Mazuri ya CCM


Hayo matatu mekundu, yameshatoweka Tanzania.

1. Hakuna wakati ambapo CCM imekuwa ikitumia karata ya kuwagawa watu kwa makabila na kanda kama sasa. Sasa hivi CCM, kwa kuogopa M4C inadiriki kuwaambia watu wa mikoa na kanda fulani fulani hapa Tanzania kuvikataa vyama vya upinzani kwa hoja zisizo na mashiko. Hii inadhoofisha huo umoja wa kitaifa na chanzo ni CCM.

2. Amani na utulivu, baada ya kuua watu Arusha, Songea, kumtesa Dr. Ulimboka, mauaji ya Arumeru na Igunga (makada wa CDM) n.k n.k. naona amani na utulivu ni hadithi tu sasa.

3. Udini: Kwa sasa mjadala wowote hauwezi kukosa kuweka hoja za udini. Haijalishi mjadalauwe wa kisiasa, kiuchumi au kijaamii. Chanzo pia ni CCM kudhani kuwa inaweza kuwashikilia baadhi ya wanachama wake wasikitose kwa hoja ya dini!

Hayo mengine, kama yanafanywa kwa kodi ya wananchi na yamechelewa sana, yangepaswa kuwa tayari yameshafanyika, ni wajibu wa msingi wa serikali.
 
Wanajamvi nimeona leo tujadili mazuri ya CCM ambayo wameyafanya ili tuone upande mwingine wa shilingi maana hapa kila kitu kina pande mbili.
1. Umoja kitaifa na MGAWANYO wa matabaka
2. Amani na Utulivu kwa vitisho na ubabe
3. Kuondoa udini kinadharia na kuutekeleza kivitendo
5. kuukema ukabila na kukumbatia UTOTO wa nani [shemeji au ntoto au njukuu wa flani]
6. Daraja la Kigamboni coming soon provided OBAMA saYz YES
7. kuukubali upinzani na kuuthengenya mf mh ngatia
8. Ujenzi wa nyumba za wafanyakazi wote [wale wenye kufahamiana na wapiga mihuri] ambapo collateral ni deposits zao za NSSF na PFPF PPF
9. Ujenzi wa babrara nchi nzima lkn sio kanda ya ziwa kama BIHARAMULO,GEITA,KAGERA nk
10. Ujenzi wa Udom na vuo vikuu vingi vya kumwaga vyenye kutoa elimu duni
11.UTHENGE
12.UPHITHADI
13.UMABWEPANDE
14.MAJAJI NA WAENDESHA MASHTAKA VIHIYO yaani VICHWA H2O NA WATA-ALARM wenye elimu za kubumba kama Re is One aka Mwanassheria wa MIGODI NYONYAJI TANGANIA
15.MIGOGORO KILA SEKTA [solution ni ulimbokalization na ukolimbalisation]


 
Mengine haya hapa...


Akina mama wakiwa hospital, DSM Tanzania.




Dr. Ulimboka baada ya kupata kipigo. LIWALO NA LIWE.

bora useme wewe... Maana wengine tutaambiwa tunahatarisha Amani ya nchi. Unafanya kitu cha miaka 20 kwamiaka50 alafu unaomba pongezi?
 

Namba 3, 6, 8 na 9 ni uongo na pia ktk miaka 50 hawana lolote la kujivunia
 
Safii in short mazuri ni mengi sana sana tunaweza kuandika vitabu kadhaa ukifanya uchambuzi yakinifu na kuacha kusikiliza kelele za hao wanaolialia kama mbuzi

pole sana maana hujui ulipo na wala unalotakiwa kulifanya
 
Aiseeee baba yangu ni kweli kabisa ccm imeweza kununua rada, imeweza kumteka dr ulimboka 2endelee

leo napata mbege taratibuuu
 
Mengine haya hapa...


Akina mama wakiwa hospital, DSM Tanzania.




Dr. Ulimboka baada ya kupata kipigo. LIWALO NA LIWE.

