Maswali yangu kuhusu tume ya uchaguzi.

DUBULIHASA

JF-Expert Member
Nov 26, 2016
3,563
5,955
Tayari Rais Magufuli ameteua viongozi wa tume ya uchaguzi hususani mwenyekiti wa tume pamoja na makamu wake. Ningependa niwaulize machache wanaccm, wapinzani pamoja na wasio na vyama maswali machache, unapojibu swali/ maswali unaweza ukasema au usiseme uko kundi gani kutoka katika makundi hayo matatu. Maswali yangu ni kama ifuatavyo

-Je kuna ulazima wowote rais kuchagua tume ya uchaguzi bila kuwashirikisha upinzani kama wadau wakubwa kwenye tume? Na kwa nini?


-Je wale waliochaguliwa na rais kwenye tume hawawezi kumpendelea rais na chama chake? Toa sababu.

-Je ni vipi wapinzani wataweza kushinda uchaguzi kihalali chini ya tume iliyochaguliwa na rais ambaye pia naye ni mshindani kwenye uchaguzi?

-Je wapinzani wamechukua hatua gani kuhakikisha kunakuwepo na tume huru ya uchaguzi?

-Je iwapo kama hawatakubaliwa kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi wapinzani watafanya nini?

TAFADHALI JIBU KISTAARABU KWA SABABU DHUMUNI NI KUJENGA SIO MASHINDANO.
 
Katiba yetu inampa rais kuteua watumishi wa n.e.c,haijalishi huyo rais anatoka chadema au c.c.m au chama chochote nje ya hao!
Upinzani kugomea uteuzi wa rais ni kupoteza muda,sana sana waende bungeni na kupeleka hoja ya mswada wa mabadiliko ya katiba au baadhi ya vifungu vinavyompa rais mamlaka makubwa mpaka kile kifungu kinachokataza matokeo ya urais kuhojiwa!
Dhamira kama ipo wanaweza dai hata katiba ya warioba!
Ila wasiwasi wangu ni kuwa sijaona Upinzani wakufanya hivyo kama ilivyo Raila Odinga na CORD yake kule Kenya!
So,the ball is in their court!
 
Katiba yetu inampa rais kuteua watumishi wa n.e.c,haijalishi huyo rais anatoka chadema au c.c.m au chama chochote nje ya hao!
Upinzani kugomea uteuzi wa rais ni kupoteza muda,sana sana waende bungeni na kupeleka hoja ya mswada wa mabadiliko ya katiba au baadhi ya vifungu vinavyompa rais mamlaka makubwa mpaka kile kifungu kinachokataza matokeo ya urais kuhojiwa!
Dhamira kama ipo wanaweza dai hata katiba ya warioba!
Ila wasiwasi wangu ni kuwa sijaona Upinzani wakufanya hivyo kama ilivyo Raila Odinga na CORD yake kule Kenya!
So,the ball is in their court!
Hapo kweli mkuu na ndio maana kwa mtu unayeona mbal still malalamiko ya wapinzan baada ya uchaguzi yatakuwa yaleyale bila kubadilisha hivi vifungu vya katiba.
 
Rais huyo huyo ndo mwenyekiti wa ccm na huyo huyo ndo mgombea urais ccm na ndo huyo huyo anamteua mwenyekiti wa NEC(mtu wa kutangaza matokeo ya urais). Afrika bado sana, mambo mengine haya-make sense kabisa.
Mm huwa nabaki nashangaa sans kila uchaguz wapinzan wanadai watashinda kwa kishindo wakati mambo yako hvhv. HILI NO SWALA LA KULIPIGANIA WAPINZAN KABLA YA SWALA LOLOTE
 
Katiba yetu inampa rais kuteua watumishi wa n.e.c,haijalishi huyo rais anatoka chadema au c.c.m au chama chochote nje ya hao!
Upinzani kugomea uteuzi wa rais ni kupoteza muda,sana sana waende bungeni na kupeleka hoja ya mswada wa mabadiliko ya katiba au baadhi ya vifungu vinavyompa rais mamlaka makubwa mpaka kile kifungu kinachokataza matokeo ya urais kuhojiwa!
Dhamira kama ipo wanaweza dai hata katiba ya warioba!
Ila wasiwasi wangu ni kuwa sijaona Upinzani wakufanya hivyo kama ilivyo Raila Odinga na CORD yake kule Kenya!
So,the ball is in their court!

Mkuu
Usije linganisha Kenya na Tanzania.
Wenzetu wakenya wameendelea sana kwenye kuelekea demokrasia ya kweli.
Sisi ndo kwanza tunazidi kurudi nyuma.
Wapinzani hawana nafasi na hawaheshimiwi kama nao ni sehemu yà kuleta changamoto la kisiasa.
Tanzania inaendeshwa na vyombo vya dola kama itakavyo kuwa tume hiyo ya uchaguzi kwani wote ni wateule wa Rais hivyo wapo kwa ajili ya aliye wateua.
-vyama vya siasa vyote viko kwa masilahi ya vyama vyao ndo maana hawana dhamira ya kuunganisha mawazo ili kunenga nchi. Kila chama kipo kwa lengo la kutetea masilahi yake.
-Kusudi la kukandamiza katiba ya wananchi a.k.a ya Warioba lengo lilikuwa kulinda vifungu vinavyo nyima wananchi kuhoji na kuvibadili.
-Hakuna tume huru ya uchaguzi, vyombo vya dola vinatumika kulinda watawala,mahakama pamoja na kuwa na learned judge's wameshindwa ku apply doctrine ya separation of power nao wanatumika kisiasa hivyo tusitegemee kuwa na Demokrasia ya kweli.
Angalizo:
Wale waliopewa dhamana ya kuiongoza nchi hii wasituingize kwenye majanga. Kwani dalili zinaonyesha kuwa wamejisahau kuwa tumewapa dhamana na wala siyo kwamba wao ni naboss wetu. Wangejitambua wangetuheshimu kama waajiri wao.
Mimi hadi sasa sijajiunga na chama chochote. Hivyo natoa maoni yangu kama Mtanzania.
 
Rais huyo huyo ndo mwenyekiti wa ccm na huyo huyo ndo mgombea urais ccm na ndo huyo huyo anamteua mwenyekiti wa NEC(mtu wa kutangaza matokeo ya urais). Afrika bado sana, mambo mengine haya-make sense kabisa.
Hivi walikuwa wanatunga katiba waliwaza nini kuingiza vipengele kama Hivi lakini maana no non sense kabisa ndio sababu hata ya kutufikisha hapa
 
Back
Top Bottom