Maoni: JF Members SACCOS LTD

Cybergates

JF-Expert Member
Dec 2, 2016
672
1,390
Hellow bosess!

Dunia ya saivi sio ya miaka ile ya 70 saivi technolojia ina impact kubwa tu kwa maisha ya saivi na baadae. Twende kwenye mada
Mkuu apo juu amekuja na wazo lakuanzisha Jf saccos kaeleza vizuri sana kuhusu wazo lake
maoni yangu kuhusu
1.Ku-rise fund
->umeeleza vizuri kuhusu michango ya member wa jf. Kwangu mimi ili ku rise fundi na kutengeneza mtaji cha kwanza alizima Saccos iwe na ushirika na main Jf (ya max mello) kwa ujumla ili member tupate usalama wa ela zetu tutakazo invest kwako
->Tuwe na app itakayo kua na sehemu kuu tatu au zaidi, moja ya hiyo sehemu iwe ni sehemu ya kununua na kuuza hisa za jf saccos. Kwa mfano Jf saccos itataka mtaji wa 2 au 3 billion tunaingia kwenye code tuna tengeneza share zenye dhamani ya 3bl kila share inakua inauzwa kwa labda elf 1 au elf 3 kila mwana jf ananunua hisa kulingana na uhitaji wake na uwezo wake lakini pia kwa wakati huo huo mtu apewe uwezo wa kuuza hizo hisa zake hapo hapo kwenye app alipo nunulia mfano mm cybergates nilinunua hisa kwenye app ya jf saccos za elfu 50 nikapata hisa 120 baada ya miezi mitatu nataka niuze hisa 60 nipate hela yangu so simply naingia kwenye app yangu ya jf saccoss upande wa buy and sell share na click sell naweka idadi ya share nazotaka kuuza 60(au zote 120) ni ki click done zile share zinaingia sokoni nasubiri msiko
Impact ya hiyo featuse
1.kwanza ili mtu aweze kujisajili kwenye app ya jf saccos lazima awe member wa jf (tutatumia database ya jf kupata member)
2.urahisi kwa kununua hisa itakua simple mtu akisha jisajili moja kwa moja anapata uwezo wa kuweka ela kwenye jf sacos walet yake kwenye app ambapo ateweza kufanya malipo mbalimbali kwenye app au ataweza kununua kupitia reference number(eg 555 333 kwenye mitandao ya sim mpesa), debit card au bank account moja kwa moja hapo hapo kwenye app
3.urahisi wa mtu kuuza share zake, hii itafanya mtu awena huhakika wa kupata hela alizo wekeza jf sacos kwa maana anajua taauza tu kirahisi kupitia app
4.usalama na uhakika wa kumonitor capital, itakua rahisi sana kwa jf sacos kujua ni mtaji kiasi gani wamepata hisa kisasi gani umeuza na za sh ngapi na pia zimebaki ngapi na za sh ngapi
inaendelea 1/4
 
Hapa ntaongelea kuhusu wings na wikundi ambayo vipo chini ya jf saccos
wings
kama ulivyo sema kutakua na wings alabda ya arusha, dodona na mwanza
kazi za wings
1. Ku perform logistic service
->kwa mfano kikundi cha jf saccos mbeya kimepata order ya kuleta organi vegetable hapa arusha kwenye hotel in large quantinty kazi ya wing mbeya ni kuhakikisha mzigo wa kikundi hicho cha mbeya unafika arusha salama salmini garama za usafiri zitagaramiwa na kikundi husika hii itafanya uhakika wa kikundi kuuza bidhaa zao popote pale tz kwa kuwepo na safirisaji kirahisi
2.to register vikundi eneo husika
-> hapo tuta import terms na condition (minimum member etc) za vikundi ambavyo vitakua chini ya wings ya eneo husika kila kikundi ninachotaka kupata mtaji kutoka jf saccos lazima kiwe kimesajiliwa china ya wings ya eneo husika au karibu yake hapa tuta reduce fraud ya vikundi na kuweza kuvi-monitor vikundi vyote vya jf saccos kwa kutumia hizo wings
3.kutoa mikopo
->wings itatumia kutoa na kufatilia mikopo kwa vikundi walivyo visajili ili kuhakikisha marejesho yanafanya kwa wakati
4. Kutafuta masoko ya bidhaa za vikundi
->hapa wings husika itakua inahusika tutafuta masoko kwa bidhaa za vikundi ambavyo vipo chini yao iwe ndani au nje ya nchi pia na pia kutoa seller id kwenye ecommerce ya jf saccos (ntaeleza post ya 3)
5.ku supply packing product
->hapa wings itakua na ulazima kutafuta na kuuza vifungashio vya bidhaa zinazo zaliswa na vikundi vilivy china yake
6.kutoa elimu kwa vikundi na kuvisimamia
->hapa wings itakua itakua na jukumu la kutoa elimu ya ujasiliamali kwa vikundi na kuvisimamia
inaendelea 2/4
 
