Mchochezi
JF-Expert Member
- Feb 29, 2012
- 10,409
- 6,555
1. Man Utd 4-3 Man City (mwaka 2009.)
Wakati Craig Bellamy akiisawazishia Man City dakika ya 90 na kufanya ubao usomeke 3-3 wengi waliamini mechi hiyo ingeisha kwa sare, zikaongezwa dakika 4, City wakarudi nyuma kupaki basi.
Ghafla Michael Owen akaibuka shujaa baada ya kufunga goli la ushindi dk ya 96 nje ya zile 4 za nyongeza. Kocha wa Man City alilalamika sana baada ya Refa kushindwa kumaliza mpira kwa muda sahihi.
2. Liverpool 3-3 Ac Milan (Fainali ya Uefa 2005)
Fainali hii iliyofanyika Instanbul, Liverpool walikuwa nyuma kwa magoli 3-0 wakati wa mapumziko, kipindi cha pili kinaanza kwa kocha Benitez kumuingiza Dietmar Hamann ambaye alienda kumzuia Pirlo asicheze na kuwafanya Liverpool warudi mchezoni, dk 90 mechi inaisha 3-3 na Liverpool wanaenda kubeba ndoo kwa penati baada ya extra time.
3. Derpotivo La Coruna 4-0 Ac Milan ( Robo Fainali ya Uefa, April 7, 2004)
Mabingwa watetezi wa Ulaya, AC Milan wakiwa na advantage ya ushindi wa 4-1 walioupata nyumbani San Siro, walienda kuwafata Derpotivo wakiwa vifua mbele lakini wakakutana na dhahama nzito ya kipigo cha 4-0 toka kwa Derpotivo. Walter pandiani kaibuka staa wa mchezo kwa kutakata na kuwapoteza mastaa wa Milan kama Kaka, Pirlo, Inzaghi na Shevchenko.
Ac Milan wakatolewa kwa jumla ya Magoli 5-4.
Karibu mdau ututajie na wewe mechi zako 3 unazozikubali.
Wakati Craig Bellamy akiisawazishia Man City dakika ya 90 na kufanya ubao usomeke 3-3 wengi waliamini mechi hiyo ingeisha kwa sare, zikaongezwa dakika 4, City wakarudi nyuma kupaki basi.
Ghafla Michael Owen akaibuka shujaa baada ya kufunga goli la ushindi dk ya 96 nje ya zile 4 za nyongeza. Kocha wa Man City alilalamika sana baada ya Refa kushindwa kumaliza mpira kwa muda sahihi.
2. Liverpool 3-3 Ac Milan (Fainali ya Uefa 2005)
Fainali hii iliyofanyika Instanbul, Liverpool walikuwa nyuma kwa magoli 3-0 wakati wa mapumziko, kipindi cha pili kinaanza kwa kocha Benitez kumuingiza Dietmar Hamann ambaye alienda kumzuia Pirlo asicheze na kuwafanya Liverpool warudi mchezoni, dk 90 mechi inaisha 3-3 na Liverpool wanaenda kubeba ndoo kwa penati baada ya extra time.
3. Derpotivo La Coruna 4-0 Ac Milan ( Robo Fainali ya Uefa, April 7, 2004)
Mabingwa watetezi wa Ulaya, AC Milan wakiwa na advantage ya ushindi wa 4-1 walioupata nyumbani San Siro, walienda kuwafata Derpotivo wakiwa vifua mbele lakini wakakutana na dhahama nzito ya kipigo cha 4-0 toka kwa Derpotivo. Walter pandiani kaibuka staa wa mchezo kwa kutakata na kuwapoteza mastaa wa Milan kama Kaka, Pirlo, Inzaghi na Shevchenko.
Ac Milan wakatolewa kwa jumla ya Magoli 5-4.
Karibu mdau ututajie na wewe mechi zako 3 unazozikubali.