Mapambano dhidi ya rushwa: Tujifunze toka Rwanda

Mapambano dhidi ya rushwa: Tujifunze toka Rwanda

mwengeso

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2014
Posts
9,286
Reaction score
6,727
Kichwa cha mada hii ni cha gazeti la Mwananchi - alhamisi, septemba 10, 2015 kuhusu makala ya Prof. L. Lipumba.

Kabla ya kuchangia makala hiyo niwaombe wana jamvi tupunguze kuweka picha za nyomi za mikutano ya kampeni kana kwamba ndiyo kura halisi. Tuchukue muda wetu kurejea sera, ilani za vyama na ahadi za wagombea kwenye kampeni kama zinakidhi matarajio yetu ya mabadiliko. Mimi ninayaita mabadiliko ya kifikra na kiutendaji kwa kila Mtanzania. Hivyo kura yangu nitampa kiongozi yule tu atakaye nishawishi kuwa anayo mikakati ya kuleta mabadiliko hayo.

Prof. Lipumba kwenye makala hiyo anasema: "Rushwa na ufisadi ni adui wa haki na pia ni kikwazo kikubwa cha maendeleo.... Madhara ya rushwa ni mengi. Viongozi wanatumia vibaya madaraka yao kwa maslahi binafsi. Inasababisha Serikali na Asasi zake kushindwa kufikia malengo yake. Mapato ya Serikali hayakusanywi ipasavyo". Anatoa mfano wa Rwanda ambako imeundwa Ofisi ya Mchunguzi Maalum (Ombudsman) inayosimamia na kuratibu kuzuia na kupambana na rushwa, kwetu ni TAKUKURU. Pia Rwanda imeanzisha "Baraza la Ushauri la Taifa la kuzuia na Kupambana na Rushwa. Pia kuna Mabaraza ya Ushauri katika ngazi za chini." Amenukuliwa Prof. Lipumba.

Kwenye kampeni zinazoendelea tumemsikia JPMagufuri akiahidi kuunda mahakama ya kushughulikia mafisadi na kwamba akiingia tu madarakani ni kuwakamata hao mafisadi. Kwa jinsi anavyotamuka ni wazi hilo linatoka moyoni mwako na kwamba anatambua na kubainisha 'rushwa na ufisadi' ni kero namba moja ya watanzania na maendeleo. Gazeti hilohilo la Mwananchi, limenukua kampeni zake Mkoani Tanga kwamba "Dk Magufuri alisema anataka Serikali yake iwe rafiki kwa wafanya biashara wote, lakini wawekezaji wakubwa ni lazima waondolewe misamaha ya kodi isiyokuwa na tija ili fedha zitakazopatikana zisaidie kuendeleza miradi mbalimbali ya Serikali". Hilo likiwa jibu la Prof Lipumba kuhusu mapato ya Serikali kutokukusanywa ipasavyo kwa sababu ya kukithiri kwa vitendo vya rushwa.

Nahitimisha kwa kusema hadi sasa ni mgombea Urais wa CCM (Dk Magufuri), tofauti na vyama vingine, ambaye amejipambanua wazi kwamba rushwa na ufisadi ndio adui na moja wa maendeleo ya nchi hii. Nitampa kura yangu.
 
kusema sii kutenda je jeno lisemwalo kiongozi lazma amlinde kiongozi aliyepita hapo vp
 
mwengeso

Mimi natofautiana kabisa na maudhui ya mada hii. Nimeapa Katu sitompa kura yangu kiongozi yoyote yule simply kwa kutoa ahadi tu. Watanzania tuache hizi cheap politics za kudanywa danganywa kwenye majukwaa ya siasa hasa katika kipindi cha campaign. Sote tunafahamu ya kwamba CCM ndio inayowalea na kuwakumbatia hao wala rushwa na MAFISADI (rejea maneno ya Kinana na Nape).

