Mapenzi ya siku hizi bwana

Mapenzi ya siku hizi bwana

Ze Chinji

New Member
Joined
May 24, 2013
Posts
2
Reaction score
0
Mapenzi ya siku hizi yana mtazamo wa tofauti na yale ya zamani.
Mapenzi ya zamani mtu alikuwa yuko radhi kufanya lolote kuhakikisha anamuonesha mapenzi ya kweli yule mpenzi wake kwa hali yoyote nikimaanisha maskini au tajiri lakini kwa sasa ni tofauti kabisa.

Mwanaume au mwanamke kwa enzi za sasa anaangalia je yule ninayekwenda kumpenda ana hela,so siku hizi kigezo cha mapenzi ni pesa mambo mengine baadae japo kuna wachache wanaopenda kikweli bila kuangalia hali ya uchumi.
Kwa hiyo hebu tujaribu kuangalia na kujifunza mapenzi ya zamani yalikuwaje na walikuwa wanafanyaje ili tuweze kupendana kufuatana na mila na desturi za taifa letu.
 
kila kitu kinabadilika na mfumo wa mapenz haupo kwenye kisiwa chake chenyewe sema binadam mgumu kupokea mabadiliko
 
watu wanazungumzaga tu pesa
bila kuwa na unit moja
kuna watu milioni ni pesa
na kuna watu milioni sio pesa

so tunaposema tu pesa kwa ku generalize..tuzingatie haya
 
Mapenzi ya zamani ya KIMASKINI mda wake ulisha expire! Tumehamia digitali tunaangali MONEY in the longrun watoto wetu hawatoangalia pesa tena but WEALTH of a man hivo hivo.

Sasa badala ya kukaa kungoja mapenzi ya zamani yarudi wewe fight ku acquire money and live in your times not your grand grand pa times kama enzi za Kuntakinte!!!!!!!!!
 
Hizo zamani mijadala kama hii ilikuwa kwa njia gani????!!!!!!!
Unajua tofauti ya shanti na nivea???!!!!
Cobra na joop????
Tofauti ya clere c na victorias secret???!!!!!
 
Mambo yanabadilika mnataka vitu vingine vyote vichange halafu MAPENZI ya remain Constant

haiwezekani!!!!!!!!
 
Hapo umeongea point sana, siku hizi wenye mapenzi ya kweli niwachache sana, wale waliofundishwa maadili ya mema ya kitanzania, wengi mapenzi yao ni ya biashara , hakuna tofauti changudoa na mpenzi wako,kwani wote huwezi kulala nao kama huna pesa, mpenzi wako huwezi kuishi nayekama huna pesa. Mwanaume wapenzi wengi anaowanunua kwaajili ya ngono na mwanamke anawapenzi wengi anao wauzi mwili wake iliapate pesa.mpenzi yakweli hutoka moyoni,huzaliwa, hukua na kuzaa matunda na kama hayakutunzwa basi hunyauka na kukauka
 
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom