Marekani yang'aka, Escrow ngoma bado mbichi

Marekani yang'aka, Escrow ngoma bado mbichi

Wangeendelea kuzizuia hadi rais wetu Mh.Edward Ngoyai Lowasa atakavyoapiswa rasmi kama CIC of our defences force ndo waliruhusu maana hapo hakutakuwa na ubabaishwaji kazi ni moja tu,MAAMUZI MAGUMU,NA SIO MAGUMU TU,NA NIYANAYOTEKELEZEKEKA,hakuna namna



aghhh hyu mwehu wenu hawezi kuwa rais labda rais wa WAMA,mtu mwenyewe afya mgogoro bado mnataka awe rais? we don't need walking corpse
 
wasiwape kabisa hawa jamaa, au tuwatumie sisi account zetu za Nmb na Nbc watuwekee ili nasi tuziohore!!!
 
aghhh hyu mwehu wenu hawezi kuwa rais labda rais wa WAMA,mtu mwenyewe afya mgogoro bado mnataka awe rais? we don't need walking corpse


Mtachonga sana,afya mgogoro unaijua wewe lakini sisi tunavyomgahamu namkujua Rais Lowasa yuko gado kama kisiki cha mpingo,msihangaike sana ni hapo tu kesho kutwa ndo utajutia maneno yako,lakini kwa hilo hakuna na wala hatatokea mtu atakayempinga lowasa na hii ndo salama ya CCM,no lowasa for president then UKAWA wanachukua hii nchi kwa goli la kisigino,miaka hii wananchi wamebadilika sana sio kipindi kile cha mwalimu mnawalazimishia watu kuchagua kitu kisichochagulika,kumbuka MKAPA na nguvu zote including baba wa taifa but aliambulia asilimia 61,hapo ujue watu walikuwa hawajafunguka kama sasa hivi,leo wamlete mtu wao utaona mziki wa vijana wa kitanzania kwamba shule sio tena kukremu things but ni kuelewa na kuchambua vitu/mambo
 
Kikwete anakuja Marekani by mwisho wa mwezi huu kuombeleza apewe msamaha.

Wanyamwezi hatutaki hata kumsikia.
 
Kikwete anakuja Marekani by mwisho wa mwezi huu kuombeleza apewe msamaha.

Wanyamwezi hatutaki hata kumsikia.

Na mumtenge kama mgonjwa wa U.K.O.M.A maana kwa kweli tuko na hali mbaya kwa ajili ya udhaifu wake,tume ya uchaguzi is in crises ya hela mashine za BVR zilizoshafika nchini ni 250 tu,out of 8000 machines na watu wako kimya kuna wenye hela na wanaoona million kumi ni hela za mboga na wako tu hapa Tanzania,tume huku inalalamika hakuna ndege inayaokuja huku yenye nafasi ya kubeba hizo BVR,huku kila kukicha fastjet yuko angani kila kona ya dunia,lakini ikifika kiwenye mambo ya muhimu kwa taifa utasikia hakuna hela,mimi nadhani mtu aliyetuloga alishakufa siku nyingi sana na kupata dawa ya huyo si rahisi,so tuendelee tu kuugua hadi na sisi kama nchi ife
 
Na mumtenge kama mgonjwa wa U.K.O.M.A maana kwa kweli tuko na hali mbaya kwa ajili ya udhaifu wake,tume ya uchaguzi is in crises ya hela mashine za BVR zilizoshafika nchini ni 250 tu,out of 8000 machines na watu wako kimya kuna wenye hela na wanaoona million kumi ni hela za mboga na wako tu hapa Tanzania,tume huku inalalamika hakuna ndege inayaokuja huku yenye nafasi ya kubeba hizo BVR,huku kila kukicha fastjet yuko angani kila kona ya dunia,lakini ikifika kiwenye mambo ya muhimu kwa taifa utasikia hakuna hela,mimi nadhani mtu aliyetuloga alishakufa siku nyingi sana na kupata dawa ya huyo si rahisi,so tuendelee tu kuugua hadi na sisi kama nchi ife

Hiyo mimashine kwanza haitakiwi kutumika katika uchaguzi.

Nchi zenye muamko wa haki za binadamu huwezi kusikia mtu anachukuliwa fingerprint ili kupiga kura.

Fingerprint ni kitu cha kuchukuliwa mhalifu au mtu anayefanyiwa background checks.

It is an invasion of privacy. It is a matter of undue collection of private data with a huge security implication.
 
