Mataifa yanaungana Tanzania tunatengana!!

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,578
8,600
Mimi nasikitika sana kuona sisi kamataifa moja tamaduni moja lugha moja tunakuwa na mawazo yakutengana kwakutafuta sababu eti muungano uvunjwe iwepo serikali ya zanzibar naserikali ya tanganyika na serikali ya muungano.

Mimi nasema huu niupungufu wa fikra nauhuni kwanini tusiwe nchi moja? kwanini wanaosema muungano uvunjwe uwa hawana hoja ya msingi?Au tuseme serikali ya zanzibar ndiyo inashinikiza muungano uvunjwe kwa kuwatumia watu?

Nakumbuka kwa jinsi walivyo anza kudai bendera wakadai wimbo wataifa!wamebadilisha katiba yao na kuweka vipengele vinavyokinzana na katiba ya Jamuhuri ya Muungano je Serikali ya JMT aioni kama hii nikasoro ilitakiwa ikemee kwa nguvu zote?

Kama ni hivyo je kesho watadai nini?
 
kinatuponza ni katiba isiyoeleweka, kwanini Tanganyika tumeingia kwenye serikali ya UMOJA yaani ya MUUNGANO huku wakijaa Wazanzibari wanotuzuga, kwao wakiwa na serikali makini na imara yenye hata majeshi, na nyinyi jidanganyeni kuwa sio jeshi, kwa wazenji wanatukoromea kwa nini? wako juu!!!! tumebaki mzigo kwao.
 
Hatujatengana na wala hatutatengana kwa ajili ya maslahi ya watu wachache. Tufikirie east african federation, kamwe sioni uwezekano wa muungano kuvunjika zaidi ya kelele za watu wachache ambao hawajui hata wanachokisema wala kukitaka, ni mbumbumbu tu.
 
Ni utamu wa Madaraka - kila mtu anataka kuwa na Sauti ya Mwisho

Achilia Mbali Mali, Ufisadi kuoneana Wivu
 
Hiyo East Africa Federation mnayoizungumzia haiondoi utaifa (Sovereignty) wa hayo mataifa husika!. Kama Kenya itabaki kuwa Kenya na nchi nyingine hivyohivyo! tunachotaka hapa ni haki sawa katika pande zote mbili. kAMA hakuna Tanganyika then Zanzibar isiwepo ibaki Tanzania. Nyie ni wa wapi?! moto umeisha waka na hakuna tena wa kuuzima. NI TANZANIA au TANGANYIKA NA ZANZIBAR!!!!!
 
Kwangu mimi Muungano ni tunu na dhahabu nisioweza kumruhusu mtu yeyote kuchezea eti kaona jua linachomoja Uarabuni; je likija kuzama magharibi ndio tutaanza kuukimbilia tukaungane tena??? Hadithi za sijui iliundwa na CIA mara Mwl Nyerere na Karume tu wala mtu asiniambie.

Tukishavunja muungano halafu wale watoto wenye familia mchanganyiko juu chini kati ya Bara na Visiwani ndio tutaanza kuwaeleza nini???

Hivi kuabudu ni mpaka nchi kujiunga na OIC bila hata kufikiria ustawi wa watoto niliowataja hapo awali kweli?? Upuuzi huo tukazungumze mambo mengine ya kusaidia kutunisha mikate ya familia zetu pale Katiba itakapoundwa upya kuendana na matakwa ya sasa.

Sote tupanue zaidi akili jinsi gani ya kujadili Muungano kiuwazi kabisa kwenye mkutano mkuu wa taifa wa wananchi tukijiundia KATIBA yetu wenyewe kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii.

Lengo letu wakati wote wa mjadala huo uwe ni kule kutafuta njia bora zaidi kunawirisha Muungano wa Tanzania basi!!!
 
Watoto wa pande mbili watachagua nchi wanayotaka ikiwa ya tanganyika au zanzibar mbona swali lako ni rahisi sana. Mie nimezaliwa znz lkn leo niko tanganyika napigana vikumbo na wanyamwezi,makonde,wakurya,wachaga etc so sio lazima mtu akae nchi aliyozaliwa. We vipi au umetoka kunywa pombe saivi maana leo ni j'1
 
Ni utamu wa Madaraka - kila mtu anataka kuwa na Sauti ya Mwisho

Achilia Mbali Mali, Ufisadi kuoneana Wivu

yap. Na kamwe hatuwezi kusonga mbele.
Hivi sisi tunaweza kweli kuamua kuungana nchi zote za africa tukatoa raisi mmoja, waziri mkuu mmoja kuokoa resources iwapo kamuungano haka tunashindwa kukaendeleza!!
 
Kwa sababu sisi ni imara kuliko iliyokuwa Soviet Union na kwa kuwa sisi ni binadamu tofauti na wao na tunaishi Dunia nyingine Muungano huu hautavunjika!!! Imefika mahali hata nchi ambazo zinashirikiana ktk mambo kadhaa sisi tunadanganyana hapa kuwa zimeungana! Jamani wekeni wazi faida za muungano kwa Tanganyika. Pia kumbukeni chenye mwanzo....
 
Ingelikuwa kweli muungano hu mzuri ambao wazanzibar wanahaki sawa na watanganyika ndani ya serikali ya muungano basi tungefikiria kuwa kitu kimoja taifa moja,lakini hakuna hilo ni ubaguzi wa hali ya juu,tumetupiliwa mbali wazanzbari,tunateseka tunanyanyaswa na muungano,maisha yamekuwa magumu zanzbar,pia elimu tunafanyiwa ubaguzi hasa ya juu,kikichezo,afya,kijamii,

Kwa hio muandishi wa mada hii unaonekana hukufuatilia makongamano ya zanzbar juu ya muungano jinsi wanavyotumia hoja za msingi,walikuwa hawana hoja ni viongozi wa muungano ambao ni watanganyika kama Pinda.

Kwa kukuelewesha zaidi,zanzibar ni nchi,hakuna nch yoyote duniani inayotaka iungane na nchi nyengie ikisha uvunje utaifa wake,hakuna hilo,hata huo muunganno wa EAC,KILA MTU ANACHAKE,

Sikiliza mahojiano ya leo mchana baina ya Zitto Kabwe N mzee Nassor MOYO Juu ya muungano.

Taafifa ya bahari hii kutoka radio ya ujerumani fungua hapo chini

Redio | Mzalendo.net

Sikiliza habaya ya 15:00-16:00

Acheni kuropoka mpaka Zitto kabwe ameongea kuwa wazanzbari wanatumia hoja za msingi kudai haki zetu,zitto ni msomi na kweli kasoma na anaelewa nini anacho kifanya,na ndio maana hapa tanzania amekubalika.
 
Back
Top Bottom