Maskini Nchi Yangu!!

Maskini Nchi Yangu!!

Dr.Menuka

Member
Joined
Aug 10, 2013
Posts
14
Reaction score
2
Nini kifanyike nchi inapokosa wa kuisemea?? Tumeambiwa nchi imesimama haiendelei tena hali vijana wake wapo bize na malumbano ya kidini na siasa! Ndg zangu,yapo mambo mengi yanazungumzwa sasa ktk mitandao mbalimbali lakini kwa bahati mbaya wazungumzaji wote wanatofautiana mawazo(hawana umoja) kulingana na dini ama chama cha siasa!

Itoshe kusema kuwa wote hatuelewani lugha kwa kuwa kila mtu anavutia kwake ,halafu kwa mlengo huo tunasema kuwa tunataka kuijenga nchi yetu!Kwa kawaida nchi haiwezi kujengwa ktk utofauti wa wajenzi wenyewe ktk itikadi na ubaguzi wa imani.

Wana JF wakati umefika tujue kuwa hatima ya nchi yetu ipo mikononi mwetu bila kujali tofauti zetu,tunatakiwa kuijenga nchi hii! Ni ujinga sana na utumwa wa kifikra kutetea jambo la hovyo eti kwa kuwa limesemwa na kiongozi wako ama wa dini au siasa" Ujinga huu tuukatae! ukweli usemwe wazi na uovu ukemewe wazi na sote bila kujali tofauti za imani ama itikadi ili tujenge nchi ambayo sasa haina wa kuisemea.

Nchi ni vijana na wao ni sisi,utumwa wa fikra ni mauti ya taifa.Lazima tujiulize kuwa nani katufikisha hapa? Tutatokaje hapa? Nani atatutoa hapa? na lini tutatoka hapa?

Mimi nasema 'NCHI YANGU KWANZA'
 
Ndugu yangu kutoka hapa tulipo inahitajika jitihada za ziada vijana ndo hao wanafifishwa hakili kwa madawa ya kulevya, na waliowengi wanarubuniwa kwasababu ya ufukara na hizi ni strategy za watawala ili waendelea kutawala, so mzee tunakazi ya ziada simchezo.
 
Watanzani wengi tunashabikia wanyarwanda wafukuzwe waende kwao hata wale ambao walikuwa na vijimali vyao wanaondoka na kuviacha. Utu sio lazima awe mtanzania mwenzako, kama uamuzi huo umepita basi wapewe muda kufungasha kila kilicho chao kwa amani. Tusiwahukumu wanyarwanda wote kwa kauli ya kagame, wale bado ni majirani zetu tu.
Wengine wanaenda mbali na kusema kagame alete mchezo tumchape, anayesema hivyo ukimuuliza swali hili: unajua status ya jeshi lako au lile la rwanda, jibu lake toka rohoni litakuwa hajui ila la mdomoni atakwambia acha tanzania ni noma kwenye vita.
Kwa taarifa ile ya uganda mpaka leo tunailipia, tukiingia nyingine wale tunaowaona viongozi wetu watachukua kila kitu na kuhamishia familia zao nje ya nchi, utawaona ukipotezaa na watoto wako unaowapenda hivi hivi wawe wadogo au wakubwa. Kila jambo litasingiziwa vita, na vihela vyenu vya bank wata vi hold kwa madai vita ilivuruga system za kibenki. msiombe jamani.
Binafsi naogopa,
 
anayeshabikia vita hana akili
 
Tunaitaji mtu mwenye maono huru ya kuliongoza taifa,,anaesema na kutenda,,mwenye kuapa kimoyo moyo kuwa kapewa dhamana ya kuliweka taifa letu kwenye list ya nchi tajiri dunia,,taifa lenye watu wasio na njaa,,watu huru wa kusema na kusikilizwa,,tunaitaji mtu ambae hata hajawahi kuwa ndani ya Serikali lakini aliyetokea dalaja la wakulima ama wafugaji mwenye kuhisi umaskini wa mkulima na shida za mfugaji/mkulima ni zake..Hatuwezi tolewa hapa kwa watu hawa walioko kwenye mfumo.
 
Kak umesema vyema lkn kwa tulivo ss vijana wenye kupenda ishabiki wa kijinga,je mambo hay yatawezekana?
 
Watu wanasikia vita tu huko na huko lakini ni mbaya. vita ni pesa, pesa tunayo???? Hivi karibuni nilisikia nchi inataka kufilisika watu hawalipwi mishahara na kadhalika. Vita ikianza na hiyo mishahara msahau.
 
Umsema kila kitu safi lakini nahisi umechemka hapa kwenye red...."Lazima tujiulize kuwa nani katufikisha hapa? Tutatokaje hapa? Nani atatutoa hapa? na lini tutatoka hapa.
Inabidi tutambue kuwa tuna uwezo wa kuwa zaidi sana ya hapa tulipo,lakini tukiishia kwenye siasa na dini,wengi wetu hatuna muda wa kufanya mambo ya maendeleo.Watu wa kututoa hapa wapo ila wanaogopa gharama yake.Ya nyuma hayasaidii sana ,maana nao walifanya kwa kadri walivyoona.Kutoka hapa tulipo ni gharama sana.
Ningekuwa najua siasa na uongozi!ningejaribu hata ku copy.Mungu ibariki TZ
 
Back
Top Bottom