SERIKALI ya Marekani imeendelea kuichunguza Tanzania kama inakidhi vigezo vya kupewa msaada wa Shirika la Msaada wa Maendeleo la Marekani (Millennium Challenge Corporation- MCC) unaofikia Dola za Marekani milioni 700, sawa na Sh trilioni 1.3.


Tathmini hiyo imeendelea kufanyika wakati nchi ya Ghana ikiwa tayari imeshapata msaada wake, huku Tanzania ikikabiliwa na harufu ya ufisadi unaokwamisha kupitishwa kwa msaada huo.


Taarifa hizi mpya zimepatikana baada ya kikao kilichofanyika Washington DC Februari 27, mwaka huu, kati ya Makamu wa Rais wa MCC, Kamran Khan na Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Liberata Mulamula, ambapo pamoja na masuala mengine, imeamriwa kuwa Bodi ya MCC itakutana kwa mara ya mwisho Septemba, ili kuamua kama Tanzania ipewe msaada au isipewe.


“Kikao cha bodi cha mwezi Machi hakiwezi kuwa cha kufanya uamuzi wa kuipatia Tanzania msaada mpaka kile cha mwezi Septemba 2015, ambacho kitafanya tathmini,” linaeleza andishi lililotunza kumbukumbu ya kikao kati ya Khan na Liberata.


Khan alisema kuwa kikao hicho kilikuwa ni muhimu ili kufanya tathmini sahihi ya yale ambayo walikubaliana na Tanzania, hasa katika masuala yanayohusu ufisadi kabla ya kikao cha bodi cha Machi, mwaka huu.


Ni katika mwenendo huo huo wa kuifuatilia Tanzania, hivi karibuni Makamu wa Rais wa MCC, Kamran Khan na Makamu Rais wa Sera na Tathmini, Beth Tritter, walifanya ziara nchini kwa lengo la kutathmini kama Tanzania imekidhi vigezo vya kupewa awamu ya pili ya msaada wa MCC.


Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo ambayo MTANZANIA Jumamosi imeiona, Khan na Tritter waliwasili nchini Machi 1. Khan na Tritter ambao kesho yake baada ya kuwasili (Machi 2) walikutana na Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress na msaidizi wake, Virginia Blaser, kabla ya kupata taarifa ya mradi wa ‘Power Team Africa’, inaelezwa baada ya kupata maelezo kuhusiana na uchunguzi unaoendelea kuhusiana na kashfa za ufisadi, ikiwemo suala la uchotwaji fedha katika akaunti ya Escrow, bado wameonekana kutoridhishwa na hatua ambazo serikali imezichukua.


Imebainika kuwa katika ziara hiyo ambayo pia ilikuwa na lengo la kupata picha juu ya kile ambacho kitafanyika kuhusiana na mchakato wa maoni ya Katiba mpya pamoja na Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu, viongozi hao walikutana na mjumbe wa MCC na Balozi Childress.


Pia walikutana na Waziri wa Fedha, Saada Mkuya, Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, Mkurugenzi wa Tanesco, Felichesmi Mramba, Mkurugenzi Mtendaji wa Ewura, Felix Ngamlagosi, Mratibu wa Taifa wa Akaunti ya Maendeleo ya Milenia (MCA) na wengineo.


Siku hiyo pia Khan na Tritter walitembelea makao makuu ya MCA katika jengo la Shirika la Maendeleo (NDC), kabla ya kukutana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Richard Ndassa, kwa lengo la kusikia vipaumbele vya kamati hiyo, hasa katika gesi asilia. Baadaye walimaliza ratiba ya siku kwa kufanya mkutano na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, Ikulu.


Ratiba yao inaonyesha kuwa Machi 3 walikutana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe, ili kupata taarifa za sakata la IPTL na Akaunti ya Escrow kwa ujumla na baadaye walipata chakula cha mchana na wawakilishi wa Benki ya Dunia (WB), Shirika la Maendeleo ya Sweden (Sida), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB) na wawakilishi wa Norway ili kusikia mikakati yao katika sekta ya nishati.


MCC inafadhili miradi mbalimbali, ikiwemo ya maji, barabara na nishati.
Waziri wa Fedha, Saada Mkuya, alipoulizwa na gazeti hili alikiri kukutana na Khan na Tritter kwa lengo la kutathimi vigezo vya Tanzania kupata msaada wa awamu ya pili wa MCC ambazo ni kiasi cha Dola za Marekani 700 milioni (Sh 1.3 trilioni).


