Wana - JF,
Tunajua kuwa kwa mujibu wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA), Tanzania itabadilisha mfumo wa urushaji wa matangazo ya TV toka analogue kwenda digital kuanzia 31st December 2012.
Sasa, mimi naona kuwa muda umeisha, na TCRA haitoi elimu na matangazo ya kutosha kuhusu swala hili.
Wakati fulani TCRA walisema kuwa watu wanatakiwa kununua ving'amuzi ili wapate matangazo ya digital TV.
Nimezunguka madukani kuulizia ving'amuzi vya TV, mpaka sasa nimekutana na ving'amuzi vya StarTimes na Easy TV tu.
Ving'amuzi hivi vyote ni vya TV za kulipia matangazo ya TV kwa mwezi (usipolipia huoni matangazo).
Sasa hii ina maana kuwa watanzania wanalazimika kulipia matangazo ya TV kwa sababu ya kubadilika kwa mfumo wa TV kwenda digital !!
Kwenye maduka niliyotembelea sijaona ving'amuzi ambavyo havitahitaji kulipia matangazo ya TV, yaani ving'amuzi vitakavyoshika matangazo ya digital TV bila ya kulazimika kulipa malipo ya kila mwezi.
Wana-JF, naomba tuelimishane kuhusu swala hili ili tusije kujikuta tunakwama kupata matangazo ya digital TV ifikapo tarehe 31st December 2012.
Nawasilisha, na naomba maoni na michango yenu.