Kwa kifupi.
MH. Mbowe amesema umoja huo unakusudiwa kuongeza changamoto na nguvu mpya ya kisiasa nchini, lakini kuna haja ya kuangalia vyama unavyoungana navyo
"Umoja ni jambo jema utapunguza utani kwenye mambo serious ya kuendesha siasa ndani ya vyama, nasema utapunguza utani kwa sababu kuna vyama vina miaka 20 na zaidi lkn havina hata mkiti wa mtaa, sasa utaunganaje na chama kama hicho, ila kuna vingine vina muda mfupi lkn unaweza kuona vimefanya kitu". alisema Mbowe.
"Ila kwanza sijui kwa nini Zitto alizungumzia muungano wa vyama au umoja wa kidemokrasia msibani. Tulichokuwa tunafanya pale kwa kuwa mbunge alichaguliwa na wananchi wote ni kushirikiana kumhifadhi na baadaye kutafuta mgombea mmoja atakayekuwa na nguvu, lakini hilo suala sio la mimi kusema tu ni la vikao vya chama".