“Ni kweli Khan alikuja na tumezungumza na mapendekezo yetu ameyapeleka kwenye Bodi ya MCC,” alisema Mkuya.
Alipoulizwa kama MCC wameridhishwa na hatua za Serikali katika utawala bora na hasa kashfa ya Escrow, Mkuya alisema:
“Hayo sasa ni yako, ila mimi najua wameridhishwa na hatua za Serikali hata katika hilo suala la Escrow. Hizi ni hatua za kawaida tu katika kupata huo msaada. Tunategemea utakuwa tayari ifikapo Septemba,” alisema Mkuya.


Kwa upande wake, Mbunge wa Sumve ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Richard Ndassa, alikiri kukutana na Khan.


“Nani kakupa hizo taarifa?” alihoji Ndassa, akionyesha kushtuka, kisha akaendelea: “Niambie chanzo chako ili nikusaidie… La msingi walitaka kujua maendeleo ya awamu ya kwanza msaada wa MCC kwa kuwa tunakwenda kwenye awamu ya pili (MCC Compact 2) hasa kwa upande wa umeme,” alisema Ndassa na kuongeza:
“Walituuliza wabunge kama tumeridhishwa na msaada wa MCC na jinsi Serikali inavyochukua hatua. Tumesema tumeridhika kwa kuwa Bunge limechukua hatua… si unajua yalitolewa mapendekezo? Utawala nao umechukua hatua ya kuwasimamisha mawaziri na watendaji wa Serikali na Mahakama nayo inafanya kazi; kwa sasa unaona Baraza la Maadili linaendelea kuwahoji wahusika.”
Escrow bado mbichi


Kwa upande mwingine, Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, alisema bado Tanzania haijakidhi vigezo vya kupewa msaada wa MCC.
Katika ujumbe wake mfupi wa simu, Kafulila, aliyeibua sakata la Escrow bungeni mwaka jana, alisema kipengele kilichoguswa katika sakata hilo kinahusu watu waliopewa fedha na Mkurugenzi wa Kampuni ya VIP Engineering, James Rugemarila.


“Tanzania bado haijakidhi vigezo vya MCC, Ghana wenzetu wameshaanza kupata fedha hizo. Kikubwa kichozuia bodi ya MCC kuamua ni namna ambavyo Serikali inavuta miguu kuchukua hatua kuhusu ufisadi wa Escrow,” alisema Kafulila na kuongeza:
“Mpaka sasa hatua zilizochukuliwa ni kwa watu waliohusishwa na Rugemarila (James) ambaye alifaidi asilimia 30 tu. Bado waliofaidi kupitia Harbinder Singh Sethi (Mwenyekiti Mtendaji wa Pan African Power Solutions Tanzania Limited (PAP) aliyepata asilimia 70 ya fedha zote.”
Kafulila alisema nchi za Ulaya zinajua kwa kina suala hilo kuliko Watanzania.


“Bila shaka majasusi wa Ulaya na Marekani wanajua hata kilichomo ndani ya ripoti ya PCCB (Taasisi ya Kupambana na Kudhibiti Rushwa,” alisema na kuongeza:
“Hili huenda likaigharimu nchi nchi kwa miaka mingi kama ufisadi wa Goldenberg ulivyovunja uhusiano wa Kenya na nchi za Magharibi.”
Desemba 2014, Bodi ya Wakurugenzi ya MCC ilionyesha wasiwasi wao kuhusu kukithiri kwa rushwa nchini, hasa kesi ya hivi karibuni ya IPTL.
“Kwa miaka saba iliyopita, Bodi imegundua Tanzania imeshindwa kudhibiti rushwa (rushwa inaongezeka) kwa mujibu wa vipimo vya jitihada ya kupambana na Rushwa,” ilisema taarifa ya bodi hiyo na kuongeza:
“Wakati Bodi imekubali kuiruhusu Tanzania iendelee kuandaa mapendekezo yake, ila ni muhimu Serikali ya Tanzania ionyeshe kuchukua hatua suala la rushwa kabla ya fedha kutolewa.”


Mkurugenzi wa Takukuru, Dk. Edward Hosea, hakuwa tayari kuzungumzia ripoti ya taasisi yake, hasa kwa asilimia 70 za mwamala ulioihusisha kampuni ya PAP.