Mwengeso huyu unayempigia kampeni wewe anatoka chama hicho hicho cha MAFISADI na wala rushwa. Dr. Magufuri (Kama unavyomuita mwenyewe) pindipo akichaguliwa kuwa Raisi wa nchi hii basi kuna uwezekano mkubwa wa kuwa yeye kuwa ni MWENYEKITI wa Chama cha MAFISADI na wala rushwa. Hivi ni kweli inaingia akilini ya kwamba mwenyekiti wa chama cha mafisadi kupiga vita ufisadi na Rushwa simply kwa kutudanganya majukwaani kama watoto wa kuku tu?

Watanzania hatudanganyiki tena maana nimejifunza ya mwaka 2010 tuliempa kura zetu alituahidi MAISHA BORA lakini tumeambulia MAISHA DUNI. Hitimisho: Watanzania tufikiri na kwa kutumia ubongo na sio makalio maana kipindi tutaahidiwa mpaka pepo wakati bado tuko duniani.
 
Last edited by a moderator:
Kura yangu inakwenda UKAWA. Ccm wamekuwepo madarakani kwa zaidi ya nusu karne. wamezalisha rushwa na ufisadi na kia mwaka wanatoa sera na maneno lukuki ambayo wameshindwa kuyatelekeza.

Ccm wala magufuli hawana lengo, nia wala uwezo wa kupambana na maslahi yao binafsi. Nani aliyekuambia tatizo la ufisadi na rushwa ni udhaifu wa ki makama au sheria zetu Lini ccm iliwafikisha mafisadi mahakamani ikashindikana kwa sababu ya legal structure?

Inakupasa kuwa mkweli.

Propaganda zako zimechelewa. Mlikuwa na miaka 50 ya kufanya mema lakini mkafanya mabaya na kutu abuse.

TUNACHAGUA UKAWA. UMESIKIA WEWE?
 
mwengeso

Magufuli kwanini hakumshauri Kikwete afungue hiyo mahakama ya mafisadi anayotaka kufungua
 
Last edited by a moderator:
Ccm ni waigizaji tu, anakwambia TZ yake ni ya viwanda miaka 10 iliyopita wamefufua vingapi? , atafunga mafisadi je hao wanaokupereka madarakan utawafunga, yeye mwenyewe atajifunga? Uongo mtupu
 
Hao mafisadi watakaoshughulikiwa na mahakama ya magufuri ni wakina nani na kwanini hawakushughulikiwa kwenye huu utawala wa awamu ya nne?
 
Kura yangu inakwenda UKAWA. Ccm wamekuwepo madarakani kwa zaidi ya nusu karne. wamezalisha rushwa na ufisadi na kia mwaka wanatoa sera na maneno lukuki ambayo wameshindwa kuyatelekeza.

Ccm wala magufuli hawana lengo, nia wala uwezo wa kupambana na maslahi yao binafsi. Nani aliyekuambia tatizo la ufisadi na rushwa ni udhaifu wa ki makama au sheria zetu Lini ccm iliwafikisha mafisadi mahakamani ikashindikana kwa sababu ya legal structure?

Inakupasa kuwa mkweli.

Propaganda zako zimechelewa. Mlikuwa na miaka 50 ya kufanya mema lakini mkafanya mabaya na kutu abuse.

TUNACHAGUA UKAWA. UMESIKIA WEWE?

CHADEMA ni waasisi wa kupambana na ufisadi, inakuaje wanakuwa kimya, au ilikuwa funika kombe mwanaharamu apite!!!!
 
Hao mafisadi watakaoshughulikiwa na mahakama ya magufuri ni wakina nani na kwanini hawakushughulikiwa kwenye huu utawala wa awamu ya nne?

Baada ya tarehe 25/10 hao mafisadi utawasikia wakiwa jela, labda watoroke mapema. Wengine CHADEMA inawajua na itasaidia kuwataja zaidi ya wale 11 iliyokwisha kuwataja. Mashabiki na wanachama wa UKAWA, kama wewe, nanyi mnawafahamu kisa cha kusema CCM ni ya mafisadi. Hao hao mafisadi wa CCM watakamatwa kama walivyokatwa na wengine kuhamia UKAWA.
 
