Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 57,240
- 90,297
Masheikh wa BAKWATA wamekomalia propaganda ya kwamba raia wakidai au kuzitka haki za msingi za kijami wakati huu ni kuvunja amani amani ya nchi. Huu ni uongo mtupu, propaganda chafu na ubinafsi. Watu wanaodai haki sio wavuruga amani wa nchi bali ni watu wanaotaka nchi bora na yenye usawa kuliko tuliyo nayo sasa.
Wapigania haki au wanaozidai haki wanataka;
1. Wafanyabiashara wafanye biashara zao na kufanikiwa bila kulazimika kujikomba na kuwa chawa kwa CCM. Wasilazimike kuchangia shughuli za CCM au za mwenge au kutundika picha za Samia katika biashara zao ila kupata unafuu wa kibiashara.
2. Wafanyakazi wa umma wafanye shughuli zao kwa bila mashinikizo ya CCM
3. Raia wachague viongozi wao kwa uhuru na haki, kura zihesabiwe na ziwe na maana
4. Ufisadi, Rushwa na upendeleo serikalini vikomeshwe.
5. Rasilimali za umma zisiuzwe kiholela au kutolewa kwa mikataba ya hovyo
6. Wakosoaji na wapinzani walale majumbani mwao bila hofu ya kutekwa, kupotezwa , kuuwawa au kufunguliwa kesi za mchongo.
7. Ajira nzuri na unafuu wa maisha
Ni yapi kati ya madai haya ni kuvunja amani au kinyume cha uislamu wa BAKWATA??
Wapigania haki au wanaozidai haki wanataka;
1. Wafanyabiashara wafanye biashara zao na kufanikiwa bila kulazimika kujikomba na kuwa chawa kwa CCM. Wasilazimike kuchangia shughuli za CCM au za mwenge au kutundika picha za Samia katika biashara zao ila kupata unafuu wa kibiashara.
2. Wafanyakazi wa umma wafanye shughuli zao kwa bila mashinikizo ya CCM
3. Raia wachague viongozi wao kwa uhuru na haki, kura zihesabiwe na ziwe na maana
4. Ufisadi, Rushwa na upendeleo serikalini vikomeshwe.
5. Rasilimali za umma zisiuzwe kiholela au kutolewa kwa mikataba ya hovyo
6. Wakosoaji na wapinzani walale majumbani mwao bila hofu ya kutekwa, kupotezwa , kuuwawa au kufunguliwa kesi za mchongo.
7. Ajira nzuri na unafuu wa maisha
Ni yapi kati ya madai haya ni kuvunja amani au kinyume cha uislamu wa BAKWATA??