Mi mi
JF-Expert Member
- Jul 14, 2024
- 5,752
- 10,523
Ikulu ya White House imetoa taarifa ikisema kuwa Marekani imetangaza makubaliano ya kibiashara na China baada ya mazungumzo kati ya ujumbe wa Marekani na China kufanyika nchini Uswisi siku ya Jumapili.
Hata hivyo, haijawa wazi mara moja kama makubaliano hayo yamefikiwa rasmi.
Waziri wa Fedha, Scott Bessent, alisema wamepiga hatua kubwa katika mazungumzo hayo na taarifa kamili itatolewa kesho. Aliongeza kuwa mazungumzo yalikuwa ya mafanikio na kwamba Rais Trump amepewa taarifa kamili.
Mwakilishi wa Biashara wa Marekani, Jamieson Greer, alisema mazungumzo ya siku mbili yalikuwa ya kujenga na walikubaliana kwa haraka, jambo linaloashiria kuwa tofauti kati yao hazikuwa kubwa kama ilivyodhaniwa.
Baada ya kutangaza hali ya dharura ya kitaifa, Rais Trump alipandisha ushuru wa bidhaa kutoka China hadi 145%. Greer alihitimisha kwa kusema wana imani kuwa makubaliano hayo yatachangia kutatua hali hiyo ya dharura.
Hata hivyo, haijawa wazi mara moja kama makubaliano hayo yamefikiwa rasmi.
Waziri wa Fedha, Scott Bessent, alisema wamepiga hatua kubwa katika mazungumzo hayo na taarifa kamili itatolewa kesho. Aliongeza kuwa mazungumzo yalikuwa ya mafanikio na kwamba Rais Trump amepewa taarifa kamili.
Mwakilishi wa Biashara wa Marekani, Jamieson Greer, alisema mazungumzo ya siku mbili yalikuwa ya kujenga na walikubaliana kwa haraka, jambo linaloashiria kuwa tofauti kati yao hazikuwa kubwa kama ilivyodhaniwa.
Baada ya kutangaza hali ya dharura ya kitaifa, Rais Trump alipandisha ushuru wa bidhaa kutoka China hadi 145%. Greer alihitimisha kwa kusema wana imani kuwa makubaliano hayo yatachangia kutatua hali hiyo ya dharura.