Mashabiki wa Mh. Lissu siyo watanzania

Mudawote

JF-Expert Member
Jul 10, 2013
10,071
12,610
GTs,
Umofia kwenu. Asubuhi njema kabisa ndiyo najiandaa kwenda job.
Nimefanya ka utafiti kidogo nikagundua wanaompatia kichwa cha kutukana serikali mh. Lissu hawapo Tanzania, wengi ni wabeba box huko nchi za ng’ambo. Tena ukitaka kuwafahamu vizuri hebu waambie juu ya sheria na taratibu za nchi yetu, yaani hawajui kitu.


Ukitaka pia kuhakikisha tizama jinsi ambavyo wanamuacha mwenyekiti wao wa kikundi cha upinzani Mh Mbowe akisota jela bila hata kusema lolote, na hii ni kwa sababu ni rahisi kumsemea waliyenaye ughaibuni kuliko mswahili mbowe aliye segerea.

Je hawa mashabiki wa Mh Lissu wanaijua Tanzania au wanahisia tu? Tujadili wadau
 
Mkuu umenena kweli wengi wanabeba mabox na kusafisha vibibi vizee vya kizungu huko ughaibuni na wanamsongo wa mawazo ile mbaya hivyo huja hapa JF kupunguza mihemuko yao. Ngoja ifike saa sita za EA watakuwa wengi wameamka muda huo uone mapovu ya OMO yatakapo mwagwa hapa!!
 
Kweli kabisa, wana muda maalumu. Ngoja niwa CC BAK, Mwanahabari Huru, Salary Slip, Mmawia ila huyu Mshana Jr yeye kwa sababu anajua uganga anaweza kuwa anakuja bongo kwa njia zake na kurudi kubeba box
 
Kama utafiti huo umekupa picha hiyo, basi utafiti huo pia umethibitisha kiwango cha chini kabisa cha uelewa na uchanganuzi wa mambo. Lakini sidhani hivo - mashabiki wengi wa Lissu wako humu Tanzania na ndio maana viongozi wa humu Tanzania ndio wanahangaika kukabiliana na Lissu ambaye hayuko hata Tanzania.

Na umekosea kuita jambo ulilofanya kama utafiti. Nadhani zilipaswa kuitwa hisia.
 
EBBO!! Rudi tena kwa aliekutuma,itakuwa umechanganya namna ya kufikisha hii habari.
 
Siyo utafiti huu..ni mihemko yako tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
EBBO!! Rudi tena kwa aliekutuma,itakuwa umechanganya namna ya kufikisha hii habari.
Nitajia supermarket iliyopo kamata kwa sasa. Ukiweza hilo jibu nitajua wewe siyo mbeba box. Pia nitajie Morogoro ni mkoa au wilaya?
 
Mbona Kuna watanzania wengi Sana tu wanampenda Tundu Lisu
Utafiti wako sio sahihi

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahah, acha uongo. Hakuna mtanzania anayempenda lisu mdanganyeni nyie wabeba box. Itakuwa kama Mbow alidhani akiwekwa ndani watu wata riot, ila mpaka sasa nchi ipo shwari kabiaa
 
Nitajia supermarket iliyopo kamata kwa sasa. Ukiweza hilo jibu nitajua wewe siyo mbeba box. Pia nitajie Morogoro ni mkoa au wilaya?
Sasa akutajie suoermarket iliyopo kamata kwa sasa kwani watanzania wote wanaishi Dar es salaam?
 
Reactions: Cyb
kwani bora kipi,wabeba box wanaosimama naye kwny shida au ninyi msio wabeba box ambao mlitaka kumuua???
 
Hahahah, acha uongo. Hakuna mtanzania anayempenda lisu mdanganyeni nyie wabeba box. Itakuwa kama Mbow alidhani akiwekwa ndani watu wata riot, ila mpaka sasa nchi ipo shwari kabiaa
Yaani lisu yupo kwenye wheel chair mnahaha hivi,atakaponyanyuka kabisa nahisi mtazimia kabisa
Huyu lisu anawawasha midomoni mwenu,mmelala mmeamka mnawaza Leo mumsemee nini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku zote ukishaingia mwezini inakuwa tabu tupu hapa jf.
 

Umebananishwa kolokolo! Mtabwabwaja sana mwaka huu, maana zinauma si NCHEZO!!
 
Yaani lisu yupo kwenye wheel chair mnahaha hivi,atakaponyanyuka kabisa nahisi mtazimia kabisa
Huyu lisu anawawasha midomoni mwenu,mmelala mmeamka mnawaza Leo mumsemee nini

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna anaye hahaha, nyie box people ndiyo mnahaha, mbona siye tunakula bata tu chini ya utawala wa Dr Magufuli
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…