“Siwezi kuzungumzia suala hilo… niko msibani, siwezi kuzungumzia masuala ya kazi,” alisema Dk. Hosea na kukata simu yake.
Mbali na Marekani, hivi karibuni nchi wahisani wanaofadhili bajeti walisema hawajaridhishwa na hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kashfa ya akaunti ya Escrow.


Nchi hizo zilitoa Sh 25.8 bilioni kati ya Sh 959 bilioni wanazopaswa kutoa kwa kile walichosema bado hawajaridhishwa na hatua za Serikali katika utawala bora.


Hatua za Serikali
Sakata la akaunti ya Escrow liliibuliwa bungeni mwaka jana na baada ya kujadiliwa kwa urefu, Bunge lilitoa mapendekezo ya kuwawajibisha mawaziri na watendaji wa Serikali.


Waliowajibika ni pamoja na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema, huku Rais Jakaya Kikwete akimfuta kazi aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na baadaye aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, aliyekuwa amemweka kiporo.


Kwa upande mwingine, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, alisimamishwa kazi kupisha uchunguzi.
Kwa upande wa Mahakama, baadhi ya watendaji wa Serikali wamefikishwa mahakamani, akiwemo Mkurugenzi wa Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Julius Angelo, Ofisa Mwandamizi wa TANESCO, Steve Urassa na Leonard Lutabingwa wa TRA.


Mbali na mahakamani, Baraza la Maadili ya Watumishi wa Umma chini ya Mwenyekiti wake, Jaji Hamisi Msumi, limewahoji watumishi wa Serikali waliopokea fedha kutoka kampuni ya VIP Engineering. Waliohojiwa ni pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Philip Saliboko na Mnikulu, Shaaban Gurumo.


Baadhi ya wabunge walihusishwa na kashfa hiyo, akiwemo Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, aliyekata rufaa Mahakama Kuu akipinga kuhojiwa.


Wengine ni Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja.
Hivi karibuni CCM imetangaza kuwatema wabunge hao kushiriki kwenye vikao vya maamuzi, yaani Halmashauri Kuu na Kamati Kuu.


Chanzo:Mtanzania

Kwa hali hii tunalo
 
10/2015 tusifanye makosa.
Sisi ni nchi kubwa ambayo ilitakiwa iwe juu ya nchi nyingi Afrika ila sababu ya ubinafsi wa watu fulani tuko hapa tukisumbuana na misaada
 
Njia ya Muongo huwa ni fupi sana; Ndassa, Mkuya au awe awaye; ngoma mbichi hii; Wafadhili hawadanganyiki!
 
Kale kamama kawaziri kafedha, kalisimama bungeni na kusema waziwazi mkataba wa MCC phase 2 tumeshasign, ni utekelezaji tu unasubiriwa. Yaani yule mama ni bogus kwelikweliii...!

Hata mimi kananiudhi na sijui jk alikateua kwa vigezo gani
 
Kwa upande wake, Mbunge wa Sumve ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Richard Ndassa, alikiri kukutana na Khan.



Chanzo:Mtanzania

Huyu Ndassa alikua anaongea nao kwa lugha gani? maana jamaa ni Standard 7 wakutupwa..unless alikua anatumia mkalimani
 
Wapi saada salum mkuyati

Hivi kwani yumo huku mkuu?! ama anachunguliaga mara moja moja kupitia dirishani na kukimbia??!!! akili za wana JF hazitamruhusu kukaa humu kamwe atakufa kwa BP
 
Lakini akitoa speech huwa anaongea vizuri sana.Vipi huko Azam tv wenye studio za kisasa wanaweza mchukuwa kwa kusoma habari za kitaifa na kimataifa??
 
Halafu yule Mkwere bin DHAIFU anatamka eti "Najivunia rekodi yangu" sijui ni rekodi ipi anayojivunia wakati kila sekta ni shakalabaghala.
 
Wangeendelea kuzizuia hadi rais wetu Mh.Edward Ngoyai Lowasa atakavyoapiswa rasmi kama CIC of our defences force ndo waliruhusu maana hapo hakutakuwa na ubabaishwaji kazi ni moja tu,MAAMUZI MAGUMU,NA SIO MAGUMU TU,NA NIYANAYOTEKELEZEKEKA,hakuna namna
Jiandae kisaikolojia Lowassa hawezi kuwa rais wa nchi hii.
r
 
BY SHEILA MBAGA.................Sheila Mbaga is offline
Sheila Mbaga

Join Date : 27th February 2015

Default Re: Taarifa sahihi kuhusu ulinzi wa Dk. WillibrodSlaa dhidi ya upotoshwaji unaoenezwa

