kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,247
- 16,169
Nahisi kama vile ni mzee sana kumudu kukimbizana na vijana, au macho yangu yananidanganya?.
===
Miaka kadhaa tangu aondoke kwenye ramani ya soka la Tanzania, kocha raia wa Brazil, Marcio Maximo ameibuka upya baada ya kutambulishwa rasmi kuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya KMC inayomilikiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.
Maximo amechukua mikoba ya Kally Ongala ambaye aliondolewa kwenye klabu hiyo kutokana na mwenendo mbovu wa kikosi hicho mwanzoni mwa mwezi Mei mwaka huu.
Maximo anakumbukwa zaidi kwa kipindi chake akiwa Kocha Mkuu wa timu ya taifa, Taifa Stars ambaye aliiwezesha timu hiyo kufuzu Michuano ya CHAN kwa mara ya kwanza mwaka 2009.
===
Miaka kadhaa tangu aondoke kwenye ramani ya soka la Tanzania, kocha raia wa Brazil, Marcio Maximo ameibuka upya baada ya kutambulishwa rasmi kuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya KMC inayomilikiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.
Maximo amechukua mikoba ya Kally Ongala ambaye aliondolewa kwenye klabu hiyo kutokana na mwenendo mbovu wa kikosi hicho mwanzoni mwa mwezi Mei mwaka huu.
Maximo anakumbukwa zaidi kwa kipindi chake akiwa Kocha Mkuu wa timu ya taifa, Taifa Stars ambaye aliiwezesha timu hiyo kufuzu Michuano ya CHAN kwa mara ya kwanza mwaka 2009.