KANYEGELO
JF-Expert Member
- Nov 12, 2019
- 2,150
- 4,754
Kwenye kanisa la pale mwenge na matawi yake yote nchini kama ungekuwa ushauri wangu ningetoa maoni waiangalie kwa upya swala la zaka La sivyo umekuwa ni mzigo ambao watu wamebebeshwa ila hawana pa kusemea.
Imewekwa sheria ya KULIPA zaka kila jumapili ya mwisho wa mwezi,ukipitiliza inazidishwa mara tatu .
Na sheria hiyo ni lazima ulipe hiyo zaka ,usipolipa inazidishwa mara tatu, yaani kama zaka yako ni milioni moja ukipitiliza mwezi husika inabidi ulipe milioni nne .Yaani itapigwa milioni moja mara tatu na JUMLISHA na milioni moja unayotakiwa KULIPA
Na usipolipa unakufa kizaka na hutapata huduma zozote za kichungaji hata kama utaumwa,utalazwa,au vyovyote hutapata huduma za kichungaji.
Sasa huyu mwanamke alipitiloza ,deni likawa kubwa....Kwa kuwa alizidi kudaiwa na lilipokuwa kubwa ni kama alipata nafasi ya kujitafakari na kuona kama mbona ni kama ni mateso wakati kutoa ni kwa hiari na upendo??
Akaona hata wacha ahame kanisa.....Na kwa kawaida ukihama kanisa huko unakuwa ni muasi...akaonekana ni muasi,na hata mumewe akamuona anaishi na muasi hakukubaliana na uasi wa mke ambaye mara nyingi alihoji ni vipi zaka imekuwa kama ni kifungo au toza za TRA! kila akiombwa anajibu hana hela na kumbe akaingia gharama ya kamlipia deni lote mkewe,na amekuwa akimwambia mkewe hakuna mahali popote wanapofundisha injili ya kweli zaidi ya hapo full gospel
Wengine wote ni manabii wa uongo na wanaenda motoni
Mwanamke analipiwa pesa ila moyo unamuuma kwasababu anaona kama anatapeliwa......anachojua fika ni kwamba hakuna sadaka za aina hiyo kwa Mungu za kukabana na riba kubwa tofauti na biblia isemavyo.
"Mume wangu anazidi kupeleka pesa na kwamba deni bado halijaisha zinaenda huko imekuwa kama saccos sasa .
Na ni bola hata saccos ukitaka kukopa unaenda kukopa na ukapewa mkopo ,kuliko hivyo"
Mwanamke ndoa yake iko hatihati maana anaambiwa na mumewe
1. AMEANZISHA VITA DHIDI YAKE KAMA MUME
2.DHIDI YA KANISA LA (F......)
3.DHIDI YA ASKOFU MKUU
4.DHIDI UA MAFUNDISHO YA KANISA HILO
5.DHIDI YA MUNGU WANAYE MWAMINI
"SASA VITA HII UMEANZISHA WAULIZE WALIO FANYA VITA NA MIMI KUPINGA IMANI,MUNGU NINAYEMTUMIKIA ATAKUJIBU" maneno ya baba kwa mama.
Swala la zaka pale full gospel hata kama mapato yako yamepungua unaambiwa uza vyote ,hakuna kupunguza kiwango Cha makadilio uliyopangiwa,na vilevile katika ulipaji katika kile kiasi ulichopangiwa inapaswa ulipe ndani ya mwezi mpaka jumapili ya mwisho wa mwezi husika na usipolipa ndio unapigwa penati mara tatu kipa akiwa hayupo.
Na hapo Kuna changizo pia Kila mwezi ,kanuni ya changizo unalipa nusu ya zaka .Yaani kama zaka ni milioni moja ,changizo ni laki tano ,Hivyo inakulazimu Kila mwezi milioni moja na nusu bila kukosa ,ukirukisha inajizidisha mara tatu
Kabla ya kuanza KULIPA Kuna fomu unajaza ,kuhusu mapato yako Kisha unakadiriwa kadirio la juu kuwa utalipa kiasi Fulani. Na kama labda umepoteza kazi,au biashara zimeyumba huruhusiwi kupunguza zaka ,unaambiwa uza vyote.....