[h=1]Ukweli wa Mauaaji haya hapa: Membe, Gotham na Ridhiwani wahusishwa [/h]
Ni kwa kipindi chamuda mrefu kumekuwepo na kikundi kinachoratibu mauaji ya watu mbali mbali. hayatunayoyasikia kwa Dr. Slaa siyo mageni masikioni mwetu bali ni muendelezo wakile kinachoratibiwa na kundi hilo. Ni wazi kuna mipango yaliyoanza kutekelezwakwa baadhi ya wana CCM na baadhi wa wapinzani, leo hii naomba niwatelee ukweliwa haya mauaji yote na mipango ya kuuwa watu wengine....

1. Mjumbe wa NecLudewa: Huyu ndiyo alikuwa mhanga wa kwanza katika mauaji ya hivi karibuni,mjumbe huyu wa halmashauri kuu ya Taifa ya CCM, aliwekewa sumu katika kikao chaNEC kilichofanyika mwezi wa 11 mwaka jana katika mji wa Dodoma, bila kupepesamacho uratibu wa kumwekea sumu uliratibiwa na bwana moja anayejulikana kwa jinala Jack Gotham, ambaye ni kada wa Chama cha Mapinduzi.

2. Mjumbe wa Nec waCCM kutoka Kahama: Huyu ni mjumbe wa NEC wa chama cha mapinduzi kutoka wilayaya Kahama, ambaye ni mdogo wake waziri Marry Nagu, naye ni muanga wa kuwekewasumu, ambapo aliwekewa sumu katika kikao hicho hicho kilichoketi Dodomamwishoni mwa mwaka jana.

3. BeatriceShelukindo: Huyu ni mbunge wa Kilindi kupitia chama cha mapinduzi, na ni mjumbea halmashauri kuu ya Taifa kupitia wilaya ya kilindi, ni kwa muda mrefu sanaMama Beatrice amekuwa akiugua na kutibiwa India. Beatrice aliwekewa sumubungeni na wahusika hawahawa ambao nitawataja hapa chini. kama unakumbukaBeatrice Shelukindo alikuwa moja wa wabunge waliokuwa wakali sana kuhusu swalala Richmond ila baadaye alipogundua ukweli akaamua kuwakimbia na kusimama katikaukweli. Ni jambo la kumshukuru Mungu ya kwamba kwa sasa Beatrice yuko nchini naanaendelea vizuri baada ya juhudi kubwa za madaktari wa India kuweza kuondoasumu aliyowekewa.

4. Kapteni Komba:Komba amekuwa mbunge wa Mbinga Magharibi na mjumbe wa NEC kupitia Nyasa, baadaya mazishi yake yaliyofanyika wiki iliyopita sasa ni wazi kilichomuuwakimejulikana. Komba aliwekewa sumu na hao hao wahusika sababu kubwa sikiwambili, mosi ni ahadi aliyopewa Stella Manyanya kuhusu jimbo husika na pili niwazi Komba alikuwa instrumental katika siasa za Edward Lowassa ambaye anawatoaroho huko CCM katika kinyanganyiro chao cha uchaguzi wa ndani. Ni Komba sikuchache kabla ya kuwekewa sumu alisema wazi wazi kwamba anamuunga mkono Lowassakuwa mgombea wa chama cha mapinduzi.

5. Salum Awadh: Huyualikuwa ni mjumbe wa kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi, kifo chakehakikupishana na cha Komba, pamoja na sifa zote ila alikuwa na sifa moja kubwaambayo ni ujasiri, Ni Awadh aliyediriki kusema mbele ya Mkt Jakaya kwamba kamani kosa la maadili basi wagombea wote ndani ya CCM wana kosa hilo la maadili nasiyo wachache kama tunavyoaminishwa, pili ni Awadh aliyetoa hoja binasfi ndaniya kamati kuu kwamba Nape Nyauye ambaye ni mwenezi wa chama afukuzwe ndani yachama na anyanganywe kadi yake mara moja kwa sababu alishakisaliti CCM na kuwamoja wa waanzilishi wa CCJ, vile vile Awadh aliongezea hoja yake kwamba kwasasa Nape yupo kwa ajili ya kukibomoa chama badala ya kukijenga...