Ecommerce
kama nivyo sema tutakua na app ya jf sacos hii app itakua sio ya kuuza na kununua share za sacoss pia itakua na ecommerce option. Itafanyaje kazi twende pamoja
1.ecommerce lazima iwe na seller na buyers hapa itakua ivi
seller
jf sacos itatoa seller id kwa vikundi ambavyo vimesajili chini ya wings zake hapa tutakua tumetoa opportunity kwa vikundi kupata market za bidhaa zake (usisahau logistic itafanywa na wings ya kikundi) na pia kulimit number of fraud product na pia fake seller na kuongeza usalama kwa buyer
buyer
hapa tutafanya simple buyer ni yoyote yule aliyekua register kwenye app yetu (ikiwa ni mwana jf ataweza kununua hisa na kuuza akiwa sio wana jf ataweza kununua bidhaa tu!). Hapa tutapata market ya watu na trust ivyo kuongeza demand na user demand
Payment
hapa mmunuzi ataweza kufanya malipo kwa njia kuu tatu au zaidi
1.kupitia hisa zake za jf sacoss
->hapa kama mnunuzi alikua na hisa za jf anaweza kutumia hisa zake ulipia product kwenye ecommerce ndani ya jf sacos app systeam ita convent hisa into cash (hapa tutacheza na code ili hisa zi be convented kama tuzo point za voda)
2. Kupitia mpesa, tigo pesa etc
->hapa tutatumia namba ya kampuni kwa maana hii mitandao haijiamini na security yake upande wa payment, hata tatumia systeam kama ya mbet user atapata slip number na kuifanyia malipo kupitia mpesa au tigo pesa
2.debit, credit cards na Bank account
->hapa haina haja ya maelezo kwa maana inaeleweka
3.paypal
->kwa ajili ya ku accept international payment
fullfillment
hizi fullfillment zitakua kama maduka ya jf huko mtaani kwa mfano mm nipo arusha nimenunua asali kutoka kikundi cha jf saccos kupita ecommerce kwe app kabla sijafanya malipo napata option ya kuchangua fullfillment iliyopo karibu yangu labda naselect fullfillment ya uzunguni jf saccos ffmemt sasa hapa jf wings itailazimu isafirishe bidhaa asali yaku kutoka bukoba hadi uzunguni ffment center ambapo mm mitaweza kwende kuchukua bidhaa yangu niliyo nunua hapa jf ecommerc bidhaa ikifika ntapata notification kwenye app kwamba mzigo umefika nikachukue. Na hizi ffment zitakua maeneo mbalimbali eg Tandale, mikocheni etc
inaendelea 3/4
 
Kuongezea apo kwenye app
1. Itakua na sehemu ya current news ili watu wapate update kirahisi
2. Itakua na information za kujisajili kikundi
3. Kupokea feedback
4. Na features nyingine nyingi (labda user kuona maeneo zilizopo wings, fullfillments etc)
5. Pia unaweza kuweka sehumi ambapo user wa eneo husika wanaweza kuunda kikundi au user kuomba kujiunga na kikundi flani (inamaanisha kutakua na profile ya kila kikundu kutoka wings zote za jf saccos)

hayo ni maoni au nyongeza inayoweza kutumia kuhakikisa ndoto yako ya saccos inatimia kama itakupendeza unaweza kutumia hayo maoni yangu hayana copyright ni free to everyone good luck mkuu
C.c mkuu mwenye mada
mwingine anaweza kuongezea hapo kwenye maoni yangu ili kumsaidia huyu mkuu, mm nimefikia mwisho hapa
mwisho 4/4
 
Hahaa Hii Topics naona kila mara inaibuliwa.

Hii kitu ili oparate na baadae ikafa.

Kuendesha vitu kama hivi si kazi ya kitoto i ahitaji commitment mno.

Na Pia ili mfanikiwe lazima muwe na Common interest yaani mawazo yanayo fanana.

Ndo maana kuna SACCOS ya wafanyakzi mara wa Bandali au TANESCO na ladhika. wale wana common yaani wana kitu kinawaunganisha pamoja ambacho ni wao kuwa wafanya kazi wa TANESCO.

Watu kama wafuga kuku au wafuga Ng'ombe wa maziwa wanaweza kuwa na SACCOS yao kwa sababu wana common things.

Sasa humu tunaongelea SACCOS kwanza kwa ID Feki na hapo tu ni Disqulification tiyari hakuna atate trust.

Pia humu kuna watu wako pembe kuu za Tanzania wapi wakulima, wapo wafanyabiasha tofauti wapo wasio kuwa na kazi wapo Wajeda na wapo wanafunzi.

Huu mchanyato ni mgumu sana ku oparate SACCOS.

Kwa Dunia ya sasa kuna Systema zimetengenezwa unaweza run SACCOS bila hata kufanya vikao yaani kila kitu kina kuwa online ila hii haiondoi kwamba lazima muwe na kitu common.

Na ikishindikana kitu common basi angalau watu wa eneo fulani mji fulani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom