Marekani wanakwama wapi?

MKEHA

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
714
1,137
Wakati wa maandamano ya nchi za Kiarabu Marekani walichekelea sana kwa kuzitukana nchi za kiarabu kwamba hazina demokrasia. Yakaja tena maandamano ya Iran Marekani walafurahi sana kwa kuona Iran inavyopata shida kuzima yale maendeleo.

Sasa ni zamu ya Marekani, leo ni siku ya nane mfululizo watu wako barabarani, hawasiki cha mwazini, sheria za Curfew zimewekwa kwenye miji mingi lakini watu hawaelewi. George Floyd kifo chake kimechochea moto ambao unaonekana kuzimika utaidharimu pakubwa sana Marekani.

Majumba ya serikali na maduka makubwa yamechomwa moto, magari na vituo vya polisi vimechomwa moto, Ikulu ya White House kama imetekwa vile kiasi kwamba rais Trump alifichwa kwenye chumba cha shimoni baada ya kuona hali ya usalama ni tete.

Ufaransa nako jana moto umewaka kwa kumbikumbu ya kifo cha Adama Traore aliyefariki miaka minne iliyopita.
Kila nchi sasa inaunga mkono maandamano ya Wamarekani.

Hii inaweza kuwa ni African American Spring. Je Trump atakuwa na uhakika wa kurudi kwenye kiti baada ya uchaguzi mwaka huu. Kumbe hata Marekani kuna shida nyingi sana za kijamii japo hawazisemi na kuzitangaza.

Ama kweli muoshwa huoshwa.
 
Dhambi ya ubaguzi haijamuacha mtu Salama, CORONA + MAANDAMANO vimeigharimu sana Marekani

Sent from my JSN-L21 using JamiiForums mobile app
Wakati US anaandamwa na KORONYA na MAANDAMANO ambayo yanaonekana kabisa sio yakawaida UCHINA kule wanaendelea naharakati zao kama kawaida

Mshana Jr nakumbuka aliwahi kuleta uzi wenye kichwa cha habari Marekani haitamalaki kwenye Utukufu alimaanisha
 
Wakati US anaandamwa na KORONYA na MAANDAMANO ambayo yanaonekana kabisa sio yakawaida UCHINA kule wanaendelea naharakati zao kama kawaida

Mshana Jr nakumbuka aliwahi kuleta uzi wenye kichwa cha habari Marekani haitamalaki kwenye Utukufu alimaanisha
Laana inawatafuna, wanapofanya machafuko kwenye nchi za watu Mungu anawatia adabu apa duniani kwanza
 
Ni njaa tu.. Lockdown imewapiga sana. Mamilioni wamepoteza ajira.
 
... Marekani ni taifa la kidemokrasi sana. Ingekuwa China au kule kwingine saa hizi ambulance zingekuwa busy kuzoa maiti za wananchi waliouliwa kwa risasi za polisi na jeshi mitaani kwa amri ya serikali. Texas na state gani huko polisi wamewapigia wanachi magoti kuomba samahani; umewahi kuiona wapi hiyo?
 
Wameona kitaendelea kunuka, wazungu hawapendi nchi yao ichafuke ila wanapenda nchi za watu zichafuke, hao askari wanaopiga magoti ni wanafiq tu sio kwamba wanafanya ivyo eti kwa heshima
... Marekani ni taifa la kidemokrasi sana. Ingekuwa China au kule kwingine saa hizi ambulance zingekuwa busy kuzoa maiti za wananchi waliouliwa kwa risasi za polisi na jeshi mitaani kwa amri ya serikali. Texas na state gani huko polisi wamewapigia wanachi magoti kuomba samahani; umewahi kuiona wapi hiyo?
 
Wameona kitaendelea kunuka, wazungu nchi yao ichafuke ila wanapenda nchi za watu zichafuke, hao askari wanaopiga magoti ni wanafiq tu sio kwamba wanafanya ivyo eti kwa heshima

Sent from my JSN-L21 using JamiiForums mobile app
... wewe endelea kuhisi ni unafiki Mkuu; ila kwa unyenyekevu mkubwa wameomba samahani kwa "the people". China au Iran hayo yapo? Tulia ujifunze maana halisi ya demokrasia kwa vitendo kutoka kwa baba wa demokrasia - taifa la Marekani.
 
... Marekani ni taifa la kidemokrasi sana. Ingekuwa China au kule kwingine saa hizi ambulance zingekuwa busy kuzoa maiti za wananchi waliouliwa kwa risasi za polisi na jeshi mitaani kwa amri ya serikali. Texas na state gani huko polisi wamewapigia wanachi magoti kuomba samahani; umewahi kuiona wapi hiyo?
Mbona HONGKONG hatukuona Hizo gari zakubebea wagonjwa zikibeba wagonjwa ?!

Ila kwa upuuzi wa trump mnayotaka kuyaona wala usijali mtayaona tu soon

Hayo magoti yao si unafiq tu nandio maana watu bado wamekamatia pale pale hawataki kupaachia.....
 
... wewe endelea kuhisi ni unafiki Mkuu; ila kwa unyenyekevu mkubwa wameomba samahani kwa "the people". China au Iran hayo yapo? Tulia ujifunze maana halisi ya demokrasia kwa vitendo kutoka kwa baba wa demokrasia - taifa la Marekani.
Utaiona demokrasia soon ww ngojea tu
 
... wewe endelea kuhisi ni unafiki Mkuu; ila kwa unyenyekevu mkubwa wameomba samahani kwa "the people". China au Iran hayo yapo? Tulia ujifunze maana halisi ya demokrasia kwa vitendo kutoka kwa baba wa demokrasia - taifa la Marekani.
Baba wa democrasia huyu alieuwa na kutia ulemavu mamilioni ya watu Japan, Iraq, Afghanistan
20200601_144924.jpg
20200601_144912.jpg
20200601_145715.jpg
fm_facts-20200531-0001.jpg


Sent from my JSN-L21 using JamiiForums mobile app
 
... Marekani ni taifa la kidemokrasi sana. Ingekuwa China au kule kwingine saa hizi ambulance zingekuwa busy kuzoa maiti za wananchi waliouliwa kwa risasi za polisi na jeshi mitaani kwa amri ya serikali. Texas na state gani huko polisi wamewapigia wanachi magoti kuomba samahani; umewahi kuiona wapi hiyo?
Demokrasia ipi hiyo Askari wanauliwa na masinipa?,,hakunaga Cha demokrasia,,wanajua wakitumia nguvu kubwa na watu wafe wanarisk uwepo wa civil wars,wamarekani kibao Wana silaha na Ni haki yao kijkatiba kuwa na silaha
 
... Marekani ni taifa la kidemokrasi sana. Ingekuwa China au kule kwingine saa hizi ambulance zingekuwa busy kuzoa maiti za wananchi waliouliwa kwa risasi za polisi na jeshi mitaani kwa amri ya serikali. Texas na state gani huko polisi wamewapigia wanachi magoti kuomba samahani; umewahi kuiona wapi hiyo?
Unasifia demokrasia kwenye hayo maandamano hali ya kuwa hayo maandamano yanatokana na vifo vya watu weusi kuuliwa na polisi na haki haitendeki.
 
Back
Top Bottom