Masikitiko yangu kuhusu Chama Changu

Masikitiko yangu kuhusu Chama Changu

DURUYAPILI

Senior Member
Joined
Apr 23, 2015
Posts
132
Reaction score
47
Habari wadau

Nimeifuatilia move hii ambayo wengine wanaoita kwa majina tofauti tofauti kama season nk. mimi kama mpenda mabadiliko na maendeleo ya nchi yangu, maumivu ya moyo huzidi hasa pale inapoonekana kuna kitu hakiendi sawa harafu watu wanajivika miwani nakuona kana kwamba hakuna kinachoendelea.

Namkubali sana kiongozi wangu wa chama taifa. mh. Elkael Mbowe, ni mtu shupavu, mpiganaji, mwenye uwezo wa kuchukua maamuzi magumu kwa wajasilia mali tungemwita ni risk taker mara anapoona opportunities katika field ya siasa. Nitakuwa ni mnyimi wa fadhira kama nitaacha kumtaja mh. Mbowe kuwa ndye alini inspire katika harakat za siasa za vyama vingi mwaka 2005 ambapo aliipeperusha bendera ya chama. hakika nilifrijika sana.
Naomba nisifanye lisara ndefu sana niende kweye point ya msingi.

.pamoja kwamba mzee MBOWE namwita ni risk taker mzuri na mshauri maamuzi yake yaelezwe wazi kwa wadau.
Nakumbuka ktk hotuba yake alitamka maneno haya......kama kuna watu wanaona kitendo cha mimi kumkaribisha mh. lowasa basi nawaombea kwa Mungu busara waweze tambua.....na kama kufukuzwa uenyekiti kwa hili nipo tayari.......
jamani uongozi mzuri ni kuwa transparent kwa maamuzi ufanyayo kwa watu na siyo unaposhindwa kuwaeleza vizuri watu wakaelewa kwamba huyu mtu mlituaminisha ni fisadi na fisadi papa harafu leo anakuwa msafi tena ghafra et watu wasishangaee....?.na kama watu hawamuelewi waombewe kwa Mungu kana kwamba jambo hili ni Nmuujiza ambao hauwezi kueleweka mpaka maombi?.

Ni kweli tunapenda mabadiliko lakini tunapenda mabadiliko yenye kufuata democrasisia na uwazi ndo nguzo yake. hivi inakuwaje mtu aliyejulikana ni fisadi kwa jamii nzima tunamkaribisha ktk chama bila mashart yoyote ile na kama hiyo haitoshi anapewa lidhaa ya kugombea urais bila competition yoyote ile?

lnawezekana mwisho mzuri which is still probability, lakini means ilotumika ni mbovu je mshikamano wetu utaendelea kama sasa. tumeshafikiria kama tutashindwa uchaguzi huu vipi itakuwa hatima umoja na mshkamano wetu kama chama. je huyu tuliyemkaribisha ataendelea kutuunga mkono au lengo lake ni uras tu?

pamoja na hayo yote tunelidhiana vizuri ndani ya chama nakujiridhisha kama letu ni moja na kila mmoja wetu anaweza kusimama kwa ujasiri kabisa kuyatetea maamuzi yalofikiwa au awchache tu ndo watakoweza.

nasema hivi kwani kuna kila moja anaongea la kwake kuhusu mzee wangu dr. slaa na kijana mchapa kazi mh Mnyika ambao kimsingi mkubwa wa chama chetu tukuka. lakini kwa bahati mbaya sijamskia kiongoz yeyote akisimama kutolea maelezo kuhusu hili na wala sijasikia wahusika wenyewe wakisema lolote zaid ya kanusho la dr. slaa jana harafu tunaendelea kutumainishiwa et mambo shwari. kwa mwanachama mwenye kukipenda chama chake leo na miaka thelathuni ijayo angependa kujulishwa kuhusu hali ya kisiasa ndani ya chama chake hasa ktk wakat huu mgum.

kuna watu wanadiriki hata kumtusi mzee wetu et anaziraziri na kejeri nyingi , mtu ambaye kimsingi amekifia chama na kuukumba ulemavu wa kudumu halafu tuseme et anazirazira? kwa nini asizile wakati wa mapambano makali ya kudhalilishwa na askali na kuumizwa?

ombi langu kwa viongozi wajaribu kikaa na mzee huyu na kufikia agreement nzuri.. kwan hakuna asiyejua kuwa hyu mzee ni lulu si tu kwa chama bali kwa taaifa kwa falsafa na misimamo yake ktk kulikomboa taifa hili kwa changamoto nyingi badala ya kuanza kumdhihaki bila kujua what wrong has gone somewhere.

najua uzi huu utawakwaza wengi lakini ukweli lazima uwe spoken out ili kama tumekosea somewhere turekebishe ili tujenge chama bila kuharibu dira na malengo ya kulikomboa taifa letu

Namaliza kwa kusema THE MEANS SHOULD JUSTIFY THE END FOR DECISION TO BE RETIONAL AND NOT THE END TO JUSTIFY THE MEANS
 
Kinachonisikitisha zaidi ni kwanini Dr alikatwa na kitengo juu kwa juu? Kwanini hakupewa na fasi na yeye kuchukua fomu? Jibu ni...Dr anawatu wengi zaidi wanaomkubali na kama angepewa nafasi ya kuchukua fomu, angemtupilia mbali Lowassa.
Lesson learnt: chadema ina wenyewe
 
Hii ni vita kati ya CCM na wanamabadiliko, silaha yoyote yaweza tumika ili kushinda vita hii, kwa wale mnaochgua silaha katika vita mtatusamehe, kwa sasa EL ndio silaha muafaka kuingamiza CCM wala hatutaangalia mazara ya silaha hiyo kwasasa. Dk Slaa na kundi lako mtusamehe.
 
Habari wadau

Nimeifuatilia move hii ambayo wengine wanaoita kwa majina tofauti tofauti kama season nk. mimi kama mpenda mabadiliko na maendeleo ya nchi yangu, maumivu ya moyo huzidi hasa pale inapoonekana kuna kitu hakiendi sawa harafu watu wanajivika miwani nakuona kana kwamba hakuna kinachoendelea.
Namkubali sana kiongozi wangu wa chama taifa. mh. Elkael Mbowe, ni mtu shupavu, mpiganaji, mwenye uwezo wa kuchukua maamuzi magumu kwa wajasilia mali tungemwita ni risk taker mara anapoona opportunities katika field ya siasa. Nitakuwa ni mnyimi wa fadhira kama nitaacha kumtaja mh. Mbowe kuwa ndye alini inspire katika harakat za siasa za vyama vingi mwaka 2005 ambapo aliipeperusha bendera ya chama. hakika nilifrijika sana.
Naomba nisifanye lisara ndefu sana niende kweye point ya msingi.
.pamoja kwamba mzee MBOWE namwita ni risk taker mzuri na mshauri maamuzi yake yaelezwe wazi kwa wadau.
Nakumbuka ktk hotuba yake alitamka maneno haya......kama kuna watu wanaona kitendo cha mimi kumkaribisha mh. lowasa basi nawaombea kwa Mungu busara waweze tambua.....na kama kufukuzwa uenyekiti kwa hili nipo tayari.......
jamani uongozi mzuri ni kuwa transparent kwa maamuzi ufanyayo kwa watu na siyo unaposhindwa kuwaeleza vizuri watu wakaelewa kwamba huyu mtu mlituaminisha ni fisadi na fisadi papa harafu leo anakuwa msafi tena ghafra et watu wasishangaee....?.na kama watu hawamuelewi waombewe kwa Mungu kana kwamba jambo hili ni Nmuujiza ambao hauwezi kueleweka mpaka maombi?.
Ni kweli tunapenda mabadiliko lakini tunapenda mabadiliko yenye kufuata democrasisia na uwazi ndo nguzo yake. hivi inakuwaje mtu aliyejulikana ni fisadi kwa jamii nzima tunamkaribisha ktk chama bila mashart yoyote ile na kama hiyo haitoshi anapewa lidhaa ya kugombea urais bila competition yoyote ile?
lnawezekana mwisho mzuri which is still probability, lakini means ilotumika ni mbovu je mshikamano wetu utaendelea kama sasa. tumeshafikiria kama tutashindwa uchaguzi huu vipi itakuwa hatima umoja na mshkamano wetu kama chama. je huyu tuliyemkaribisha ataendelea kutuunga mkono au lengo lake ni uras tu?
pamoja na hayo yote tunelidhiana vizuri ndani ya chama nakujiridhisha kama letu ni moja na kila mmoja wetu anaweza kusimama kwa ujasiri kabisa kuyatetea maamuzi yalofikiwa au awchache tu ndo watakoweza.
nasema hivi kwani kuna kila moja anaongea la kwake kuhusu mzee wangu dr. slaa na kijana mchapa kazi mh Mnyika ambao kimsingi mkubwa wa chama chetu tukuka. lakini kwa bahati mbaya sijamskia kiongoz yeyote akisimama kutolea maelezo kuhusu hili na wala sijasikia wahusika wenyewe wakisema lolote zaid ya kanusho la dr. slaa jana harafu tunaendelea kutumainishiwa et mambo shwari. kwa mwanachama mwenye kukipenda chama chake leo na miaka thelathuni ijayo angependa kujulishwa kuhusu hali ya kisiasa ndani ya chama chake hasa ktk wakat huu mgum.
kuna watu wanadiriki hata kumtusi mzee wetu et anaziraziri na kejeri nyingi , mtu ambaye kimsingi amekifia chama na kuukumba ulemavu wa kudumu halafu tuseme et anazirazira? kwa nini asizile wakati wa mapambano makali ya kudhalilishwa na askali na kuumizwa?
ombi langu kwa viongozi wajaribu kikaa na mzee huyu na kufikia agreement nzuri.. kwan hakuna asiyejua kuwa hyu mzee ni lulu si tu kwa chama bali kwa taaifa kwa falsafa na misimamo yake ktk kulikomboa taifa hili kwa changamoto nyingi badala ya kuanza kumdhihaki bila kujua what wrong has gone somewhere.
najua uzi huu utawakwaza wengi lakini ukweli lazima uwe spoken out ili kama tumekosea somewhere turekebishe ili tujenge chama bila kuharibu dira na malengo ya kulikomboa taifa letu
Namaliza kwa kusema THE MEANS SHOULD JUSTIFY THE END FOR DECISION TO BE RETIONAL AND NOT THE END TO JUSTIFY THE MEANS

Mkuu ubarikiwe sana kwa kuvunja ukimya
 
Twende kazi 4umovement hamtuwezi
 
Mimi nikiwa kama mwana chadema sipingani na kitendo cha lowasaa kuhamia kwetu.....bali napingana na kitendo cha yeye kupewa nafasi ya kugombea tena kwa kuweka sharti la bila kupingwa....huu ni uminywaji wa demokrasia ndani ya chama ambapo kama ambavyo lowasa alivyo na haki ya kugombea ndivyo wanachama wengine walivyo na haki ya kugombea....kwanini msingeacha kura ziamue ili kila mtu aridhike......
Bado wana chadema wengi tuna imani na dk slaaa.....
Ki ukweli mpaka sasa kura yangu ya uraisi ipo njia panda.......nangojea tamko au kauli ya dk slaa ndipo nitafanya maamuzi..
 
Mimi nikiwa kama mwana chadema sipingani na kitendo cha lowasaa kuhamia kwetu.....bali napingana na kitendo cha yeye kupewa nafasi ya kugombea tena kwa kuweka sharti la bila kupingwa....huu ni uminywaji wa demokrasia ndani ya chama ambapo kama ambavyo lowasa alivyo na haki ya kugombea ndivyo wanachama wengine walivyo na haki ya kugombea....kwanini msingeacha kura ziamue ili kila mtu aridhike......
Bado wana chadema wengi tuna imani na dk slaaa.....
Ki ukweli mpaka sasa kura yangu ya uraisi ipo njia panda.......nangojea tamko au kauli ya dk slaa ndipo nitafanya maamuzi..

Mkuu kwani usiongee na alie/waliofanya maamuzi mpaka kufikia hapa?au tunajivika upofu kana kwamba Ni Dr.Slaa alieamua haya yaliotokea yatokee??unapojikwaa unaangalia ulipojikwaa?Au ulipoangukia???
 
Maajabu nchi zetu hayataisha. Wanaopigania demokrasia ndio wanaoiminya. Kumpitisha mgombea bila kumshindanisha na wengine si demokrasia. Tukatae mambo haya.
 
