P. Majaribu
JF-Expert Member
- Jun 2, 2014
- 1,192
- 625
Wewe endelea kupoteza muda tu,mambo yamebadilika sana.Sio kweli na km hivo si wafanye usaili wenyew huko huko km TRA na vikosi vya ulinzi, unapoteza umma ww.
Wewe endelea kupoteza muda tu,mambo yamebadilika sana.Sio kweli na km hivo si wafanye usaili wenyew huko huko km TRA na vikosi vya ulinzi, unapoteza umma ww.
Wewe endelea kupoteza muda tu,mambo yamebadilika sana.
Inawezekana kabisa sekretariet inakua na nia nzuri ila nia inapotea kwa kulazimishwa kufuata maelekezo ya wakubwa fulani ambayo husababisha utendaji wake kuchafuka, na ndio maana kinahitajika chombo huru ambacho si kwamba kitakua kinasikilza malalamiko tu bali pia kitailinda sekretariet na kuifanya iwe huru kiutendaji. Kwa mfano usahili wa National Audit Office (NAO), pale naweza kusema kwa uhakika kuwa sekretariet ilifanya makosa ya wazi japo hawawezi kiri, na inaonekana ilikua nje ya uwezo wao kuepuka walicho kifanya
Kazi zipo omba na kuomba,ukisema kazi zinawenyewe na wakati kila leo watoto wa wakulima wanapata kazi
Walifanya nini?
hawa utumishi wanavituko sana siku hizi,walitangaza nafasi ya mkurugenzi mkuu chuo cha taifa cha utalii na waliweza kushorlist watu sita, matokeo yake waliita watu wawili tu, mmoja akiwa mkurugenzi aliyemaliza muda wake na mwingine ni ni mwalimu wa hapohapi chuoni. Lakini habari za uhakika ni kwamba huyo mkurugenzi anahonga watu wa utumishi ili aletewe watu ambao hawana ushindani kwake au akikujua kwamba umeomba hiyo kazi na nitishio kwake basi atakutafuta na kukuhonga ili usionekane kwenye interview. Cha ajabu kingine ni kwamba hata majina ya walioitwa kwenye interview hayakuwekwe kwenye website yao. Kimsingi secretarieti ya ajira siyo ya kuitegemea sana.tunashukuru kwa kazi ambayo sekretarieti ya ajira wamekua wakiifanya, japo mapungufu yapo lakini pia wamesaidia ajira za serikalini kufahamika wazi panapokua na uhitaji.
Lakini ingependeza zaidi kama pangekuwepo na chombo huru ambacho kinaikagua sekretarieti katika utendaji na utekelezaji wa shughuli zake; ili kuhakikisha taratibu, sheria na kanuni zinafuatwa. Chombo hiki pia kipewe mamlaka ya kusikiliza malalamiko yenye mashiko kwa watu ambao hawajaridhika na utendaji wa sekretarieti katika jambo flani au kwa ujumla, na kutengua maamuzi ya sekretarieti pale inapobidi, maana kadiri siku zinavyo songa mbele weledi wa sekretarieti unaonekana kushuka na inaonekana kufanya kazi kwa mazoea.
Hii itasaidia kuboresha mfumo wa ajira nchini hasa kupitia kwa sekretarieti na kupunguza madhaifu ambayo yamekua yakiumiza na kusikitisha sana haswa kwa "watoto wa wakulima".
Narudia tena kuishukuru na kuipongeza sekretarieti katika yale iliyofanikisha, na kwa yale madhaifu naamini uwepo wa chombo hicho utayapunguza.
Nawasilisha.