NonsenseKila siku mnaimba hapa demokrasia, demokrasia, mara sijui Tanzania hakuna demokrasia kama Ulaya, haya Waziri Mkuu wa Uingereza anajiuzulu kwa sababu ameshindwa kutimiza kile ambacho alikiahidi Chama chake/ kambi yake, sasa Mbowe unajiuzulu lini?
Kwa maana umeiongoza chadema chaguzi tatu na umeshindwa zote lkn bado wewe ni Mwenyekiti wa Chama na kama hilo halitoshi wewe bado ni KUB vipindi viwili mfululizo ingawaje hakuna uchaguzi uliyowahi kushinda!
Sasa mbona hapa hamtaki kuiiga demokrasia ya Wazungu? Au demokrasia ya Wazungu nzuri pale mnaponufaika?
Tayari tunamsikia fisadi Lowasa anataka kuwania tena uraisi mwaka 2020 huku akiimba demokrasia ingawaje alishindwa uchaguzi na isitoshe hakuna kikao chochote kilichompitisha kugombea uraisi 2020, je hiyo ni demokrasia?
Vile vile Zito Kabwe ambaye umekua ukipayuka sana siku za hivi karibuni kuhusu demokrasia na umeenda mbali zaidi na kumtuhumu Magufuli wetu kwamba hafwati demokrasia kama unavyoielewea wewe yaani demokrasia ya kizungu, mbona wewe hujajiuzulu kama Kameruni (Waziri Mkuu wa Uingereza) au Wazungu wengine wafanyavyo pindi vyama wanavyoviongoza vinaposhindwa Uchaguzi?
Zito Kabwe amekiongoza Chama chake cha ACT kwenye Uchaguzi ameshindwa vibaya sana siajabu haijawahi kutokea ktk Historia ya Dunia hii Kiongozi anayejinasibu kama Zito kwamba yeye ndiyo yeye anashindwa hata kupata Mbunge mmoja zaidi ya yeye mwenyewe hivyo kidemokrasia ina maana Zito Kabwe ni failure na hapaswi hata kuwa kiongozi, kwa maana ameshindwa kutushawawishi Watanzania tupigie kura Wabunge wake, vipi hapo demokrasia? Au ikifika hapo inakuwa wale ni Wazungu na sisi ni Waafrika?
Lisu, Baregu &Co. mko wapi kuhusu hili?
Hiyo msg ilitakiwa kupelekwa kwa CCM, wameahidi maisha mazuri kwa Watanzania tangu napata akili mpk leo hali ni ile ile, Ulimwengu anasema tunarudi nyuma miaka 50........nadhani kwa kushindwa kuwapa Watanzania maisha bora kwa wakati wote huo CCM ndio walipaswa wakae pembeni ili kuona wengine watalifanyia nini Taifa.......hata Zanzibar tu ingetosha kuonesha tofauti ya fikra na uongozi wa Nchi.
Dah! Kweli kuna watu wana macho lakini hawaoni. Nani wakujifunza hapo.nani asiyekubali kushindwa? Umesikia jeshi la polisi au tume wakitumia nguvu yoyote?Kila siku mnaimba hapa demokrasia, demokrasia, mara sijui Tanzania hakuna demokrasia kama Ulaya, haya Waziri Mkuu wa Uingereza anajiuzulu kwa sababu ameshindwa kutimiza kile ambacho alikiahidi Chama chake/ kambi yake, sasa Mbowe unajiuzulu lini?
Kwa maana umeiongoza chadema chaguzi tatu mfululizo na umeshindwa zote lkn bado wewe ni Mwenyekiti wa Chama na kama hilo halitoshi wewe bado ni KUB vipindi viwili mfululizo ingawaje hakuna uchaguzi uliyowahi kushinda!
Sasa mbona hapa hamtaki kuiiga demokrasia ya Wazungu? Au demokrasia ya Wazungu nzuri pale mnaponufaika?
Tayari tunamsikia fisadi Lowasa anataka kuwania tena uraisi mwaka 2020 huku akiimba demokrasia ingawaje alishindwa uchaguzi na isitoshe hakuna kikao chochote kilichompitisha kugombea uraisi 2020, je hiyo ni demokrasia?
Vile vile Zito Kabwe ambaye umekua ukipayuka sana siku za hivi karibuni kuhusu demokrasia na umeenda mbali zaidi na kumtuhumu Magufuli wetu kwamba hafwati demokrasia kama unavyoielewea wewe yaani demokrasia ya kizungu, mbona wewe (Zito) haukujiuzulu kama Kameruni (Waziri Mkuu wa Uingereza) au Wazungu wengine wafanyavyo pindi vyama wanavyoviongoza vinaposhindwa Uchaguzi?
Zito Kabwe amekiongoza Chama chake cha ACT kwenye Uchaguzi ameshindwa vibaya sana siajabu haijawahi kutokea ktk Historia ya Dunia hii Kiongozi anayejinasibu kama Zito kwamba yeye ndiyo yeye anashindwa hata kupata Mbunge mmoja zaidi ya yeye mwenyewe hivyo kidemokrasia ina maana Zito Kabwe ni failure na hapaswi hata kuwa kiongozi, kwa maana ameshindwa kutushawawishi Watanzania tupigie kura Wabunge wake, vipi hapo demokrasia? Au ikifikia hapo inakuwa wale ni Wazungu na sisi ni Waafrika?
Lisu, Baregu &Co. mko wapi kuhusu hili?
Hivi ccm lini walifanya uchaguzi wa mwenyekiti akashindanishwa na mwanachama mwingine wa ccm?
Basi utakuwa mgeni wa nchi hii na utaratibu na Katiba ya CCM hauijui, na isitoshe CCM siku zote wanasema wanafwata demokrasia ya Kitanzania, yaani siyo kila kinachofanywa na Wazungu lazima tuige lkn Upinzani (ukawa) wanailaumu nchi yetu kwa kutokufwata demokrasia ya kizungu wakati wao wenyewe linapokuja kwenye swala la Uongozi wanaikanyaga hiyo hiyo demokrasia ya kizungu!
Waziri mkuu alitudanganya kuwa hawarushi matangazo ya bunge live kwa kuwa hata ulaya hakuna kwa hiyo wameiga ulaya wakati ni uongo, sasa kamwambie majaliwa kuwa ulaya wanarusha matangazo live na wanachanel maalumu ya bunge tu kwa hiyo na tz warushe matangazo live