Du inatisha hasa hiyo ya akina mama walioko wodini, kumbe mama zetu wanatuzalia ktk mazingira magumu na hatarishi yanayosababishwa na serikali ya ccm, sijui kodi zetu wanazielekeza wapi?
 
11. Misamaha ya kodi kwa wawekezaji kiasi cha TZS 2trilion kwa mwaka inayowawezesha kuendelea kuwepo na kutoa ajira kwa watz
12. Shule za kata nchi nzima maarufu kama vodafasta
13. Mikataba mizuri kwenye sekta ya madini inayoiwezesha serikali kukusanya mrabaha wa 3%
15. Mikataba mizuri ya mafuta na gesi inayotuwezesha kukusanya kodi tu lakini kukosa umiliki wa rasilimali hiyo muhimu
16. Mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura inayotuwezesha kupata umeme wa dharura japo kwa bei ya kifisadi.
17. Imewezesha kukua kwa sekta ya anga (Precision, Fly540, Zara, nk) japo shirika letu linadidimia/kufa.
18. Imewezesha uhusiano wetu na India kukua kwa kutumia vema hospitali zao kwa tiba za viongozi wetu.
19. Imewezesha viongozi wetu wengi kufanikiwa kumiliki nyumba maeneo nyeti kwa kuwauzia kwa bei poa.
20. Imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwaondoa wachimbaji wadogo maeneo yenye madini kwa lengo la kuwapatia wawekezaji wakubwa ambao watalipa mrahaba wa 3%

Kwa kweli mambo ni mengi ndugu Senkenke1 ukifanikiwa kuyataja yote ni nani asiye upande wetu atakayehimili kusimama na kusikilizwa?
 
Jingine zuri ililofanya ni kugawa chakula na kanga kipindi cha uchaguzi.
 
Kumpiga Nduli Idd Amin na Lugha ya Kiswahili nchi nzima. Wasio na macho waone smooth transfer of power
 
Serikali ya CCM kuruhusu upinzani kuwepo na kuendelea kufanya shughuli zao za kisiasa
 
CHADEMA ni mabingwa wa kulalama na kupinga kila jambo linaloanzishwa na serikali ya CCM.
1. Walipinga posho ya wabunge; kwa kificho wanachukua
2. Mbowe alitamka Gari la VX ni matumizi mabaya ya fedha; mwenyewe analitumia alilopewa na serikali
3. Walipewa fursa na JK kuchagua mtua wao aingie tume ya mabadiliko ya KATIBA, Prof. Baregu yumo ndani; leo wanasema mchakato wa KATIBA ni batili
4. Wanajipigia debe kuwa chama chao ni cha kidemokrasia wakati Dr. Slaa na Mbowe ni wagombea wa maisha wa URAIS na Uenyekiti wa Chama

CHADEMA manatakiwa mbadilike ili watanzania waanze kuwaamini kwenye chaguzi zijazo
 
yele yale kila siku, njooni na mapya tumewachoka.
 
Hivi Dr. Slaa amekuwa katibu muda gani? Mpaka iwe maisha
 
Hivi slaa amekuwa katibu muda gani? Mpaka iwe maisha

Umesahau Zito alipingana na Mbowe mara alipoonyesha nia ya kugombea Uwenyekiti wa Chama. Pia chama chako kinamuona Zito ni msaliti kwa vile ameonyesha nia ya kugombea URAIS mwaka 2015
 
Chadema ni chama kizuri sana! Tatizo kuna udikteta ndani yake
 
Mengine haya hapa...


Akina mama wakiwa hospital, DSM Tanzania.




Dr. Ulimboka baada ya kupata kipigo. LIWALO NA LIWE.

Huyu kijana ana mwili mkubwa kunizidi mimi, lakini kwa umri wake angeweza hata akawa mtoto wangu. Nani atakubali mtoto wake kupigwa kiasi hiki. Sitaki kuiona hii picha. Inanipandisha hasira. Naomba muitoe hii picha tafadhali! Jamani kina Sikonge na Mlenge, bado mnayo tu? Ujue inauma hii picha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…