Mbeya: Ngozi ya Simba yakamatwa

Mbeya: Ngozi ya Simba yakamatwa

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
26,715
Reaction score
59,251
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limekamata nyara za serikali ambazo ni ngozi moja ya simba na vipande 15 vya meno ya tembo vilivyokuwa vimebebwa kwenye pikipiki.
mpinga.jpg

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi Mohamed Mpinga amesema tukio hilo limetokea majira ya 10:00 alasiri mnamo Julai 27, mwaka huu katika pori la hifadhi ya taifa la Ruaha lililopo Rujewa wilayani Mbarali mkoani humo katika msako uliofaywa kwa kushirikiana na TANAPA.

DCP Mpinga amesema jeshi hilo kwa kushirikiana na TANAPA liliendesha msako na kufanikiwa kukamata nyara hizo ambazo zilizogundulika baada ya kukamata pikipiki sita ambazo wahusika wake walikimbia na kuzitelekeza, mbili zikiwa hazina ‘plate namba’ na nyingine zikiwa na usajili.

Katika matukio mengine, jeshi hilo limefanikiwa kukamata wahamiaji haramu wenye uraia wa Ethiopia saba katika nyakati tofauti katika mkoa huo baada ya kufanya msako katika maeneo mbalimbali.

Chanzo: EATV
 
Duh nikajua ngozi ya Diamond platnumz a.k.a first born wa Zarina
 
Back
Top Bottom