Mapambano yanaendelea

Mapambano yanaendelea

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Asitokee mtu kujifanya yeye hafanyi. Isisikike sauti ya kulaumu kinachoendelea kwakuwa wote wanafanya sawa. UKAWA dhidi ya CCM na washirika wake wanaendelea na mapambano ndani na nje ya Bunge la Katiba. Mapambano ya kujenga na kuimarisha demokrasia na mustakabali wa Taifa hili.

UKAWA wameanza mikutano ya nje ya Bunge.Wameanzia Mwanza. CCM nao,kwa mwamvuli wa ziara za Katibu Mkuu wao Kinana,wanatembea wakijadili masuala hayo hayo ya Katiba kwenye mikutano ya hadhara. Walianzia Mwembeyanga Temeke,jijini Dar es Salaam. Mwigulu Nchemba,Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara,ameibukia kanisani na kueleza kuhusu Katiba mpya.

Nasema asije akaonekana mmoja ni mkorofi na mwenye kuharibu mchakato wa Katiba mpya.Kwakuwa pande zote ziko kwenye mapambano. Na kwenye mapambano,mbinu mbalimbali hutumika. Asiombe mtu poo. Katiba ni Sheria mama ya nchi.Kuandikwa kwake lazima kuambatane na mapambano ili ikipatikana ipatikane yenye meno kweli. Katiba nzuri haitapatikana kwa lelemama.

UKAWA pigeni kazi nje na ndani ya Bunge;CCM endeleeni kukisemea na kukisimamia mnachokiamini. Mapambano yanaendelea..
 
Huu upuuzi unaofanywa ktk katiba mpya ni kuteketeza hela tu! Katiba ya upuuzi wa sera za CCM utakwama kwenye kura za wananchi, na ikipita TZ bara itakwama TZ visiwani!
...
Na katiba ikifeli CCM mjiandae kutuua tu, hatukubali kamwe kuendelea kutumia katiba ya kifisadi iliyopo!
 
wajumbe wanapiga tu ela zetu, hamna katiba wala nini, ni msimu tu huu tunapita, na sisi tuandike historia ya kujaribu kupata katiba mpya.
 
Muungano wetu ulikuwa wa nchi mbili za TANGANYIKA na zanzibar kuunda Tanzania. Tunaona zanzibar bado ipo tena ikijitangaza kama nchi kamili lakini TANGANYIKA hatuioni japo kila Desemba 9 tunaadhimisha uwepo wake. Tunahitaji Tanganyika inayoonekana na kama ilivyo Zanzibar. Tanganyika kwanza Tanzania baadaye
 
Back
Top Bottom