Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,768
- 49,934
Wananchi hatupingi kuchangia shughuli za maendeleo kwaajili ya ustawi wa Taifa letu, lakini uchangiaji huo uwe unazingatia uhalisia wa maisha ya watanzania.
Wananchi tutambue kuwa hatuna wa kututetea. Serikali inatudidimiza badala ya kutuwezesha. Bunge linatuzika badala ya kutufufua.
Tukisema tuandamane ili kuelezea hisia zetu za kutoridhishwa na ongezeko la zaidi ya 100% kwenye huduma za utumaji na upokeaji fedha kwa kupitia mitandao ya simu, mjue akina afande Muroto bado wapo hai, wao wanajua kuwa kazi kubwa ya Polisi ni kutoa kipigo cha mbwa koko na siyo kuwalinda raia.
Chaguo tulilo nalo ni hili ambalo hakuna atakayetugusa:
1) Wananchi tujibane kwa namna yoyote tuwezayo, kila mmoja asitume wala kutoa fedha kupitia mtandao wa simu kwa muda wa siku 14. Hiyo iwe ni kuanzia leo.
2) Wananchi tusitumie simu za mkononi kuongea kwa siku 14, isipokuwa kwa dharula tu kama vile ugonjwa na misiba. Mawasiliano yawe kwa sms, fb na whatsapp.
3) Kila mmoja ajitahidi kuwapata watu wasiopungua 20 ambao nao watafikishiwa ujumbe huu, na wao wawafikishie wengine.
Ukombozi wetu upo mikononi mwetu wenyewe. Mtambue ukombozi una gharama kubwa. Wapo waliopoteza maisha, ndiyo sisi tukawa huru. Wapo waliofungwa ndiyo sisi tukawa huru. Wapo waliolemazwa, ndiyo sisi tukawa huru. Sisi, hakuna atakayekufa, hakuna atakayepata ulemavu, hakuna atakayefungwa kwa kujitoa katika hili. Maumivu yatakuwepo kiasi kidogo sana kwa kuikosa huduma tuliyokuwa tumeizoea
Wanaounga mkono wagonge like. Na tusiishie kwenye kubonyeza like. Ukigonga tu kitufe cha like, toka dakika hiyo unaanza kutekeleza.
Maoni ya namna ya kuboresha litakuwa ni jambo jema.
Wananchi tutambue kuwa hatuna wa kututetea. Serikali inatudidimiza badala ya kutuwezesha. Bunge linatuzika badala ya kutufufua.
Tukisema tuandamane ili kuelezea hisia zetu za kutoridhishwa na ongezeko la zaidi ya 100% kwenye huduma za utumaji na upokeaji fedha kwa kupitia mitandao ya simu, mjue akina afande Muroto bado wapo hai, wao wanajua kuwa kazi kubwa ya Polisi ni kutoa kipigo cha mbwa koko na siyo kuwalinda raia.
Chaguo tulilo nalo ni hili ambalo hakuna atakayetugusa:
1) Wananchi tujibane kwa namna yoyote tuwezayo, kila mmoja asitume wala kutoa fedha kupitia mtandao wa simu kwa muda wa siku 14. Hiyo iwe ni kuanzia leo.
2) Wananchi tusitumie simu za mkononi kuongea kwa siku 14, isipokuwa kwa dharula tu kama vile ugonjwa na misiba. Mawasiliano yawe kwa sms, fb na whatsapp.
3) Kila mmoja ajitahidi kuwapata watu wasiopungua 20 ambao nao watafikishiwa ujumbe huu, na wao wawafikishie wengine.
Ukombozi wetu upo mikononi mwetu wenyewe. Mtambue ukombozi una gharama kubwa. Wapo waliopoteza maisha, ndiyo sisi tukawa huru. Wapo waliofungwa ndiyo sisi tukawa huru. Wapo waliolemazwa, ndiyo sisi tukawa huru. Sisi, hakuna atakayekufa, hakuna atakayepata ulemavu, hakuna atakayefungwa kwa kujitoa katika hili. Maumivu yatakuwepo kiasi kidogo sana kwa kuikosa huduma tuliyokuwa tumeizoea
Wanaounga mkono wagonge like. Na tusiishie kwenye kubonyeza like. Ukigonga tu kitufe cha like, toka dakika hiyo unaanza kutekeleza.
Maoni ya namna ya kuboresha litakuwa ni jambo jema.