Maombi ya Msaada kwa wanabodi wote

Maombi ya Msaada kwa wanabodi wote

Joined
Sep 27, 2015
Posts
78
Reaction score
19
Habari za muda wanabodi wote natumaini ni wazima wa afya njema pole na majukumu ya hapa na pale.bila kupoteza muda kama kichwa cha habari hapo juu kinavyojieleza, nakuja mbele yenu kuomba msaada wa kimawazo na vitendo ili niweze kufanikiwa.

Mimi ni kijana naishi jijini dar es salaam, kilichonifanya nichukue nafasi hii ya kuandika Uzi huu ni matatizo yanayonikabili naombeni mnisaidie ili niweze kuyatatua japo hata nusu yake.

Nilikuwa nafanya kazi kwenye shirika lisilo la kiserikali, kutokana na matatizo ya kiuchumi shirika lilishindwa kujiendesha na kupelekea kupunguza wafanyakazi kitendo hicho kimeniadhiri sana mimi kwani kimeweza kunirudisha nyuma. Kwani hapa nilipo nadaiwa kodi ya nyumba ambayo natakiwa nilipe sina pesa.

Kwahiyo nawaomba wanabodi jambo mnisaidie ili niweze kulitatua tatizo ili maana linaninyima raha sana hata kama kuna mtu anakijisehemu japo cha mimi kuweza kufanya kazi na kufanikiwa kulipa hii pesa ya watu nitashukuru sana. Naomba msaada wenu.

Asante sana kwa ushirikiano wenu.
 
Hata kama umeathirika kwa kupunguzwa kazini,hebu tupe biography yako,unaweza kufanya kazi gani,elimu yako,uzoefu,unaishi wapi,umeoa/kuolewa??????
Funguka zaidi watu wakujue zaidi!!
Kila la heri!!!))
 
Hata kama umeathirika kwa kupunguzwa kazini,hebu tupe biography yako,unaweza kufanya kazi gani,elimu yako,uzoefu,unaishi wapi,umeoa/kuolewa??????
Funguka zaidi watu wakujue zaidi!!
Kila la heri!!!))
Elimu yangu kidato cha nne, certificate of business administration, uzoefu wa kazi sales and marketing, mkufunzi wa vicoba, naishi Gongo la mboto jiji dar es salaam, nimeoa ila sina mtoto wakuu.
 
Sales & Marketing kwenye eneo gani?
Maana kuna Sales &Mkt hata kwenye kuuza majeneza!
Ulisoma shule za kata nini mbona huwezi kujieleza mkuu!!
Ulipataje mke(joking!)
Huna mtoto,ungependa kusaidiwa kupata mtoto??
 
Sales & Marketing kwenye eneo gani?
Maana kuna Sales &Mkt hata kwenye kuuza majeneza!
Ulisoma shule za kata nini mbona huwezi kujieleza mkuu!!
Ulipataje mke(joking!)
Huna mtoto,ungependa kusaidiwa kupata mtoto??
Mkuu ni kweli sale inauwanda mpana inategemea na kampuni unayokuwa nayounaifanyia kazi pia kwenye hilo unakiwa unatafuta masoko na kutangaza bidhaa kwa Wateja ambao awajafikiwa na Huduma hyo mkuu na kuhusu swala la mtoto sijasema nisaidiwe kutafuta.
 
Back
Top Bottom