Idugunde
JF-Expert Member
- May 21, 2020
- 6,273
- 6,637
Ngumu kumeza. Nitarudi baadae naenda kulima shamba.Idu...
Ndiyo nasema kuwa unapenda kujadili historia hii lakini bahati mbaya huna ujuzi wa mengi katika somo hili.
Chukua muda uisome hii historia ndipo uje tufanya mjadala.
Kuondolewa majina ya Abdul Sykes, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Mshume Kiyate kwa kuwataja wachache katika historia ya TANU haikuwa uzembe.
Hassan Upeka aliyekuwa moja wa watafiti na waandishi wa historia hiyo chini ya Chuo Cha CCM Kivukoni anasema kuwa Dr. Mayanja Kiwanuka aliyekuwa kiongozi wa jopo alikataa kupokea taarifa za Abdul Sykes.
Haya nimeyaeleza katika kitabu cha Abdul Sykes.
Hiyo book review ya Brian Eccles naifahamu sana.
Nyingine ni ya John Iliffe na James Brennan.
Sishangai aliyoandika.
Ila nashangaa kwa nini hakueleza kuwa kuwa kweli hao, '' Abdul Muslim associates,'' hawamo katika historia lau kama mchango wao ni muhimu.
Yawezekanaje kuwa baba na watoto wake wote wameshika uongozi katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na wote hawamo katika historia ya TANU.
Baba muaisisi na wanae wote waasisi.
Tuje kwa Martin Kayamba.
Martin Kayamba hakuhusika katika kuunda AA.
Hili si jambo la sisi kuvutana.
Kleist Sykes kawataja wote walioasisi AA katika mswada wa kitabu alioandika kabla hajafa.
Sasa mswada huu ni kitabu: Daisy Sykes Buruku, ''Kleist Sykes The Townsman,'' ''Modern Tanzanians,'' Ilife (Ed) 1973.
Kleist Sykes yuko pia katika Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press, New York, 2011 na mwandishi wa maisha yake ni Mohamed Said.
Nahitimisha kwa kukufahamisha kuwa gazeti la Africa Events lililokuwa na makala yangu, ''In Praise of Ancestors,'' lilikusanywa lote na kutolea katika mzunguko lisisomwe.
View attachment 1797778
View attachment 1797782
Kleist Sykes muasisi wa AA 1929, Abdul, Ally na Abbas waaaisi wa TANU 1954 kadi no 2,3, na 7.
Nina mengi katika historia ya TANU.