Mbio za Mwenge Arusha

Mbio za Mwenge Arusha

Arnold Ringo

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2014
Posts
2,318
Reaction score
394
Wanafunzi wa Shule mbalimbali kwenye Manispaa ya Arusha mjini wametolewa kwenye vipindi vyao vya masomo kuja kushanga mwenge jee ndio kuwafundisha au kuwateketeza kielimu?

Na imefuatiwa nakukosa watu kwenye mbio za mwenge jijini Arusha
 
tuwekee picha ya hao wanafunzi na ikiwezekena tutajie baadhi ya shule alafu sisi wazazi tutaruka na hao waalimu zao
 
Mwenge unamaana kubwa Sana

you must be living in an acient experience....karne hii bado unaabudu upuuzi usiyofanywa na nchi nyingine yoyote ile duniani!!
 
Wanafunzi wa Shule mbalimbali kwenye Manispa ya Arusha mjini wametolewa kwenye vipindi vyao vya masomo kuja kushanga mwenge jee ndio kuwafundisha au kuwateketeza kielimu? Na imefuatiwa nakukosa watu kwenye mbio za mwenge jijini Arusha

Suala la wanafunzi kwenda kwenye mwenge haliaanza leo, toka miaka ya themanini/tisini lilikuwepo na wanafunzi walifaulu, na waliofeli walifeli. Kwenda kwenye mwenge siku moja hakuwezi kukufanya ufeli au uteketee kielimu. Kama ni kilaza ni kilaza tu au kama shule husika haitoi elimu bora basi mwenge hauwezi kuwa kisingizio.
 
Tena mwenge zamani wanafunzi tulikua tunachangia,bora hao wameenda bure.Hakuna uhusiano wa kuteketea kwa elimu na Mwenge.Km mwanao au mdogo wako nikilaza waache hao wengine waende wakapokee mwenge.
Akili za ki.ji.nga tu km mleta uzi watakao husisha mwenge na kushuka elimu.
 
Suala la wanafunzi kwenda kwenye mwenge haliaanza leo, toka miaka ya themanini/tisini lilikuwepo na wanafunzi walifaulu, na waliofeli walifeli. Kwenda kwenye mwenge siku moja hakuwezi kukufanya ufeli au uteketee kielimu. Kama ni kilaza ni kilaza tu au kama shule husika haitoi elimu bora basi mwenge hauwezi kuwa kisingizio.

Avatar yako mwisho sana mkuu!
 
Suala la wanafunzi kwenda kwenye mwenge haliaanza leo, toka miaka ya themanini/tisini lilikuwepo na wanafunzi walifaulu, na waliofeli walifeli. Kwenda kwenye mwenge siku moja hakuwezi kukufanya ufeli au uteketee kielimu. Kama ni kilaza ni kilaza tu au kama shule husika haitoi elimu bora basi mwenge hauwezi kuwa kisingizio.
Huu ni upuuzi mkubwa sana. Ratiba ya mbio za wenge ilifahamika tangu April, hivyo kutoa fursa kubwa sana kwa watendaji wote kujipanga na kuwahamasisha wananchi wajitokeze. Ujumbe wa mwenge unawalenga watu wazima, kama hawajitokezi, hao watoto wataambiwa nini ambacho watakifanyia kazi?
Enzi a kuwatumia waafz kam vikaragosi ktk propaganda za kisiasa ziliisha CcM kilipokomeshwa KSHIKA UTAMU 1992.
Tuwe wakwel, mwenge unapoteza muda na unahatrha lama wa waafz a alimu wao.
 
Tena mwenge zamani wanafunzi tulikua tunachangia,bora hao wameenda bure.Hakuna uhusiano wa kuteketea kwa elimu na Mwenge.Km mwanao au mdogo wako nikilaza waache hao wengine waende wakapokee mwenge.
Akili za ki.ji.nga tu km mleta uzi watakao husisha mwenge na kushuka elimu.

wewe unauwakika wanafunzi wa sasa hivi awachangishwi?
 
Tena mwenge zamani wanafunzi tulikua tunachangia,bora hao wameenda bure.Hakuna uhusiano wa kuteketea kwa elimu na Mwenge.Km mwanao au mdogo wako nikilaza waache hao wengine waende wakapokee mwenge.
Akili za ki.ji.nga tu km mleta uzi watakao husisha mwenge na kushuka elimu.

wewe ndiyo kilaza maana hujui thamani ya muda.
 
Suala la wanafunzi kwenda kwenye mwenge haliaanza leo, toka miaka ya themanini/tisini lilikuwepo na wanafunzi walifaulu, na waliofeli walifeli. Kwenda kwenye mwenge siku moja hakuwezi kukufanya ufeli au uteketee kielimu. Kama ni kilaza ni kilaza tu au kama shule husika haitoi elimu bora basi mwenge hauwezi kuwa kisingizio.

Naomba nichangie Kidogo suala hili maana Waswahili wanasema Haba na Haba hujaza kibaba. Sasa siku Wamekwenda kwenye Mwenge, kesho kaja Rais kwenye Mkoa wao watapelekwa, kaja Rais kutoka nje wajipange, Sherehe za zinazoitwa ETI za Mapinduzi na Muungano wanachezeshwa Halaiki mwezi mzima. Sasa hapo mnatafuta kweli mchawi?
 
Hîcho kibatari kimepoteza maana! Kinatakiwa kupelekwa Makumbusho!
 
Back
Top Bottom