Maprofesa waliotekwa na Taliban waoneshwa kwenye video

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397


Timothy Weekes alitoa wito kwa Bw Trump kumsaidia

Wapiganaji wa Taliban wametoa kanda ya video inayowaonesha mateka wawili - Mmarekani na raia wa Australia - ambao walitekwa na wanamgambo hao nchini Afghanistan mwaka jana.

Mmarekani Kevin King na raia wa Australia Timothy Weekes walikuwa maprofesa katika chuo kikuu cha Wamarekani cha Afghanistan mjini Kabul.

Walitekwa mwezi Agosti wakiwa kwenye magari yao nje ya chuo hicho na wapiganaji waliokuwa wamevalia sare za wanajeshi wa serikali.

Baadaye mwezi huo, wanajeshi wa Marekani nchini Afghanistan walijaribu kuwakomboa lakini wakashindwa, Pentagon ilisema.

Kwenye video hiyo ambayo inadaiwa kupigwa mnamo 1 Januari na kupakiwa mtandaoni, wanaume hao wanasema wamo buheri wa afya.

Lakini wanamuomba Rais mteule wa Marekani Donald Trump kujitolea kuwabadilisha na wafungwa wa Taliban ndipo waachiliwe huru.

Wanasema watauawa iwapo Marekani haitashiriki kwenye mazungumzo ya kuwaachilia huru.

Chanzo: BBC
 


Timothy Weekes alitoa wito kwa Bw Trump kumsaidia

Wapiganaji wa Taliban wametoa kanda ya video inayowaonesha mateka wawili - Mmarekani na raia wa Australia - ambao walitekwa na wanamgambo hao nchini Afghanistan mwaka jana.

Mmarekani Kevin King na raia wa Australia Timothy Weekes walikuwa maprofesa katika chuo kikuu cha Wamarekani cha Afghanistan mjini Kabul.

Walitekwa mwezi Agosti wakiwa kwenye magari yao nje ya chuo hicho na wapiganaji waliokuwa wamevalia sare za wanajeshi wa serikali.

Baadaye mwezi huo, wanajeshi wa Marekani nchini Afghanistan walijaribu kuwakomboa lakini wakashindwa, Pentagon ilisema.

Kwenye video hiyo ambayo inadaiwa kupigwa mnamo 1 Januari na kupakiwa mtandaoni, wanaume hao wanasema wamo buheri wa afya.

Lakini wanamuomba Rais mteule wa Marekani Donald Trump kujitolea kuwabadilisha na wafungwa wa Taliban ndipo waachiliwe huru.

Wanasema watauawa iwapo Marekani haitashiriki kwenye mazungumzo ya kuwaachilia huru.

Chanzo: BBC

Ni kweli kabisa, mtu huwezi kufanya kazi katika maeneo yenye risk ya usalama namna hiyo alafu yakikuta ya kukukuta unaanza kuomba msaada na kuurumisha urumisha. Hawakunufaika na elimu waliyonayo kuweza kutambua jambo hilo.
 
Utakuwa mtu wa ajabu, kutoka nje ya jamii hizo, kwenda kufanya kazi za kawaida maeneo ya Taliban, Boko Haram, ISIS, Al-Shabaab, et. al. kwa kisingizo chochote kile. Huko waachiwe wenyewe wanaopenda kuchinjana wenyewe kwa wenyewe kama minyama pori isiyo na akili.
 
Utakuwa mtu wa ajabu, kutoka nje ya jamii hizo, kwenda kufanya kazi za kawaida maeneo ya Taliban, Boko Haram, ISIS, Al-Shabaab, et. al. kwa kisingizo chochote kile. Huko waachiwe wenyewe wanaopenda kuchinjana wenyewe kwa wenyewe kama minyama pori isiyo na akili.
Bila ya shaka walikua majasusi.ukienda kwa amani kwa hawa jamaa mbona hawana shida
Ni marekani ndio wenye matatizo.hivi kweli chuo kikuu cha marekani ndani ya aAfghanistan?
 
Bila ya shaka walikua majasusi.ukienda kwa amani kwa hawa jamaa mbona hawana shida
Ni marekani ndio wenye matatizo.hivi kweli chuo kikuu cha marekani ndani ya aAfghanistan?
Hawa jamaa sidhani kama neno AMANI limo kwenye misamiati yao unless kwao neno amani linatafsiriwa vingine. Hawa jamaa wana utaratibu wao; unatakiwa kukariri (cite) mistari kadhaa ya maandishi yao ukishindwa ni kifo. Hapo kuna amani kweli? Ndio maana nasema kwao amani lina maana wanayoijua wao na sio unavyotaka kutuaminisha hapa.
 