Mimi natofautiana kabisa na maudhui ya mada hii. Nimeapa Katu sitompa kura yangu kiongozi yoyote yule simply kwa kutoa ahadi tu. Watanzania tuache hizi cheap politics za kudanywa danganywa kwenye majukwaa ya siasa hasa katika kipindi cha campaign. Sote tunafahamu ya kwamba CCM ndio inayowalea na kuwakumbatia hao wala rushwa na MAFISADI (rejea maneno ya Kinana na Nape). Mwengeso huyu unayempigia kampeni wewe anatoka chama hicho hicho cha MAFISADI na wala rushwa. Dr. Magufuri (Kama unavyomuita mwenyewe) pindipo akichaguliwa kuwa Raisi wa nchi hii basi kuna uwezekano mkubwa wa kuwa yeye kuwa ni MWENYEKITI wa Chama cha MAFISADI na wala rushwa. Hivi ni kweli inaingia akilini ya kwamba mwenyekiti wa chama cha mafisadi kupiga vita ufisadi na Rushwa simply kwa kutudanganya majukwaani kama watoto wa kuku tu?
Watanzania hatudanganyiki tena maana nimejifunza ya mwaka 2010 tuliempa kura zetu alituahidi MAISHA BORA lakini tumeambulia MAISHA DUNI. Hitimisho: Watanzania tufikiri na kwa kutumia ubongo na sio makalio maana kipindi tutaahidiwa mpaka pepo wakati bado tuko duniani.

Ahadi zinazotolewa na wagombea wa UKAWA zina uthibisho gani zitatekelezwa! Hao mamluki kutoka Serikali ya CCM walikuwa wapi wakati maovu yanafanyika! Kama kweli wanaitakia nchi hii mabadiliko, wajibu kwa nini walichukua fomu za kugombea ndani ya CCM. Naomba msiwasemehe kama vile mbavyoshangilia wakianika madudu waliyofanya na wenzao wakiwa CCM.

Nchi hii inakosa viongozi waadilifu. Magufuri amejipambanua kuwa na nia ya kurejesha uadilifu na uwajibikaji kwangu na kwako tusio timiza wajibu wetu, lakini lawama inabebwa na Chama na Serikali yake. Nesi anamzungusha mama wa watu mjamzito ila apewe chochote, unasema ati ni Chama. Aibu kwa ufafanuzi wa kero za wananchi hivyo.
 
Ahadi zinazotolewa na wagombea wa UKAWA zina uthibisho gani zitatekelezwa! Hao mamluki kutoka Serikali ya CCM walikuwa wapi wakati maovu yanafanyika! Kama kweli wanaitakia nchi hii mabadiliko, wajibu kwa nini walichukua fomu za kugombea ndani ya CCM. Naomba msiwasemehe kama vile mbavyoshangilia wakianika madudu waliyofanya na wenzao wakiwa CCM. Nchi hii inakosa viongozi waadilifu. Magufuri amejipambanua kuwa na nia ya kurejesha uadilifu na uwajibikaji kwangu na kwako tusio timiza wajibu wetu, lakini lawama inabebwa na Chama na Serikali yake. Nesi anamzungusha mama wa watu mjamzito ila apewe chochote, unasema ati ni Chama. Aibu kwa ufafanuzi wa kero za wananchi hivyo.
Mwengeso sijui hujielewi au unalipwa kiasi gani kushabikia CCM. Tatizo la chama chako cha CCM si mtu mmoja mmoja bali ni MFUMO MZIMA uliokosa UADILIFU na UWAJIBIKAJI ambao ni tofauti na mfumo wa UKAWA. Serikali zote za CCM zilizopita basi zimeshindwa kabisa kumjali raia wa nchi hii. Zimeshindwa hata kumtimizia mtanzania japo zile haki zake za msingi (Kama Afya bora, elimu bora , maji safi, lishe bora n.k). Maisha ya mtanzania wa leo yamezidi kuwa duni wakati tuliahidiwa MAISHA BORA. CCM imeandaa mazingira ya kirushwa na kifisadi katika nchi hii kiasi ambacho kiongozi wa CCM anaona kama rushwa ya BILLIONI MOJA ni HELA YA MBOGA tu. Yote hii ilisabaishwa na kwamba CCM ililewa mno na Madaraka.

Ni kweli hao viongozi wa UKAWA uliowasema walikuwa CCM. Ndugu yangu sijui una umri gani (maana isije ikawa najadiliana na teenager hapa!!!) lakini jee unaelewa ya kwamba kabla ya mwaka 1992 tulikuwa na chama kimoja na ni CCM? Sasa ulitaka hao viongozi wa UKAWA watoke wapi kama si CCM. Unadhani Nyerere alikosea aliposema upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM ni kwa mahesabu hayo ndugu yangu!!!

Napenda tu kukufahamisha ya kwamba hao viongozi wote waliokuwa CCM na kuhamia UKAWA kwa sasa basi hawatekeleza tena MFUMO na ILANI zenu mbovu za CCM bali watatekeleza ilani za mfumo MPYA wa ukawa. Hata wewe Mwengeso Karibu UKAWA maana tunajua ukiwa huku UTANYOOKA tu. Mwisho kabisa utambue tu WATANZANIA wa leo sio wale wa mfumo ule wa ANALOGUE bali ni wa DIJITAL. Wewe baki na ushamba wako tu, wenzako wanakimbia wewe UNAPITWA kama umesimama vile.

#Badilika Mtanzania
 
Mwengeso sijui hujielewi au unalipwa kiasi gani kushabikia CCM. Tatizo la chama chako cha CCM si mtu mmoja mmoja bali ni MFUMO MZIMA uliokosa UADILIFU na UWAJIBIKAJI ambao ni tofauti na mfumo wa UKAWA. Serikali zote za CCM zilizopita basi zimeshindwa kabisa kumjali raia wa nchi hii. Zimeshindwa hata kumtimizia mtanzania japo zile haki zake za msingi (Kama Afya bora, elimu bora , maji safi, lishe bora n.k). Maisha ya mtanzania wa leo yamezidi kuwa duni wakati tuliahidiwa MAISHA BORA. CCM imeandaa mazingira ya kirushwa na kifisadi katika nchi hii kiasi ambacho kiongozi wa CCM anaona kama rushwa ya BILLIONI MOJA ni HELA YA MBOGA tu. Yote hii ilisabaishwa na kwamba CCM ililewa mno na Madaraka.
Ni kweli hao viongozi wa UKAWA uliowasema walikuwa CCM. Ndugu yangu sijui una umri gani (maana isije ikawa najadiliana na teenager hapa!!!) lakini jee unaelewa ya kwamba kabla ya mwaka 1992 tulikuwa na chama kimoja na ni CCM? Sasa ulitaka hao viongozi wa UKAWA watoke wapi kama si CCM. Unadhani Nyerere alikosea aliposema upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM ni kwa mahesabu hayo ndugu yangu!!! Napenda tu kukufahamisha ya kwamba hao viongozi wote waliokuwa CCM na kuhamia UKAWA kwa sasa basi hawatekeleza tena MFUMO na ILANI zenu mbovu za CCM bali watatekeleza ilani za mfumo MPYA wa ukawa. Hata wewe Mwengeso Karibu UKAWA maana tunajua ukiwa huku UTANYOOKA tu. Mwisho kabisa utambue tu WATANZANIA wa leo sio wale wa mfumo ule wa ANALOGUE bali ni wa DIJITAL. Wewe baki na ushamba wako tu, wenzako wanakimbia wewe UNAPITWA kama umesimama vile. #Badilika Mtanzania

Mfumo gani wa UKAWA wa kuwajibika kwa pamoja unao utetea. Wa Slaa na Gwajima (watumishi wa Mungu wanaokimbilia siasa wakawaacha kondoo malishoni) kuvuana nguo hadharani! Huo ndio UADILIFU na UWAJIBIKAJI. Wa waliotemwa na CCM kuongeza nguvu UKAWA ati wataleta mabadiliko! HAPANA kabisa. Kama ni WAADILIFU na WAWAJIBIKAJI usiwasemee, wajibu wenyewe kwa nini walichukua fomu kugombea ndani ya CCM kama ni chama kibovu kwa jinsi mnavyoking'onga.

