Mwamuzi Msaidizi namba mbili katika mchezo wa Yanga SC na Simba SC, Hamdan Said amemfungiwa miezi mitatu kwa kosa la kusimamisha shambulizi la mchezaji Prince Dube dhidi ya Simba dakika ya 61, akidai alikuwa eneo la kuotea.
Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu imesema baada ya kufanya tathmini imebaini Dube hakuwa katika eneo la kuotea.
Aidha, Mwamuzi Msaidizi namba moja wa mchezo kati ya Yanga SC na Simba SC, Kassim Mpanga amefungiwa miezi sita kwa kukataa goli la Simba.Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu imesema baada ya tathmini imebaini hakukuwa na kosa kabla ya kufungwa kwa goli hilo.