Jumanne Mkota
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 3,011
- 1,794
Mbunge wa jimbo la mwanga na Waziri wa maji Prof Jumanne Abdala Maghembe amekutana na adha ya kukataliwa mapema na wananchi kabla hata ya uchaguzi katika ziara zake kampeni zisizo na Baraka za Chama chake.
Adha hiyo alikutana nayo 16/02/2015 katika kitongoji cha Changalavo Kijiji cha Ngujini Kata ya Kisangara wilaya ya mwanga.
Awali ratiba yake ilikuwa ina mkutano wa hadhara wa wanakijiji ambapo pia ndipo Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya anapoishi na ndipo kitongoji alichozikwa mwana harakati na msomi mbobezi wa mambo ya Katiba Hayati Dr. Sengondo Mvungi.
Kwenye Mkutano huo ambapo itifaki ilivunjwa kikao kilifunguliwa na Mwenyekiti wa kitongoji hicho ambaye anatokea CCM huku wakimuacha Mweneykiti wa kijiji ambaye anatokea Chama cha demokrasia na maendeleo.
Wananchi hao walivumilia hilo lakn Mbunge akaanza kutoa matusi na vitisho kuwa kijiji cha ngujini kisahau kitu kinachoitwa maendeleo kwani kosa walilofanya la kuichagua chadema litawagharimu.
Mwananchi mmoja alisimama na kumwambia Mbunge kuwa walishasahauliwa siku nyingi so atembee mbele(yaani aondoke kabisa eneo hilo) na kama haamini kuwa hawamtaki eneo hilo aongeze neno lolote lolote lile linawahusu aone cha mtema kuni.
Baada ya Hali kuwa tete alishuka jukwaani na kukusanya msafara wake na kuondoka huku eneo hilo likihanikizwa na sauti za tapelii, mwongo, mwizi! yaani ilikuwa ni zomea zomea ya hatari
Hata hivyo Mbunge huyo aliendelea na ziara katika Kata ya Kirya ambapo pia CCM ni Chama cha upinzani ambapo pia alikutana na zomea zomea kiasi kwamba ameamua kuahirisha ziara hiyo.
Hapa jimboni mwanga siasa zake zimebadilika kiasi ambacho kinashangaza wengi. Wengi wa wananchi wanasubiri october 2015 na kama ccm itamsimamisha maghembe uwezekano wa Jimbo hilo kubaki CCM ni mdogo mno kuliko hata punje ya Ulezi ingawa vita itakuwa kali kati ya Joseph Tadayo kama CCM itamsimamisha na Henry Kileo, Au Dr. Ngoma wa CHADEMA.
Nawasilisha
Adha hiyo alikutana nayo 16/02/2015 katika kitongoji cha Changalavo Kijiji cha Ngujini Kata ya Kisangara wilaya ya mwanga.
Awali ratiba yake ilikuwa ina mkutano wa hadhara wa wanakijiji ambapo pia ndipo Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya anapoishi na ndipo kitongoji alichozikwa mwana harakati na msomi mbobezi wa mambo ya Katiba Hayati Dr. Sengondo Mvungi.
Kwenye Mkutano huo ambapo itifaki ilivunjwa kikao kilifunguliwa na Mwenyekiti wa kitongoji hicho ambaye anatokea CCM huku wakimuacha Mweneykiti wa kijiji ambaye anatokea Chama cha demokrasia na maendeleo.
Wananchi hao walivumilia hilo lakn Mbunge akaanza kutoa matusi na vitisho kuwa kijiji cha ngujini kisahau kitu kinachoitwa maendeleo kwani kosa walilofanya la kuichagua chadema litawagharimu.
Mwananchi mmoja alisimama na kumwambia Mbunge kuwa walishasahauliwa siku nyingi so atembee mbele(yaani aondoke kabisa eneo hilo) na kama haamini kuwa hawamtaki eneo hilo aongeze neno lolote lolote lile linawahusu aone cha mtema kuni.
Baada ya Hali kuwa tete alishuka jukwaani na kukusanya msafara wake na kuondoka huku eneo hilo likihanikizwa na sauti za tapelii, mwongo, mwizi! yaani ilikuwa ni zomea zomea ya hatari
Hata hivyo Mbunge huyo aliendelea na ziara katika Kata ya Kirya ambapo pia CCM ni Chama cha upinzani ambapo pia alikutana na zomea zomea kiasi kwamba ameamua kuahirisha ziara hiyo.
Hapa jimboni mwanga siasa zake zimebadilika kiasi ambacho kinashangaza wengi. Wengi wa wananchi wanasubiri october 2015 na kama ccm itamsimamisha maghembe uwezekano wa Jimbo hilo kubaki CCM ni mdogo mno kuliko hata punje ya Ulezi ingawa vita itakuwa kali kati ya Joseph Tadayo kama CCM itamsimamisha na Henry Kileo, Au Dr. Ngoma wa CHADEMA.
Nawasilisha