majina.


-Ushiriki wa Wazanzibar kwenye Timu
Wameitwa watu wawili tu,mambo mengine haya ya kero za muungano tunayataka wenyewe kwa makusudi.
Hivi hili nalo linahitaji serikali iunde kamati Dodoma ili watu wale Posho?Huu upuuzi kabisa

-Mashabiki wachache uwanjani

Juzi tumeshuhudia kati ya Real Madrid na Manchester,uwanja ulikuwa hauna pa kukanyaga kwa jinsi ulivyojaa.Na vyombo vya habari duniani vinafuatilia tukio la Ziara ya Real Madrid yote.
Sasa vyombo vyote vya wadau wa michezo duniani leo vinaangaza Tanzania ambapo ni fursa nzuri sana kwetu.Kiuchumi kwa ujumla.
Hivi tabia ya TFF kuona kwamba kila mechi watengeneze mamilioni ni tatizo,tuliona mechi iliyopita na The Mambas(Msumbuji),ambapo mashabiki kama wachezaji wa ziada mlikuwa kama hakuna,na The Mambas kwao walichofanya walijaza uwanja na kuitumia nafasi vizuri kwao mbele ya umati wa mashabiki.

Hii mechi TFF imepanga kiingilio cha 5,000 huku kiingilio cha juu kikiwa Sh 25,000 kwa VIP B. VIP C ni Sh 20,000 wakati viti vya bluu ni Sh15,000 na rangi ya chungwa Sh10,000.
Hili ni tatizo,yaani hata nchi nyingine Duniani ambapo bahati hii ziliitamani ila hazikupata nafasi,naamini hii chance wangepata Wakenya wangefanya vizuri sana.
Duniani wanatuona kwamba hivi hii nchi gani yaani timu kubwa na umuhim wa timu ile na matajiri wakubwa,maana Club Tajiri na wachezaji matajiri,lakini wanatushangaa kuona nchi yenyewe watu hawapendi mpira namna hii.Upenzi wa mpira kwa wananchi unaangliwa wingi wa watu uwanjani.Halafu mbele ya Raisi.Simba na yanga mziki unajaa,hata Simba na Mbeya City wanaujaza.
Ilitakiwa Kiingilio kiwe 2,000 tu na Orange isizidi 5,000.

-TBC
Asanteni sana kwa kutuletea Mpira Live,ila mgeomba msaada kwa AZAM Tv,maana ubora weni bado haujawa vizuri kabisa kwenye michezo ya mpira.


-AZAM TV two nao wapo live nakama kawaida yao ni mfumo wa Supersport ubora wa hali ya juu.

Pongezi:
Pongezi za dhati kwa Rais Kikwete kwa kutujali sie wadau wa wa mchezo wa mpira na wenye kujua umuhim wa ujio huu.

 
Tbc wanatoa poor broadcast. Kwenye screen hakuna scoreboard. Mtu ukiwasha tv haujui nani kafungwa nani kashinda,haujui match ipo dakika ya ngapi,madrid wamejifunga mtangazaji wa tbc anasema Kali ongara ndio kashinda. Kha!
 
sport bongo wapi na wapi?
si tunawaza jinsi ya kupiga pesa aka madili au wizi
 
Yaani kazi kweli Aisee.
Yaani umihim wa ujio wa hawa jamaa watu ilitakiwa kujaza uwanja.
Watu wanataka Pesa tu TFF za uwanja.
Halafu leo hii unataka Mbwana Samata akacheze ulaya wakati wao wenyewe wanajua kwamba hawa jamaa tuliendakwao hata mpira hawaupendi maana uwanja mweupe,itakuwa huyu mmoja kabahatisha.

Angalizo:
Inaweza kuwani ushamba wangu Ila Nimeangalia Mic ya Mtangazaji wa AZAM Tv ilikuwa ni ya kisasa kabisa,na hakuna chombo chochote cha habari nchi hii nimewahi kuona.Yaani in Digital display kwenye zile pande tatu za mbavuni,yaani Pale kwenye Mic huwa kuna jina la kituo,sasa ile yenyewe sio ya kubandika ni ya Screen yaani inbadilika picha kama vile lile Screen lao la Matangazo yao.
Acha ile aliyoshida Edo Kumwembe ni ile alioshika Mwenye Black Suit(Maestro)
 
Yaani kazi kweli Aisee.
Yaani umihim wa ujio wa hawa jamaa watu ilitakiwa kujaza uwanja.
Watu wanataka Pesa tu TFF za uwanja.
Halafu leo hii unataka Mbwana Samata akacheze ulaya wakati wao wenyewe wanajua kwamba hawa jamaa tuliendakwao hata mpira hawaupendi maana uwanja mweupe,itakuwa huyu mmoja kabahatisha.

