Mbona Hakumchinja ?

Mbona Hakumchinja ?

Idd Ninga

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
5,539
Reaction score
4,854
MBONA HAKUMCHINJA ?



1)salamu zifike kwake,natuma mkamwambie.
Lile kweli lile lake,ama yule yeye sie.
mbonaye hakumchinja ?



2)alimwacha ende zake,mbalie akibakie.
Wala hakupigwa teke,na yeye ajililie.
Mbonaye hakumchinja ?



3)kale kasindano kake,kuwachomea wenzie.
Wasinge kuwa wanzake,kumbe ingekuwa sie.
Mbonaye hakumchinja ?



4)walivyosema wenzake,naona kweli si ndie.
Kumbe mlipizo teke,wala sijatusi mie.
Mbonaye hakumchinja ?




5)yameshakufa makeke,sasa kama yeye ndie.
Mpole tena mpweke,tatizo njia ni ndie.
Mbonaye hakumchinja ?



6)kapewa tango ibike,kameza kama yesie.
Nusura atawanyike,ila kama wale sie.
Mbonaye hakumchinja ?




Shairi:MBONA HAKUMCHINJA ?
Mtunzi:Idd Ninga wa Tengeru Arusha .
+255624010160
iddyallyninga@gmail.con
 
Back
Top Bottom