Mawifi zangu wamekua kero kwenye nyumba yetu

amanda cute

JF-Expert Member
Oct 27, 2016
244
456
Nilikua nasikia kuwa mawifi na mashemeji ni mwiba kwa wanandoa nikadhani ni uongo ila kwa sasa ndiyo nimeamini kiukweli. Kuna mawifi zangu kiukweli wamekua ni mwiba mchungu kwangu baada ya kuja kwetu. Nimewashindwa kiukweli kwa majungu na fitina kuwa mimi sifai kuwa na ndugu yao.

Wanadiriki kunisengenya kuwa nimemwekea limbwata mume wangu kuwa hawajali anajali tuu upande wangu. Imetokea siku za karibuni mume wangu kuwa karibu na mimi sana kwa kuzidisha upendo kwangu na kuniona mimi ni muhimu kwake.

Hii imepelekea kuwauma kweli kweli mpaka wanadai nimemwekea limbwata kumbe hakuna lolote hii inatokana na na mahaba ninayompa mpaka kapagawa tuu.

Jamani mawifi tulieni nimpe hubby kitu roho inataka. Inakera sana kwa kweli kuingilia mapenzi ya watu. Huu mchezo hauhitaji hasira acha nimpe vitu adimu.

Poleni na wale wote mnaosumbuliwa na mawifi zenu..
 
Wanawake wengine mna haki ya kusakamwa na mawifi zenu. Wakati mwingine akili ya kawaida tu inabidi ikuongoze umsaidie mwenzio afanye maamuzi sahihi.

Kuna watu wameshindwa kabisa kufanya jambo la maana kwa ndugu zao na wazazi wao. Ila upande wa pili wamejenga, wanalipa ada, wamewafanyia mambo mengi tu.

Hiyo sio akili wala mapenzi, mwanaume wa namna hii ni mpuuzi au kalogwa. Haiwezekani ujitie unajenga ukweni wakati kijijini kwenu wazazi wako wanaishi kwenye nyumba ya nyasi au bati zilizoezekwa kipindi nchi inapata Uhuru.

Kama na wewe umemloga mmeo wakusakame tu, ndio dawa iliyobaki.
 
Achana nao wengi ndio tabia zao kuchukia wake wa kaka zao pasi sababu za msingi. Ishi na mumeo cha muhimu humvunjii mtu heshima ukishindana nao utakimbia nyumba yako huku mumeo unamtaka.
 
Mitandao hii ndio imekua kimbilio la kutoa ya moyoni, kazi kweli kweli!!!
 
We dada post zako nyingi ni mambo ya vyumbani tu, hebu toka nje kidogo kuna vingi vinakupita
 
Nilikua nasikia kuwa mawifi na mashemeji ni mwiba kwa wana ndoa nikadhani ni uongo ila kwa sasa ndiyo nimeamini kiukweli .. Kuna mawifi zangu kiukweli wamekua ni mwiba mchungu kwangu baada ya kuja kwetu nimewashindwa kiukweli kwa majungu na fitina kuwa mimi sifai kuwa na ndugu yao ..

Wanadiriki kunisengenya kuwa nimemwekea limbwata mume wangu kuwa hawajali anajali tuu upande wangu... Imetokea siku za karibuni mume wangu kuwa karibu na mimi sana kwa kuzidisha upendo kwangu na kuniona Mimi ni muhimu kwake

Hii imepelekea kuwauma kweli kweli mpaka wanadai nimemwekea limbwata kumbe hakuna lolote hii inatokana na na mahaba ninayompa mpaka kapagawa tuu ..jamani mawifi tulieni nimpe hubby kitu roho inataka ....hii inakera sana kwa kweli kuingilia mapenzi ya watu ...huu mchezo hauhitaji hasira acha nimpe vitu hadimu..poleni na wale wote mnaosumbuliwa na mawifi zenu..
Vipi kuhusu ndugu zako hawamkeri mumeo?!
 
Nilikua nasikia kuwa mawifi na mashemeji ni mwiba kwa wana ndoa nikadhani ni uongo ila kwa sasa ndiyo nimeamini kiukweli .. Kuna mawifi zangu kiukweli wamekua ni mwiba mchungu kwangu baada ya kuja kwetu nimewashindwa kiukweli kwa majungu na fitina kuwa mimi sifai kuwa na ndugu yao ..

Wanadiriki kunisengenya kuwa nimemwekea limbwata mume wangu kuwa hawajali anajali tuu upande wangu... Imetokea siku za karibuni mume wangu kuwa karibu na mimi sana kwa kuzidisha upendo kwangu na kuniona Mimi ni muhimu kwake

Hii imepelekea kuwauma kweli kweli mpaka wanadai nimemwekea limbwata kumbe hakuna lolote hii inatokana na na mahaba ninayompa mpaka kapagawa tuu ..jamani mawifi tulieni nimpe hubby kitu roho inataka ....hii inakera sana kwa kweli kuingilia mapenzi ya watu ...huu mchezo hauhitaji hasira acha nimpe vitu hadimu..poleni na wale wote mnaosumbuliwa na mawifi zenu..
Ndio maana hawaolewi wanawajazia choo tu, sasa wana mpango gani au kaka yao akikuacha awaoe wao?
 
Why experts not able to explain what happened to MH370 from collected debris... Search area
must reconsidered
 
Wanawake! wanawake! wanaume tunawavumilia, mna vimaneno vya kutukera basi tu.
 
Back
Top Bottom