Huyu dada anasema
"Kilichoniumiza ni kwamba nimehama,lakini Mume Wangu ananiambia nimeasi ,yaani nimerudi nyuma katika wokovu....Ni mtu mwenye pesa lakini nanyimwa pesa mimi, anatuma huko katika account kile kiasi ambacho nilikadiriwa.
#My_take
Utoaji wa aina hii hauna tofauti na ule wa kujimaliza pale kawe ingawa pale ni afadhali maana hulazimishwi ila unatoa Kwa hiari sawa na ulivyoamini fundisho.
Hauna tofauti na ule wa Ngomeni pale kimara
Mimi sipingi utoaji wa zaka ila nasisitiza watu watoe kwa upendo na kwa hiari yao ili baraka ziwaendee kikamilifu kuliko utoaji wa torati wa aina hii.....
Mzee Kakobe anapiga penati za zaka kuliko hata torati ilivyosema.
Eti kuna watumishi wanapiga mpaka simu kwa washirika kudai zaka?
Hivi wanaieleweje biblia? Mbona watumishi mnajiweka maungo wazi kwa kitu kinaitwa pesa??
Ndio maana watoaji wa zaka wengi kwenye mifumo ya aina hii wanapitia hali ngumu sana......watoaji wa zaka jifunzeni kumhusisha na kumsikiliza Mungu kwenye utoaji wa fungu la kumi mtakuja kunishukuru niko nimekaa pale. Kuna watu mtaambiwa pale usipeleke zaka ila peleka pale.
Kumbukumbu 12
¹³ Ujihadhari usitoe sadaka zako zako katika kila mahali upaonapo;
¹⁴ bali katika mahali atakapopachagua Bwana ndipo utakapotoa sadaka zako, ndipo utakapotenda yote nikuamuruyo.
HALAFU ZAKA HATULIPI JAMANI,TUNATOA KWA MOYO WA KUPENDA,NDANI YA ZAKA KUNA SHUKRANI JUU YA YOTE ATUTENDEAYO BWANA. WEWE UNALIPA TOZO NDIO MAANA HAZIPOKELEWI, HAKUNA MTU MIONGONI MWENU MWENYE KUMLIPA MUNGU CHOCHOTE HAPA DUNIANI.
Imewekwa sheria ya KULIPA zaka kila jumapili ya mwisho wa mwezi,ukipitiliza inazidishwa mara tatu .
Na sheria hiyo ni lazima ulipe hiyo zaka ,usipolipa inazidishwa mara tatu, yaani kama zaka yako ni milioni moja ukipitiliza mwezi husika inabidi ulipe milioni nne .Yaani itapigwa milioni moja mara tatu na JUMLISHA na milioni moja unayotakiwa KULIPA
Na usipolipa unakufa kizaka na hutapata huduma zozote za kichungaji hata kama utaumwa,utalazwa,au vyovyote hutapata huduma za kichungaji.
Sasa huyu mwanamke alipitiloza ,deni likawa kubwa....Kwa kuwa alizidi kudaiwa na lilipokuwa kubwa ni kama alipata nafasi ya kujitafakari na kuona kama mbona ni kama ni mateso wakati kutoa ni kwa hiari na upendo??
Akaona hata wacha ahame kanisa.....Na kwa kawaida ukihama kanisa huko unakuwa ni muasi...akaonekana ni muasi,na hata mumewe akamuona anaishi na muasi hakukubaliana na uasi wa mke ambaye mara nyingi alihoji ni vipi zaka imekuwa kama ni kifungo au toza za TRA! kila akiombwa anajibu hana hela na kumbe akaingia gharama ya kamlipia deni lote mkewe,na amekuwa akimwambia mkewe hakuna mahali popote wanapofundisha injili ya kweli zaidi ya hapo full gospel
Wengine wote ni manabii wa uongo na wanaenda motoni
Mwanamke analipiwa pesa ila moyo unamuuma kwasababu anaona kama anatapeliwa......anachojua fika ni kwamba hakuna sadaka za aina hiyo kwa Mungu za kukabana na riba kubwa tofauti na biblia isemavyo.