Hii ni vita kati ya CCM na wanamabadiliko, silaha yoyote yaweza tumika ili kushinda vita hii, kwa wale mnaochgua silaha katika vita mtatusamehe, kwa sasa EL ndio silaha muafaka kuingamiza CCM wala hatutaangalia mazara ya silaha hiyo kwasasa. Dk Slaa na kundi lako mtusamehe.

Hauna tofauti na wale wapiganaji wa Alquaeda ambao wao waamini ili uende peponi unaweza kuua kwanza na hapo unapata thwawabu, jambo jema halifikiwi kwa kutekeleza jambo hovu hata siku moja na ndo maana inasemwa kwaba the means justify the end ..means iliyotumiwa na Mbowe ni absolutely questionable
 
Maajabu nchi zetu hayataisha. Wanaopigania demokrasia ndio wanaoiminya. Kumpitisha mgombea bila kumshindanisha na wengine si demokrasia. Tukatae mambo haya.

Wafute jina la chama kwanza, haiwezekani ukahiubiri demokrasia alafu pembeni umepakata utemi na ubwanyenye ..haiwezekani!
 
Mkuu kwani usiongee na alie/waliofanya maamuzi mpaka kufikia hapa?au tunajivika upofu kana kwamba Ni Dr.Slaa alieamua haya yaliotokea yatokee??unapojikwaa unaangalia ulipojikwaa?Au ulipoangukia???

Binafsi naamini kabisa kwa hili mwenyekiti wangu Mbowe amejikwaa....hangepaswa kufanya hili ambalo amelifanya hasa kwa nyakati hizi....hizi ni nyakati ambazo watanzania wameaminishwa kuwa kikwazo cha maendeleo ya taifa lao ni ufisadi uliokithiri ndani ya chama tawala...na wahusika wanafahamika kwa kutajwa hadharani na hao hao viongozi wetu....sasa leo iweje hao hao tulioaminishwa kuwa ni vikwazo vya maendeleo ya taifa hili kwa ufisadi wao...iweje leo wakaribishwe pembeni ya wapenda mabadiliko huku tukiambiwa kuwa ni msafi......hili ni kosa kubwa....
 
Hii ni vita kati ya CCM na wanamabadiliko, silaha yoyote yaweza tumika ili kushinda vita hii, kwa wale mnaochgua silaha katika vita mtatusamehe, kwa sasa EL ndio silaha muafaka kuingamiza CCM wala hatutaangalia mazara ya silaha hiyo kwasasa. Dk Slaa na kundi lako mtusamehe.

We mwehu! Hujui unachosema. Hivyo kwako chama ni bora kuliko taifa? Jipime,acha ubinafsi!
 
Kinachonisikitisha zaidi ni kwanini Dr alikatwa na kitengo juu kwa juu? Kwanini hakupewa na fasi na yeye kuchukua fomu? Jibu ni...Dr anawatu wengi zaidi wanaomkubali na kama angepewa nafasi ya kuchukua fomu, angemtupilia mbali Lowassa.
Lesson learnt: chadema ina wenyewe

na wenyewe ndio sisi tunaomwelewa Mh. Mbowe.
 
Hii ni vita kati ya CCM na wanamabadiliko, silaha yoyote yaweza tumika ili kushinda vita hii, kwa wale mnaochgua silaha katika vita mtatusamehe, kwa sasa EL ndio silaha muafaka kuingamiza CCM wala hatutaangalia mazara ya silaha hiyo kwasasa. Dk Slaa na kundi lako mtusamehe.

Unacho sema nikweli .na ataa ufisadi wa Lowasa kishatolea ufafanuzi.kama ni uaminifu kwa chadema ameshaonesha tena kwa kiwango cha juu .ile tuu kusema wazi ni mamlaka ya juu ndio inahusika na richmond .tosha kabisa kuonyesha uaminifu ulio tukuka kwa chadema.laita kina mwakyembe wange mhoji kipindi kile anajiuzulu akalisema hili.hilikua hatuna uongozi huu tulionao mpaka sasa.sasa ina maana Dr Slaa ajaliona hili.alafu kwanini Slaa amelichukua hili swala binafsi sana.kwanini asingetushirikisha na sisi wanachama wa chadema anaotuongoza .why !!!??? Anyway naomba Mungu isiwe ni kweli Dr Slaa kipenzi wetu anatusaliti.
 
Chadema ni chama kinachoendeshwa kwa misingi ya ulaghai na mkono wa chuma.
 
Back
Top Bottom