Kiranja wa jamii
JF-Expert Member
- Jan 2, 2023
- 963
- 2,198
Kwa mtu anayefuatilia mambo ya nchi hii na anayejali mustakabali wa maendeleo ya nchi anajua kabisa uchawa kwa siku za hivi karibuni umeshusha uwajibikaji na hivyo unaendelea kuchangia kwa kiasi kikubwa kuliangamiza Taifa.
Zifuatazo ni mbinu zinazoweza kutumika kutokomeza tabia za uchawa japo kwa kiasi kikubwa mbinu hizi zinategemea wanaofanyiwa huo uchawa:-
1. Ikatazwe tabia ya kutaja taja majina ya viongozi au watu maarufu kwa kuyarudia rudia mara kwa mara. Kwa mfano; machawa wengi utawasikia
"namshukuru sana Mh. Rais, Dr., Mama Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania". Huku ni kupoteza muda na kuwachosha wasikilizaji/wasomaji
Kwani haitoshi kusema "...namshukuru sana Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania" bila kutaja jina lake? Nani asiyejua jina la Rais? Lengo la kutaja jina la mtu ni kumtambulisha kwa wasiomfahamu.
2. Viongozi wa Taasisi mbalimbali wawafundishe vijana kujiamini na kuthamini talanta zao. Unapomsifia mtu mwingine kupitiliza ndivyo unavyojishusha wewe. Unaonekana hauna unaloliweza zaidi ya kumtegemea unayemsifia
Unaweza kuongeza za kwako
Zifuatazo ni mbinu zinazoweza kutumika kutokomeza tabia za uchawa japo kwa kiasi kikubwa mbinu hizi zinategemea wanaofanyiwa huo uchawa:-
1. Ikatazwe tabia ya kutaja taja majina ya viongozi au watu maarufu kwa kuyarudia rudia mara kwa mara. Kwa mfano; machawa wengi utawasikia
"namshukuru sana Mh. Rais, Dr., Mama Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania". Huku ni kupoteza muda na kuwachosha wasikilizaji/wasomaji
Kwani haitoshi kusema "...namshukuru sana Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania" bila kutaja jina lake? Nani asiyejua jina la Rais? Lengo la kutaja jina la mtu ni kumtambulisha kwa wasiomfahamu.
2. Viongozi wa Taasisi mbalimbali wawafundishe vijana kujiamini na kuthamini talanta zao. Unapomsifia mtu mwingine kupitiliza ndivyo unavyojishusha wewe. Unaonekana hauna unaloliweza zaidi ya kumtegemea unayemsifia
Unaweza kuongeza za kwako