Bwana Awadh aliwekewasumu na ndugu Issa Gavu katika ofisi ya Kisiwandui, siku mbili kabla; nduguGavu alifanya kikao cha pamoja katika hoteli ya Serena akiwa na RidhiwaniKikwete na Jack Gotham ambaye ni consultant kwenye mradi wa vitambulisho vyaTaifa {NIDA), na ndiyo meneja kampeni wa Bernard Kamilius Membe..

Gotham mnano tarehe22.04. 2014 alienda Nchini Bulgaria kupata mafunzo ya kuuwa watu kwa njia yasumu na kisha akarudu na sumu aina ya CYNIDE ikiwa ni sumu mahsusi kwa ajili yakumaliza wale wote wanaoona ni kizingiti kwao katika kukamata dola. hii sumu nikwa ajili ya kuwamaliza wale waliovizingiti kwao ndani ya chama chao na nje yachama chao, ndiyo mana leo hii kusikia kuhusu Dr. Slaa kutaka kuuwawa ni swalaambalo ni serious na la ukweli. Katika hili la Dr. Slaa msimamizi mkubwa niMangula ambaye ni makamu mwenyekiti wa chama hicho (kama mlivoona kwenye vyombovya habari vya leo), na ni Membe aliyeenda kusini kumfata Mangula....

Mkakati huu unarudinyuma alivyouwawa kijana moja wa Kinyakyusa kisha wakasema ni ajali ya gari(stori hii ilikuwa reported kwenye vyombo mbali mbali vya habari). Kijana huyualiuwawa baada ya kutoa siri za Home Shopping Centre na Ridhiwani kutoa watuSouth Africa kwa ajili ya kumuuwa Bwana Masamaki ambaye ni kamishna wa Tax TRA.

Huu mchezo wa kuuwawatu haujaanza leo, hawa mabwana walianzisha utaratibu wa kutoa watu SouthAfrica na Kenya kwa kazi hiyo tu. wamefanya hivyo kwa Ulimboka Steven ambapowatu walitolewa Kenya na kushirikiana na Ramadhani Ighodu, wakafanya hivyo kwaAbsolom Kibanda (kama unakumbuka kati ya maadui 11 aliyowataja Membe, KIbandaalikuwa moja wao kama mwandishi)...

Mwaka 2012 RidhiwaniKikwete alichukuwa watu kutoka Kenya kwa ajili ya kufanya kazi maalumna mpakasasa watu hao bado wapo nchini ambapo wamepangishiwa nyumba mitaa ya Masakieneo maarufu kama Kilimanyege karibu na Jacks Bar.... Mauaji haya yamekiwayakisimamiwa na Membe na kuratibiwa na Ridhiwani pamoja na Gotham...

Nina uhakika kwambahaya yanafanyika bila Rais Jakaya kujua, hata hapa idara yetu hakuna wanaojuahili swala zaidi ya watu wa karibu wa Membe. Ridhiwani amekuwa akifanya hayayote na hao washirika wake hata bila baba yake kujua na hii ni kwa sababu dogokashaingizwa kwenye biashara haramu mbalimbali likiwemo na la kuuza madawa yakulevya. Kwa sasa ni wazi hawa watu wanafanya jitiada zozote zile waingiemadarakani ili kulinda dhambi zao, na wanafanya kila jambo ili washindeuchaguzi wa mwaka huu, kwa hali hiyo tutegemee mauaji mengi na makubwa kutokeakuanzia sasa.. Na kwa sasa bila kuwaficha ila nafanya haya kwa neema za Mungukuna mpango wa kuangusha helcopter ya Chadema... hawa watu wamekuwa wakipangakufanya haya mambo na kujadili hali ya siasa katika hoteli zifuatazo 1). Serena2). Protea na 3). Collesium Oysterbay...

Ila kwa wale mabibiwa umri kama wangu watakumbuka kifo cha kutatanisha cha Padre Serapius Kombaambapo Membe wakati huo alihusishwa. Komba aliuugua ugonjwa wa kufa ubongo polepole. Komba alikuwa Gombare wa seminari kuu Peramiho, mwandishi mahiri na mtualiyejaliwa upendo ila kwa unyama wa Membe na ushirika wake na Padre SebastianNepachichi walidiriki kukatisha uhai wa padre Komba... Hata hivyo kifo chabalozi wa Libya aliyeuwawa yasemekana kuna mkono mkubwa wa MEMBE..... Membe nimtu hatari sana na kama Taifa tusikubali kurudi kwenye zama za mauaji yakikatili....

Asanteni
Mtoto Sheila.....

like

Pasco, ocampo four and jme like this.
 
Back
Top Bottom