Mdahalo wa wazi kuhusu Muungano wa Tanzania kufanyika UDSM 26.04.2017

George Kahangwa

JF-Expert Member
Oct 18, 2007
547
148
Kwa watanzania wote,
Jumuiya ya Wanataaluma ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), imeandaa mdahalo wa wazi utakaowapa wananchi fursa ya kuutafakari Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwa kuangalia tulikotoka, tulipo na tunakoelekea.
Mdahalo utafanyika katika ukumbi wa Nkrumah wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kampasi ya Mlimani, mnamo tarehe 26.04.2016, siku ya jumatano, kuanzia saa 8.00 mchana hadi saa 12.00 jioni. Tutakuwa na wachokoza mada wakuu wanne (wawili wanataaluma na wawili wananchi).

Wananchi wote mnakaribishwa. Hakuna kiingilio.

Aidha, kwa wasioweza kuhudhuria kwa sababu mbalimbali, tunapenda kuwataarifu kuwa wanaweza kuufuatilia mdahalo huu mubashara kupitia ITV.

Karibuni sana.

George Kahangwa
Mwenyekiti wa UDASA
 
safi sana msisahau swali muhimu je ni kweli karika hati ya muungano karume hakusaini kama alivyowahi sema tundu lissu
 
Msituwekee wachokoza mada ambao ni makada wa ccm,au wanaotafuta uteuzi kutoka ikulu,mkiwaweka hao bora msirushe live,muende tu ikulu mdahalo mfanye huko
 
Na hisi utapigwa marufuku kwa kisingizio kile kile cha siku zote
Uchochezi
hao UDASA wajinga mchakakato umepelekwa kwa wananchi umejadiliwa wametoa maoni kupitia wawakilishi wao wabunge na baraza LA wawakilishi ambao ni bunge LA katiba wakatoa maamuzi hawa Udasa wanataka kujadili nini wako juu ya wananchi MA bunge la katiba? magufuli umekuwa ukiteua wasomi toka chuo kikuu change DSM hao watakaoshiriki huo mdahalo ambao ni walimu wa chuo kikuu ukiwateua Post yeyote siji tena kutetea chochote cha serikali ya CCM humu. wasomi wanatakiwa kuheshimu maamuzi ya wananchi na mihimili mingine ikiwemo bunge la katiba
 
Yehodaya;
Waliostarahabu hawatukani; kila siku kunachangamoto ya muungano na lazima tuyajadili
 
Inasemekana kero za Muungano 12 time sh a shughuli kuwa na kubaki 3 tu!!
 
Naomba Mhe. Mkuu wa Mkoa awepo achangie mada vijana wanavyotakiwa kuuenzi Muungano ktk Tanzania ya Viwanda

Naamini ombi langu litafanyiwa kazi
 
Inasemekana kero za Muungano 12 time sh a shughuli kuwa na kubaki 3 tu!!
Mkuu siulizi kinafki ila am serious naomba unisaidie je faida za muungano ni zipi kiasi kwamba ukiuongelea tu inakuwa kesi?? Nisaidie
 
Kwa watanzania wote,
Jumuiya ya Wanataaluma ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), imeandaa mdahalo wa wazi utakaowapa wananchi fursa ya kuutafakari Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwa kuangalia tulikotoka, tulipo na tunakoelekea.
Mdahalo utafanyika katika ukumbi wa Nkrumah wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kampasi ya Mlimani, mnamo tarehe 26.04.2016, siku ya jumatano, kuanzia saa 8.00 mchana hadi saa 12.00 jioni. Tutakuwa na wachokoza mada wakuu wanne (wawili wanataaluma na wawili wananchi).

Wananchi wote mnakaribishwa. Hakuna kiingilio.

Aidha, kwa wasioweza kuhudhuria kwa sababu mbalimbali, tunapenda kuwataarifu kuwa wanaweza kuufuatilia mdahalo huu mubashara kupitia ITV.

Karibuni sana.

George Kahangwa
Mwenyekiti wa UDASA
Sawa asanteni kwa taarifa.
 
Napendekeza watoa mada wawe:-
1 Tundu Lissu
2 Othman Masoud
3 Prof Sharrif
vs
4 Mwakyembe
5 Polepole
6 Prof Shivji
 
Kwa maoni yangu kwa hatua tuliyofikia hadi zanzibar wanakosa mchanga wa kujengea.Jinsi tulivyoungana kwa damu pia..
Uwepo wa Muungano ni wa lazima sio hiyari tena.
 
Msiwe na shaka maana Mimi mwenyewe nitatia timu Siku hiyo! Hivyo kama una swali unaweza ukanena sasa ili nikakuwakilishe.....
 
Mkuu siulizi kinafki ila am serious naomba unisaidie je faida za muungano ni zipi kiasi kwamba ukiuongelea tu inakuwa kesi?? Nisaidie
Kwanza hakuna sheria yoyote au maandiko yoyote ya Serikali wanasema kuongea kuhusu Muungano basi ni kesi hiyo Mimi sijawahi kusikia wala kuona hapa Tanzania.

Kuhusu faida za Muungano ni nyingi tu kwanza unaongeza market area interns of population

Pili unaongeza wigo wa usalama kwa nchi hasa mpaka ya bahari kuu

Tatu walikuwa na interest binafsi na kisiwa baada ya Muungano ni ngumu sana kwasababu kwa sasa lazima wapite Serikali ya Muungano kwa mahusiano ya kimataifa.

Visiwa vilivyo vingi huwa haviko vyenyewe tu kwa sababu za kiusalama Mara nyingi huwa viko chini ya mataifa Makubwa Pamoja na utawala wao wa ndani
 
Kwa watanzania wote,
Jumuiya ya Wanataaluma ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), imeandaa mdahalo wa wazi utakaowapa wananchi fursa ya kuutafakari Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwa kuangalia tulikotoka, tulipo na tunakoelekea.
Mdahalo utafanyika katika ukumbi wa Nkrumah wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kampasi ya Mlimani, mnamo tarehe 26.04.2016, siku ya jumatano, kuanzia saa 8.00 mchana hadi saa 12.00 jioni. Tutakuwa na wachokoza mada wakuu wanne (wawili wanataaluma na wawili wananchi).

Wananchi wote mnakaribishwa. Hakuna kiingilio.

Aidha, kwa wasioweza kuhudhuria kwa sababu mbalimbali, tunapenda kuwataarifu kuwa wanaweza kuufuatilia mdahalo huu mubashara kupitia ITV.

Karibuni sana.

George Kahangwa
Mwenyekiti wa UDASA
Msomi nyumbx, vipi mmeshapewa vya kuongea na mbowe na mamvi
 
Back
Top Bottom