Mapenzi yananitatiza

Pendaneni

Senior Member
Feb 12, 2014
134
108
Jamani mapenzi, yananitatiza, Kulala siwezi, kusema siwezi
Chakula sitaki, nakiiona sumu, Mapenzi yamenivaa, nami ugenini
Akili imenipaa, hata njia siioni, Mapenzi yana hadaa, ya kweli nawambieni

Haiba imepotea, uzuri umenitoka, mali imeangamia, maradhi hayakutoka,
Mwenzenu nimepotea, muokozi kanitoka, Enyi wenye ukarimu, siri nawatobolea
Moyo umepata sumu, madawa hayakufaa, Kupenda kitu adimu, nawambia kuna baa

Ya kweli nawambieni, myatie akilini msipende ugenini, mtaingia hatiani
Mtalala majiani , wazimu tele vichwani:)
 
Miss Chagga wahenga walisema 'mapenzi ni utumwa' na kupenda ni maradhi omba sana yasikukute! Maana hayo maradhi hayana tiba asilani.......
Mafikizolo sasa unanishauri niachane na mapenzi nifanye nini zaidi!! Siwezi kuukataa uasilia jamani!
 
Mkuu unajua umekua ukicomplain sana kuusu mapenzi kukutesa, sasa jamani kama kitu unaona unafanya chakunyima raha,amani achana nacho,hata mfanya biashara akianzisha biashara akaona haimlipi huachana nao,unafanya vitu vingine,Ongea na Mungu muombe sana haya yataisha
Miss Chagga wahenga walisema 'mapenzi ni utumwa' na kupenda ni maradhi omba sana yasikukute! Maana hayo maradhi hayana tiba asilani.......
Mafikizolo sasa unanishauri niachane na mapenzi nifanye nini zaidi!! Siwezi kuukataa uasilia jamani!
 
Jamani mapenzi, yananitatiza, Kulala siwezi, kusema siwezi
Chakula sitaki, nakiiona sumu, Mapenzi yamenivaa, nami ugenini
Akili imenipaa, hata njia siioni, Mapenzi yana hadaa, ya kweli nawambieni

Haiba imepotea, uzuri umenitoka, mali imeangamia, maradhi hayakutoka,
Mwenzenu nimepotea, muokozi kanitoka, Enyi wenye ukarimu, siri nawatobolea
Moyo umepata sumu, madawa hayakufaa, Kupenda kitu adimu, nawambia kuna baa

Ya kweli nawambieni, myatie akilini msipende ugenini, mtaingia hatiani
Mtalala majiani , wazimu tele vichwani:)


HATA MAREHEMU MBARAKA mwishehe Mwaruka aliimba hivyo hivyo, hayo ni marudio tuuu.
 
Bila shaka unamiaka kati ya 15 - 20 au kama umezidi miaka hiyo basi ulichelewa kuanza mapenzi.
 
Mapenzi matamu bwana
1454496441253.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom