WISE BOY
JF-Expert Member
- Dec 26, 2011
- 782
- 244
Tunashukuru kwa kazi ambayo sekretarieti ya ajira wamekua wakiifanya, japo mapungufu yapo lakini pia wamesaidia ajira za serikalini kufahamika wazi panapokua na uhitaji.
Lakini ingependeza zaidi kama pangekuwepo na chombo huru ambacho kinaikagua sekretarieti katika utendaji na utekelezaji wa shughuli zake; ili kuhakikisha taratibu, sheria na kanuni zinafuatwa. Chombo hiki pia kipewe mamlaka ya kusikiliza malalamiko yenye mashiko kwa watu ambao hawajaridhika na utendaji wa sekretarieti katika jambo flani au kwa ujumla, na kutengua maamuzi ya sekretarieti pale inapobidi, maana kadiri siku zinavyo songa mbele weledi wa sekretarieti unaonekana kushuka na inaonekana kufanya kazi kwa mazoea.
Hii itasaidia kuboresha mfumo wa ajira nchini hasa kupitia kwa sekretarieti na kupunguza madhaifu ambayo yamekua yakiumiza na kusikitisha sana haswa kwa "watoto wa wakulima".
Narudia tena kuishukuru na kuipongeza sekretarieti katika yale iliyofanikisha, na kwa yale madhaifu naamini uwepo wa chombo hicho utayapunguza.
Nawasilisha.
Lakini ingependeza zaidi kama pangekuwepo na chombo huru ambacho kinaikagua sekretarieti katika utendaji na utekelezaji wa shughuli zake; ili kuhakikisha taratibu, sheria na kanuni zinafuatwa. Chombo hiki pia kipewe mamlaka ya kusikiliza malalamiko yenye mashiko kwa watu ambao hawajaridhika na utendaji wa sekretarieti katika jambo flani au kwa ujumla, na kutengua maamuzi ya sekretarieti pale inapobidi, maana kadiri siku zinavyo songa mbele weledi wa sekretarieti unaonekana kushuka na inaonekana kufanya kazi kwa mazoea.
Hii itasaidia kuboresha mfumo wa ajira nchini hasa kupitia kwa sekretarieti na kupunguza madhaifu ambayo yamekua yakiumiza na kusikitisha sana haswa kwa "watoto wa wakulima".
Narudia tena kuishukuru na kuipongeza sekretarieti katika yale iliyofanikisha, na kwa yale madhaifu naamini uwepo wa chombo hicho utayapunguza.
Nawasilisha.