Matatizo ya utamkaji wa sauti r na l katika lugha ya kiswahili.

Daby

JF-Expert Member
Oct 26, 2014
33,641
75,656
Naomba tujadili juu ya hili kosa la kifonolojia ambalo watumiaji wa kiswahili wamekuwa wakilitenda panapo au pasipo kulijua na namna ya kuliepuka. Nitaeleza halafu kisha nguli wa hii lugha wataongezea.


Kwanza Sauti r na l ni zipi: hizi ni sauti ghuna ambazo hutamkwa panapokuwa na mrindimo wa nyuzi sauti wakati wa utamkaji. Yaani wakati mtu anapotamka hewa hutikisa nyuzi za sauti na hivyo kufanya kuwe na mrindimo katika ala za utamkaji. Kosa hili la kimatamshi la sauti r na l hutendwa saana na watumiaji ambao lugha yao mama haina sauti Aidha r au l mfano wasukuma na wakurya.

Nini kinapelekea kosa hili kutokea :

Athari ya lugha mama : kama lugha mama ya mtumiaji wa kiswahili haina sauti r au l uwezekano wa kufanya kosa hili ni mkubwa saana kwasababu ujifunzaji wa lugha ya kwanza hutegemea sana sayansi iliyopo kichwani ya lugha mama. Mifano nimetoa hapo juu.

Ufanano wa mahali pa matamshi : sauti r na l zote hutamkiwa kwenye ufizi...ulimi unapogusa ufizi. Licha ya r hutamkwa kwa kupigwapigwa na kukwaruzwa kwa ufizi wakati l hutamkwa kwa kukutanisha ncha ya ulimi na ufizi. Jaribu kutamka utaona.

Namna ya kuondokana na kosa hili la kimatamshi:
Mtumiaji wa lugha anapaswa Kuelewa hizi ni sauti mbili tofauti.
Pia anapaswa kuelewa utamkaji wake na mahali pa matamshi. r hutamkwa kwa kupigwapigwa na kukwaruzwa kwa ufizi. l hutamkwa kwa kukutanisha ncha ya ulimi na ufizi. Nimeleta hili hapa maana ukichungunza unaona matumizi ya r kwenye l na kinyume chake yamesharasimishwa na hadi kwenye machapisho na vyombo vya habati haya makosa yapo.
 
umenigusa,hapo kwenye R nikiitamka huwa inatetema kama 'rr' yaani hata haiandikiki.

Mkuu zile 'ara' za akina Sepenga vile;ila siilazimishagi
 
umenigusa,hapo kwenye R nikiitamka huwa inatetema kama 'rr' yaani hata haiandikiki.

Mkuu zile 'ara' za akina Sepenga vile;ila siilazimishagi
Pole mkuu hili ni tatizo na limeshachukuliwa kama ndiyo sahihi
 
Watanganyika pekee ndo muna huo upuuzi, kiswahili safi kiko huku zanzibar
 
Watanganyika pekee ndo muna huo upuuzi, kiswahili safi kiko huku zanzibar
Nafikiri haya ni mapungufu mtu anaweza kujisahihisha mwenyewe hasa kwa mtu aliyesoma kiswahili hata mpaka kidato cha 4. Ila watu sijui shida nini
 
sisi wasukuma hatunaga 'R' na maisha yasonga vizuuuri! :D:D penye 'R' tunaweka 'L' bila shaka mmetugeza!
 
Naomba tujadili juu ya hili kosa la kifonolojia ambalo watumiaji wa kiswahili wamekuwa wakilitenda panapo au pasipo kulijua na namna ya kuliepuka. Nitaeleza halafu kisha nguli wa hii lugha wataongezea.


Kwanza Sauti r na l ni zipi: hizi ni sauti ghuna ambazo hutamkwa panapokuwa na mrindimo wa nyuzi sauti wakati wa utamkaji. Yaani wakati mtu anapotamka hewa hutikisa nyuzi za sauti na hivyo kufanya kuwe na mrindimo katika ala za utamkaji. Kosa hili la kimatamshi la sauti r na l hutendwa saana na watumiaji ambao lugha yao mama haina sauti Aidha r au l mfano wasukuma na wakurya.

Nini kinapelekea kosa hili kutokea :

Athari ya lugha mama : kama lugha mama ya mtumiaji wa kiswahili haina sauti r au l uwezekano wa kufanya kosa hili ni mkubwa saana kwasababu ujifunzaji wa lugha ya kwanza hutegemea sana sayansi iliyopo kichwani ya lugha mama. Mifano nimetoa hapo juu.

Ufanano wa mahali pa matamshi : sauti r na l zote hutamkiwa kwenye ufizi...ulimi unapogusa ufizi. Licha ya r hutamkwa kwa kupigwapigwa na kukwaruzwa kwa ufizi wakati l hutamkwa kwa kukutanisha ncha ya ulimi na ufizi. Jaribu kutamka utaona.

Namna ya kuondokana na kosa hili la kimatamshi:
Mtumiaji wa lugha anapaswa Kuelewa hizi ni sauti mbili tofauti.
Pia anapaswa kuelewa utamkaji wake na mahali pa matamshi. r hutamkwa kwa kupigwapigwa na kukwaruzwa kwa ufizi. l hutamkwa kwa kukutanisha ncha ya ulimi na ufizi. Nimeleta hili hapa maana ukichungunza unaona matumizi ya r kwenye l na kinyume chake yamesharasimishwa na hadi kwenye machapisho na vyombo vya habati haya makosa yapo.
Imekuwa kawaida siku kiasi kwamba wengi wanaona kama sio kosa.Sababu ingine ni uvivu wa watumiaji lugha(wazungumzaji) kiasi kwamba hutafuta namna itakayowafanya watumie lugha kwa uwepesi na hivyo kupuuza kimandende hicho.
 
Imekuwa kawaida siku kiasi kwamba wengi wanaona kama sio kosa.Sababu ingine ni uvivu wa watumiaji lugha(wazungumzaji) kiasi kwamba hutafuta namna itakayowafanya watumie lugha kwa uwepesi na hivyo kupuuza kimandende hicho.
Hii sababu yako ipo kwa vijana wa Dar saana. Wanapenda kuifanya r iwe l mfano utaskia shauli yako...Dal es salaam
 
Mother tongues zimetuharibu jamani. . Wengine hata tufanyeje, tusameheane tu. . Kuandika twaweza jitahidi, ila kuongea mmmh
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom