Mwanaukweli
JF-Expert Member
- May 18, 2007
- 4,789
- 1,732
Wanajamvi nimeona leo tujadili mazuri ya CCM ambayo wameyafanya ili tuone upande mwingine wa shilingi maana hapa kila kitu kina pande mbili.
1. Uomoja kitaifa
2. Amani na Utulivu
3. Kuondoa udini
5. kuukema ukabila
6. Daraja la Kigamboni coming soon
7. kukubali upinzani
8. Ujenzi wa nyumba za wafanyakazi wote ambapo collateral ni deposits zao za NSSF na PFPF PPF
9. Ujenzi wa babrara nchi nzima
10. Ujenzi wa Udom na vuo vikuu vingi vya kumwaga.
11.
12.
13.
14.
Hayo matatu mekundu, yameshatoweka Tanzania.
1. Hakuna wakati ambapo CCM imekuwa ikitumia karata ya kuwagawa watu kwa makabila na kanda kama sasa. Sasa hivi CCM, kwa kuogopa M4C inadiriki kuwaambia watu wa mikoa na kanda fulani fulani hapa Tanzania kuvikataa vyama vya upinzani kwa hoja zisizo na mashiko. Hii inadhoofisha huo umoja wa kitaifa na chanzo ni CCM.
2. Amani na utulivu, baada ya kuua watu Arusha, Songea, kumtesa Dr. Ulimboka, mauaji ya Arumeru na Igunga (makada wa CDM) n.k n.k. naona amani na utulivu ni hadithi tu sasa.
3. Udini: Kwa sasa mjadala wowote hauwezi kukosa kuweka hoja za udini. Haijalishi mjadalauwe wa kisiasa, kiuchumi au kijaamii. Chanzo pia ni CCM kudhani kuwa inaweza kuwashikilia baadhi ya wanachama wake wasikitose kwa hoja ya dini!
Hayo mengine, kama yanafanywa kwa kodi ya wananchi na yamechelewa sana, yangepaswa kuwa tayari yameshafanyika, ni wajibu wa msingi wa serikali.