Maximo: Jaja ni mfungaji tu

Maximo: Jaja ni mfungaji tu

Joined
Sep 3, 2014
Posts
11
Reaction score
3
KOCHA wa Yanga, Marcio Maximo na kiungo Mbrazil, Andrey Coutinho, wamewasikia Simba kisha wakacheka sana, unajua kwanini? Simba baada ya kumuona straika,Genilson Santos ¡®Jaja¡¯ juzi Jumatano Uwanja wa Taifa walibeza sana wakadai kumbe hana lolote ni maneno tu ya kishabiki mtaani.
Simba waliwakejeli Yanga kwa madai kwamba licha ya mchezaji huyo kufunga bao pekee kwenye mechi hiyo ya kirafiki dhidi ya Thika United ya Kenya, lakini hatishi kama Emmanuel Okwi wao au Pierre Kwizera.
Lakini Maximo na Coutinho wamewajibu kwa mkato na kuwaambia kwamba watulie ligi ianze ndiyo watamjua Jaja ni nani.
Maximo na Coutinho wamesisitiza kwamba Jaja hana mambo mengi kama wanavyodhani, yeye ni mtu wa kutengenezewa na kutupia tu hataki wala hajui vyenga. Maximo alisema: ¡°Unapomzungumzia Jaja huwezi kumfananisha na mchezaji kama Coutinho au Ngassa (Mrisho) au Niyonzima (Haruna).¡±
¡°Jaja ni mtu wa kusimama kati na kazi yake ni kufunga mabao, mpasie mpira afunge na siyo kutembea pembeni kusaka mpira, yeye anatumbukiza tu.¡±
 

Attachments

  • jaja.jpg
    jaja.jpg
    4.5 KB · Views: 960
Source...?

Natumaini Maximo amenukuriwa vibaya. Jaja yeye kazi yake kusimama?Apewe mpira tu ndipo afunge?
Hafai basi hata kwa "kurumangia...."
 
jaja taip yake kama zamoyoni mogela ila tatizo mzito ngoja apungue
 
Huyu maximo akimaliza misimu miwili yanga ntashangaa sana
 
Da kuna jamaaa kanimbia Jaja alikuwa mkuki na wa matunda brazil c mchezaj wa kulipwa ndala poleni
 
kama ndivyo Maximo anahitaji kupata kiungo wa chini mahiri mwenye oasi za mwendo tofauti na Dilunga anayepiga square pass hali inayomfanya Niyonzima kucheza kama namba sita na hivyo Jaja kukosa mlishaji
 
Huyu maximo akimaliza misimu miwili yanga ntashangaa sana
mechi ya juzi nilifanya katathmini, alipoingia alishangiliwa sana lakn baada ya dk chache mambo yaligeuka, kwa Jaja ni demotion ya kwanza
 
Ni kweli wapo wachezaji wa namna hiyo duniani na inategemea mfumo wa uchezaji timu inayoutumia. Lakini je, maximo ametengeneza huo mfumo wa viungo (box to box midfield) kukaba vizuri na kupanda kumpelekea jaja pasi za mwisho. Mifumo mingi inayotumika sasa duniani haitumii senta fowadi wa kusimama na mabeki wa mwisho wa timu pinzania na mingine haitumii senta fowadi kabisa. Kwa mpira wa siku hizi timu zinaanza kukaba kwenye eneo la timu pinzani (kwani ndio sehemu ambayo mipango ya kutafuta goli inapoanzia). Hivyo basi wanahitajika mafowadi wepesi wenye pumzi muda wote wa mchezo. Kama kweli jaja ni mfungaji mzuri anaweza kuperfom vizuri iwapo tu maximo atakuwa na viungo bora kabisa wenye pumzi na uwezo wa kudribble mpira toka nyuma mpaka mbele vinginevyo yatakuwa majanga.
 
Leo naona maneno ya Maximo yametimia...

Watu kimyaaaaaa......Jaja kawaziba midomo...
 
Back
Top Bottom