Ebu 'annonymous' tueleze humu jamvini kama kweli wewe mwenyewe unatimiza wajibu wako? Kama wewe ni mwadilifu. Lakini kwa kuwa umejificha ndani ya jina la kificho, wewe si mwadilifu katu.

Samahani sikusemi wewe tu, nami najitizama, kwa nafasi yangu katika taifa hili, kama natimiza wajibu wangu ipasavyo. Ila kwa yule anayetaka kutuongoza ni lazima aanike uadilifu na uwajibikaji wake wazi, pasipo mashaka. Hao waliotemwa CCM hawafai kabisa kupewa uongozi wa nchi hii.

UKAWA irudi kwenye hali yake ya zamani ambapo tulianza kuwaamini kuwa ni wapinzani wa kweli. Lakini sasa wote ni wachumia tumbo. Annonymous, nikwambie hao viongozi wa UKAWA na mamluki wanataka nini! Uroho wa GESI na URANIUM.

Tuonane baada ya uchaguzi nikudhibitishie kuwa hao wote watakimbia nchi au watakuwa lupango wakisubiri hukumu yao kwenye mahakama ya mafisadi.
 
Baada ya tarehe 25/10 hao mafisadi utawasikia wakiwa jela, labda watoroke mapema. Wengine CHADEMA inawajua na itasaidia kuwataja zaidi ya wale 11 iliyokwisha kuwataja. Mashabiki na wanachama wa UKAWA, kama wewe, nanyi mnawafahamu kisa cha kusema CCM ni ya mafisadi. Hao hao mafisadi wa CCM watakamatwa kama walivyokatwa na wengine kuhamia UKAWA.

Sasa si watafungwa hadi maswahiba.
 
Mfano hai. Chukulia nina ondoka lakini nimekutafuta kutoka huko,nimekubeba kwa kadlili ya uwezo wangu wote, nina kukabidhi kiti. Mtoto wanguanahusika na wizi, biashara haramu, utamzuia kuendelea kutafuta ugali wake kituambacho kinaweza kupelekea kufa kwake? Je, Utamfunga? Huwezi kulipa fadhila? Jemwanangu huta mpa ofa ya Uwaziri pamoja na kwamba unasema unataka kufutautaratibu wa watoto wa vigogo kurithi madaraka?

Mimi nime wezesha chama kupata fedha za kutosha kutoka kwenyerasilimali za nchi kwa njia haramu au halali. Leo hii wewe umepata gharama zakuendesha kampeni, kuchapisha na kubandika mabango makubwa nchi nzima,matangazo kwenye vituo vya redio na runinga. Ukipata urais utaniweka pembeni?

Utawezaje kuchoma nyumba yenye viroboto ili hali wewe unaishi humo? Wewe utabaki salama?

Chambua vizuri pumba au mchele….

 
Mfano hai. Chukulia nina ondoka lakini nimekutafuta kutoka huko,nimekubeba kwa kadlili ya uwezo wangu wote, nina kukabidhi kiti. Mtoto wanguanahusika na wizi, biashara haramu, utamzuia kuendelea kutafuta ugali wake kituambacho kinaweza kupelekea kufa kwake? Je, Utamfunga? Huwezi kulipa fadhila? Jemwanangu huta mpa ofa ya Uwaziri pamoja na kwamba unasema unataka kufutautaratibu wa watoto wa vigogo kurithi madaraka?

Mimi nime wezesha chama kupata fedha za kutosha kutoka kwenyerasilimali za nchi kwa njia haramu au halali. Leo hii wewe umepata gharama zakuendesha kampeni, kuchapisha na kubandika mabango makubwa nchi nzima,matangazo kwenye vituo vya redio na runinga. Ukipata urais utaniweka pembeni?

Utawezaje kuchoma nyumba yenye viroboto ili hali wewe unaishi humo? Wewe utabaki salama?

Chambua vizuri pumba au mchele….


Hoja fikirishi.
 
Back
Top Bottom