Hawa jamaa sidhani kama neno AMANI limo kwenye misamiati yao unless kwao neno amani linatafsiriwa vingine. Hawa jamaa wana utaratibu wao; unatakiwa kukariri (cite) mistari kadhaa ya maandishi yao ukishindwa ni kifo. Hapo kuna amani kweli? Ndio maana nasema kwao amani lina maana wanayoijua wao na sio unavyotaka kutuaminisha hapa.
Hawa jamaa sidhani kama neno AMANI limo kwenye misamiati yao unless kwao neno amani linatafsiriwa vingine. Hawa jamaa wana utaratibu wao; unatakiwa kukariri (cite) mistari kadhaa ya maandishi yao ukishindwa ni kifo. Hapo kuna amani kweli? Ndio maana nasema kwao amani lina maana wanayoijua wao na sio unavyotaka kutuaminisha hapa.
Hakuna anaetaka kukuaminisha chochote ni chuki yako tu na jamii flani ndio inakuskuma kutoka povu.nimesema hivi bila shaka hawa ni majasusi iweje chuo kikuu cha marekani ndani ya kabul Afghanistan? Ardhi Imeisha marekani?Acha chuki tafakari amani ipo kila mahali lakini ukiitaka
 
Hapo naona jina la S.W a.k.a Allah, a.k.a Mohammed linatumika na linaelekea kutumika kuwachinja hawa innocent civilians, inasikitisha sana. Ni bora wangejiita hata M23 tu ijulikane kuliko kujiweka nyuma ya muamvuli wa dini ya kiislamu na kuharibu jina la dini nzuri kabisa yenye kueneza amani, na unakuta baadhi ya waislam wanachekelea na kusema mashallah
 
Hapo naona jina la S.W a.k.a Allah, a.k.a Mohammed linatumika na linaelekea kutumika kuwachinja hawa innocent civilians, inasikitisha sana. Ni bora wangejiita hata M23 tu ijulikane kuliko kujiweka nyuma ya muamvuli wa dini ya kiislamu na kuharibu jina la dini nzuri kabisa yenye kueneza amani, na unakuta baadhi ya waislam wanachekelea na kusema mashallah
Mawazo yako uko Huru kujieleza ila unaemtukana na kumdharau ndie atakaekuhukumu ila ukweli unabaki pale pale walifata nini pale kama sio majasusi?
 
Mawazo yako uko Huru kujieleza ila unaemtukana na kumdharau ndie atakaekuhukumu ila ukweli unabaki pale pale walifata nini pale kama sio majasusi?
Jiangalie nisije sema ktk Jina la Yesu Kristu then ukaanza kupiga makelele, maana nimejawa na upako
 
Nafkir Ela ndio kila kitu mtu anafanya kazi popote ilimradi awe anapokea Mkwanja Mrefu.
Ishu yakufa hata usipofanya kazi utakufa tuuu
 
Bila ya shaka walikua majasusi.ukienda kwa amani kwa hawa jamaa mbona hawana shida
Ni marekani ndio wenye matatizo.hivi kweli chuo kikuu cha marekani ndani ya aAfghanistan?

Kampala International University (KIU) ndani ya tanzania, Uganda hakuna ardhi?
 
Kampala International University (KIU) ndani ya tanzania, Uganda hakuna ardhi?
Ndio tujiulize tukijirizisha pia
Ok Uganda na tz kwanza zimeshikana pili eac tatu africa nne sote weusi tanondugu. Sasa usa na Afghanistan wapi kwa wapi?Kila kitu tofauti.halafu pia t ujiulize wamefata nini hapa kwan wasiwasi ndio akili
 
Ndio tujiulize tukijirizisha pia
Ok Uganda na tz kwanza zimeshikana pili eac tatu africa nne sote weusi tanondugu. Sasa usa na Afghanistan wapi kwa wapi?Kila kitu tofauti.halafu pia t ujiulize wamefata nini hapa kwan wasiwasi ndio akili

uganda hakuna ardhi? hilo ndo swali
 
Back
Top Bottom