"Mume wangu anazidi kupeleka pesa na kwamba deni bado halijaisha zinaenda huko imekuwa kama saccos sasa .
Na ni bola hata saccos ukitaka kukopa unaenda kukopa na ukapewa mkopo ,kuliko hivyo"
Mwanamke ndoa yake iko hatihati maana anaambiwa na mumewe
1. AMEANZISHA VITA DHIDI YAKE KAMA MUME
2.DHIDI YA KANISA LA (F......)
3.DHIDI YA ASKOFU MKUU
4.DHIDI UA MAFUNDISHO YA KANISA HILO
5.DHIDI YA MUNGU WANAYE MWAMINI
"SASA VITA HII UMEANZISHA WAULIZE WALIO FANYA VITA NA MIMI KUPINGA IMANI,MUNGU NINAYEMTUMIKIA ATAKUJIBU" maneno ya baba kwa mama.
Swala la zaka pale full gospel hata kama mapato yako yamepungua unaambiwa uza vyote ,hakuna kupunguza kiwango Cha makadilio uliyopangiwa,na vilevile katika ulipaji katika kile kiasi ulichopangiwa inapaswa ulipe ndani ya mwezi mpaka jumapili ya mwisho wa mwezi husika na usipolipa ndio unapigwa penati mara tatu kipa akiwa hayupo.
Na hapo Kuna changizo pia Kila mwezi ,kanuni ya changizo unalipa nusu ya zaka .Yaani kama zaka ni milioni moja ,changizo ni laki tano ,Hivyo inakulazimu Kila mwezi milioni moja na nusu bila kukosa ,ukirukisha inajizidisha mara tatu
Kabla ya kuanza KULIPA Kuna fomu unajaza ,kuhusu mapato yako Kisha unakadiriwa kadirio la juu kuwa utalipa kiasi Fulani. Na kama labda umepoteza kazi,au biashara zimeyumba huruhusiwi kupunguza zaka ,unaambiwa uza vyote.....
Huyu dada anasema
"Kilichoniumiza ni kwamba nimehama,lakini Mume Wangu ananiambia nimeasi ,yaani nimerudi nyuma katika wokovu....Ni mtu mwenye pesa lakini nanyimwa pesa mimi, anatuma huko katika account kile kiasi ambacho nilikadiriwa.
#My_take
Utoaji wa aina hii hauna tofauti na ule wa kujimaliza pale kawe ingawa pale ni afadhali maana hulazimishwi ila unatoa Kwa hiari sawa na ulivyoamini fundisho.
Hauna tofauti na ule wa Ngomeni pale kimara
Mimi sipingi utoaji wa zaka ila nasisitiza watu watoe kwa upendo na kwa hiari yao ili baraka ziwaendee kikamilifu kuliko utoaji wa torati wa aina hii.....
Mzee Kakobe anapiga penati za zaka kuliko hata torati ilivyosema.
Eti kuna watumishi wanapiga mpaka simu kwa washirika kudai zaka?
Hivi wanaieleweje biblia? Mbona watumishi mnajiweka maungo wazi kwa kitu kinaitwa pesa??
Ndio maana watoaji wa zaka wengi kwenye mifumo ya aina hii wanapitia hali ngumu sana......watoaji wa zaka jifunzeni kumhusisha na kumsikiliza Mungu kwenye utoaji wa fungu la kumi mtakuja kunishukuru niko nimekaa pale. Kuna watu mtaambiwa pale usipeleke zaka ila peleka pale.
Kumbukumbu 12
¹³ Ujihadhari usitoe sadaka zako zako katika kila mahali upaonapo;
¹⁴ bali katika mahali atakapopachagua Bwana ndipo utakapotoa sadaka zako, ndipo utakapotenda yote nikuamuruyo.
HALAFU ZAKA HATULIPI JAMANI,TUNATOA KWA MOYO WA KUPENDA,NDANI YA ZAKA KUNA SHUKRANI JUU YA YOTE ATUTENDEAYO BWANA. WEWE UNALIPA TOZO NDIO MAANA HAZIPOKELEWI, HAKUNA MTU MIONGONI MWENU MWENYE KUMLIPA MUNGU CHOCHOTE HAPA DUNIANI.