wadau nikiangalia mwenendo wa uongozi uliopo na vurugu zinazotokea katika club yetu naweza sema kuna unafiki mkubwa na ulafi wa madaraka unaoendelea katika club yetu ya simba
Iweje aden rage huyu huyu ambaye ameonekana ana utendaji mbovu apokelewe na watu wale wale ambao kutwa kucha wanashinda vijiweni wakimlaani kama si kiongozi bora? Au nguvu ya VIROBA IMETUMIKA?
Tukiangalia mwenendo wa timu katika mzunguko wa kwanza timu yetu ilikua ipo kati na kati iweje mashabiki hawa wafanye vurugu wakimaanisha hawa rhdhishwi na uongozi wa timu?
Rage huyu alitufanyia maigizo katika suala la uwanja wa timu kiasi mpaka leo halipo tena katika utekelezwaji
rage huyu huyu amekua na siasa nyingi mdomoni kuliko vitendo ana longolongo nyingi lakini kuna baadhi yatu hatutaki maamuzi magumu WHY?
Utashangaa hiyo tarehe moja mashabikI hawa hawa wa dar wanapiga chereko na vifijo kukubaliana na huyu MWANASIASA
KAMA MNAENDESHWA NA NGUVU ZA VIROBA NYIE WATU WA DAR TAFADHALI SIKU YA MKUTANO MKUU MSINYWE MUDA WA KUIFANYA SIMBA ITULIE NI ATOKE MTU HAPA!
ACHENI UOGA WA KITOTO
...Rage sijui ana nini ndani ya Club; sawa ataka utaratibu wa kumsimamisha haukufuata Katiba ya Club...lakini kwa jinsi hali ilivyo na mwenendo mzima wa Timu jinsi ulivyo kwasasa, inabidi ifike hatua ya kusema sasa RAGE basi; haiwezekani aendelee kugonganisha vichwa watu alafu akafumbiwa macho. Inabidi yeye binafsi atambue kuwa hapendwi tena kuendelea kuwa mwenyekiti wa Club; na kweli Rage anaitakia mema SIMBA hanabudi kuachia ngazi.
umefika wakati wa kuzia haya yanayotokea sasa