Angalizo:
Inaweza kuwani ushamba wangu Ila Nimeangalia Mic ya Mtangazaji wa AZAM Tv ilikuwa ni ya kisasa kabisa,na hakuna chombo chochote cha habari nchi hii nimewahi kuona.Yaani in Digital display kwenye zile pande tatu za mbavuni,yaani Pale kwenye Mic huwa kuna jina la kituo,sasa ile yenyewe sio ya kubandika ni ya Screen yaani inbadilika picha kama vile lile Screen lao la Matangazo yao.
Acha ile aliyoshida Edo Kumwembe ni ile alioshika Mwenye Black Suit(Maestro)
Labda wangekuja kina Cristiano Ronaldo, Balle, James Rodriguez, Iker Casillas, wakongwe itakuwa hawajakubalika
 
Kulikuwa na haja gani ya kumwonyesha Zidane, Ronaldo kwenye matangazo ya hiyo mechi ili hali wakijua hawatakuja? Utapeli wa wa TZ
 
Kulikuwa na haja gani ya kumwonyesha Zidane, Ronaldo kwenye matangazo ya hiyo mechi ili hali wakijua hawatakuja? Utapeli wa wa TZ

Nchi hii ina magumashi sana..wameleta watu hata sijawahi kuwasikia eri karembegu ! Sijui hata alichezeaga kajumulo huyu wao wanasema madrid
 
Kombe wametoa kienyeji kama vile Kombe la Kuku! Wangeweka hata ki jukwaa cha kiushkaji tu!


Sent from my iPad Air using JamiiForums
 
Luis Figo alivaa jezi na. 10 first half, second hlf akatupia na. 25 na wala refa haja mind. Kali Ongala kapumzika na baadae akaingia tena kucheza, safi sana ile mechi, tumefungwa la 3 JK kashangilia!!
 
Mao Mkami alinifurahisha, aliingia kipindi cha pili na hakumaliza dakika ... akatoka, hata hivyo tuli enjoy sana!!
 
Ilikuwa Bonge la wikiend maana nilikaa na warembo Wa kiarabu VIP B.
 
Ilikuwa Bonge la wikiend maana nilikaa na warembo Wa kiarabu VIP B.
Baada ya mechi mkaenda wap? Mimi nilielekea Ikulu kwenye mnuso, yaani nilikula, nilikunywa hadi saa hizi sijaamka, kichwa inazunguruka..
 
Baada ya mechi mkaenda wap? Mimi nilielekea Ikulu kwenye mnuso, yaani nilikula, nilikunywa hadi saa hizi sijaamka, kichwa inazunguruka..

Mnanishangaza kuhadithia stori nusu nusu, mbona husemi baada kunywa ulifanywa nini na walikuwa wangapi?
 
-Uzanzibari: je wajuaje kama wakongwe wa huko waliitwa au la. Je kama walioitikia wito ni hao wawili tu utamlaumu nani? Acha usisi na uwao. -kuhusu watu wachache: wewe ulienda?? Pia ukiweka bei ya chini zaidi, hadi wapumbavu wataingia kwenda kung'oa viti. Afadhari aingie mstaarabu mmoja kwa 5000 kuliko wapumbavu 5 kwa elfu moja. Hamna haja ya kuingiza watu wengi kwa bei ya chini kisha wakatugharimu uwanja wetu wa kisasa. Ila ni mawazo yako na ninayaheshimu. Pia suala la jina la Tanzania Eleven hapo walichemka, wenzetu wanaweza fikiri wale ndo the best eleven we can offer. Wangeiita labda Tz legends.
 
Nchi hii ina magumashi sana..wameleta watu hata sijawahi kuwasikia eri karembegu ! Sijui hata alichezeaga kajumulo huyu wao wanasema madrid
Hiyo ni moja ya 7bu zilizopelekea uwanja kupwaya, watu walitegemea majina kama ya Zizzu, Ronaldo de Lima, Roberto Carlos.... lakini sio
 
Back
Top Bottom